1- Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) anawaelekeza waumini wajitahidi na kushindana kutenda mema kabla fitina kubwa haijaingia, itakuwa ni mfano wa usiku mweusi wenye kiza totoro, hakuna mwezi wala mwanga, haionekani haki wala batili. amesema Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake): “hakika huu Umma wenu, salama yake iko mwanzoni, huko mwisho watapatwa matatizo na mambo ambayo mtaona kweli ni mabaya, inakuja fitina inafikia hatua wanaanza kutekana na kufanyana watumwa wao kwa wao, inakuja fitina, muumini anasema: hii inaniangamiza, hii inaniangamiza. Kisha inaondoka. Inakuja fitina, muumini anasema: hii sasa ndiyo inanimaliza”[1]. Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) ameamrisha kujitahidi kufanya mema kabla fitina haijaingia na kuenea; kwa sababu katika kipindi cha fitina ibada inakuwa nzito sana, kwani nafisi inajishughulisha na fitina jambo ambalo linapelekea ibada kudhoofika, na ndio maana Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) akasema: “Ibada katika kipindi cha fitina, ni sawa na kuhama kuja kwangu”[2] yaani mji wa Madina. Na akasema: “itafikia zama mtu atakae vumilia kuishika Dini yake, ni kama mtu aliye shika kaa la moto”[3]
2- Kisha Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) akaeleza kwamba, fitina hizo zina uwezo mkubwa wa kumshambulia mtu, kiasi kwamba zinamtoa mwislam katika dini yake haraka sana, ni kama tu ni ndani ya mchana mmoja. kwa sababu nyoyo ni nyepesi kubadilika na kuiacha haki, zinapenda sana upotevu, zikikosa ndani yeke kinga, zinapata maradhi mabaya na kuziua”[4]. Kwa kuwa mitihani na matatizo ikikithiri kwenye nafsi inaziharibu kwa kuzizidia na kuzisababishia kuwa ngumu[5].
3. Kwa hali kama hiyo, mtu anaweza kuiuza dini yake kwa kitu kidogo katika Dunia, inaweza kuwa ni mali au cheo au vinginevyo katika mapambo haya ya Dunia yenye kuisha
MAFUNDISHO
1. Pupia kufanya mema, kama ibada, kusoma, kufundisha, kuoa, kuunganisha ndugu na mengineyo. Usiendekeze matarajio kwa kujichelewesha mpaka kesho au kesho kutwa, au kwa kusema, nikikuwa, au nikipata kitu fulani. Mitihani ambayo inamkwaza mtu kutekeleza dini yake na ibada zake inaweza ikateremka, pupia kwa juhudi kabla vikwazo havijashuka.
2. Mara nyingi mtu hafanyi ibada kwa sababu anataka afikie kiwango anacho kiwaza, nikama mtu anachelewesha kusambaza kitabu kwa kusubiri kila kitu kitimie, au anachelewesha kumapatia mke wake zawadi mpaka ikamilike, au hasomi Qur`an wala hasikilizwi mpaka ajiweze, ataendelea kuahirisha mpaka anabanwa na majukumu, au anakata tamaa au vinginevyo. Lau angelifanya anacho kiweza, angelipata wepesi kwa kiasi kikubwa.
3. Kuwa msitari wa mbele katika mambo mema ni ustadi, anajifunza mwanadamu kwa kukithirisha kuwa msitari wa mbele yeye mwenyewe, itakuwa ni kazi ngumu mwanzoni na ataichukia, kisha baada ya muda itakuwa nyepesi, inamvutia kuifanya kadri awezavyo. Jizoeshe kuwa mstari wa mbele kwa matendo mema, na uhesabu ni mara ngapi umekuwa mstari wa mbele kwa kutoa maneno mazuri, au sadaka au kusaidia mtu kwa tatizo lililo mpata bila matarajio, sawasawa ni ndugu au si ndugu.
4. Jikurubishe kwa Mwenyezi Mungu ukiwa na raha, atakukumbuka ukiwa na matatizo. kuwa msitari wa mbele kwa matendo mema pindi unapokuwa na wasaa, afya na unajitambua. Namuomba Mwenyezi Mungu akulinde na fitina.
5. Inatakiwa mwislaam akithirishe kumuomba Mwenyezi Mungu amjaalie ashikamane na dini yake, na asimpatie mitihani; Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) mara nyingi alikuwa akisema: “Eh Mwenye kubadisha nyoyo, ujalie moyo wangu ushikamane na dini yako”[6].
6. Mwanadamu anapokuwa amezama katika fitina, huenda asitambue kwamba anauza dini yake, anaweza kupuuzia miamala ya kifedha, au ardhi, kwa kuzidishiwa ambacho si haki yake, au huenda akasengenya, au akaacha kusengenya ili kumridhisha tajiri yake. Jifuatilie mwenyewe na ujitathmini, na wala jicho lako lisitizame panapo dhuru Imani yako, Dini ndio kitu cha thamani zaidi.
7.Amesema mshairi:
Kuwa msitari wa mbele madamu umri bado upo***uadilifu wako unakubalika na ulicho kitoa ni cha thamani .
Jitahidi, pupia na utumie ujana***kwani ni muda unaoweza kuutumia ukafaidika. Fanya haraka, kwani kifo kiko nyuma yako kinakuja kwa kasi***haiwezekani hata kidogo kukikwepa au kukishinda.
Marejeo
- Muslim (1844), kutoka kwa Abdullah bin Amr bin Al-Aas, Mungu awe radhi nao
- .Muslim (2948),kutoka kwa Ma’qil ibn Yasar
- Al-Tirmidhiy (2260), kutoka kwa Anasa
- l'iifsah an ma`ani alsahahi" cha Ibn Hubayrah (8/163).
- “Al-Mufhim lamaa 'ushakil min talkhis kitab Muslim” cha Al-Qurtubi (1/326)
- . Ahmad (12107), al-Tirmidhiy (2140), na Ibn Majah (3834).
1. Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) anabainisha na kutahadharisha juu ya jambo hatari lenye kubatilisha ibada, ameliita ushirkina mdogo, ili kutofautisha kati yake na shirki kubwa inayo mtoa mtu katika Uislamu.
2. Wakamuuliza kuhusu ushirikina mdogo; kwa sababu ushirikina unajulikana, nao ni kumuwekea Mwenyezi Mungu mshirika katika mambo ambayo hakuna anaye stahiki zaidi yake. Kutofautisha kati ya ushirikina mdogo na mkubwa inahitaji ufafanuzi zaidi au mfano ili kuweka wazi zaidi.
3. Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) akawaeleza kwa mfano ili kuwaweka wazi zaidi, na kwamba jambo analo lihofia zaidi kwenu nyinyi ni riyaa; maana yake ni mtu kudhihirisha ibada kwa watu wafahamu, ili wamtaje vizuri na kumsifia. Huu ndio mfano wa ushirikina mdogo, na mifano mingine ni kuapa kinyume na Mwenyezi Mungu, mtu kusema: ametaka Mwenyezi Mungu na fulani, kuitakidi mikosi, ruqya zisizo kuwa nzuri na mengineyo yasiyo ondoa asili ya Tawhiid kwa kwenda kinyume kabisa, japo kuwa ni aina ya ushirikina [1].
Ijulikane kwamba mambo haya yanaweza kupelekea katika ushirikina mkubwa, kwa sababu mtu anapo apa kinyume na Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kuitakidi kuwa ni kitukufu, au akimkubali kuhani kwa kudai kwamba anajua ghaibu, na riya ikiwa katika ibada zake zote, au ipo katika kiini cha itikadi yake, au akidhani kwamba hirizi na ruqya ndio vinazuia madhara na kuondoa maradhi, haya yote ni katika ushirikina mkubwa [2] .
4. Kisha Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) akasema kwamba, Mwenyezi Mungu atawaadhibu siku ya kiyama baada ya kuwalipa viumbe, wao wakiwa wanasubiri malipo ya ibada walizo zifanya kwa riya.
5.Mwenyezi Mungu atawambia; nendeni kwa mlio kuwa mnafanya ibada mbele yao ili wawaone na kuwasikia, muone, je mnapata malipo ya ibada zenu? Na hii ni kuwadhihaki na kuwadhalilisha. Mwenyezi Mungu Mtukufu atabatilisha matendo yao mema
amesema Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake):
“amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Mimi nimetosheka na washirikina kwa ushirikina wao, yeyote atakae fanya ibada akanishirikisha na chochote, ninamuacha na ushirikina wake”[3].
Lengo analolifikia anae fanya ili watu wamuone, ni kupata sifa kidogo, kisha inafuatia fedheha
amesema Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake):
“mwenye kufanya ibada ili asikike, Mwenyezi Mungu atamfanya asikike, na mwenye kufanya ibada ili aonekane, Mwenyezi Mungu atamfanya aonekane”[4].
Yaani mwenye kukusudia katika ibada yake watu, Mwenyezi Mungu atawafanya waione na kuisikia. Na hayo ndio yatakuwa malipo yake, na huenda Mwenyezi Mungu Mtukufu akamdhalilisha na akadhirishia watu maovu yake asiyo penda yajulikane [5] Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) ameeleza kwamba, wakwanza kuchomwa moto siku ya kiyama, ni mtoa sadaka, msoma Qur`ani na anaye ipambania Dini, sababu walifanya hayo ili waonekane, matendo yao yakabatilika na wakakosa malipo [6].
MAFUNDISHO
1. Fuata muongozo wa Mtume wako (Rehma na Amani ziwe juu yake) katika kuwafundisha watu. Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) ametumia usulubu wa kumfanya mtu aogope na akaweka wazi nasaha mwanzo wa maneno yake, alipo sema (Rehma na Amani ziwe juu yake): “Hakika ninalo ogopea kwenu zaidi”. Ufikishaji wa namna huu unamfanya mtu awe makini na kuhudhurisha akili na usikivu wake, ni bora zaidi kwa anaye toa nasaha atumie usulubu wa kumtamanisha mtu, na kunfanya awe makini.
2. Ushirikina ulio jificha, unaweza kuharibu moyo bila mtu kujua, kwa sababu ameghafilika, mtu anaweza kuingia katika sala au kumtaja Mwenyezi Mungu, au kusoma Qur`an, au kutoa sadaka au mengineyo, akaona watu, akataka waone ibada yake na wasikie sauti yake, kama akipambana na nafsi yake na kuliondosha moyoni kadri awezavyo, halita athiri ibada yake, ama akiendekeza na akabadili niya yake kwenda kwenye riya, ibada hiyo itabatilika. Jifuatilie mwenyewe, na jizoeshe kuwa na Ikhlaas.
3. Twalhat bun Muswarrif -Mwenyezi Mungu amrehemu- alikuwa ni msomaji mzuri wa Qur`ani wa eneo la Kufa, alipo ona kuna watu wengi wanamkubali, aliogopea riya, akaenda kwa A’mash akamsikiliza Qur`ani, watu wakamkubali A’mash na kumuacha Twalhat. Huenda Twalhat [7] alikusudia kuwaonyesha ubora A’mash na wala wasikimbile kwake tu ikampelekea kubadilika, kwani malengo yake ni watu wafaidike.
4. Mja anaweza kudhihirisha ibada, si kwa ajili ya riya, bali anatakata kudhirisha alama za Mwenyezi Mungu, au kuhuisha Sunna iliyo sahaulika,yaani mafundisho ya Mtume, au anafanya ili watu wajifunze kwa vitendo na waathirike, hayo si katika kutaka kujionesha. Riya ni lengo la mtu katika ibada iwe ni watu wamuone ikhalaas, unyenyekevu na ibada yake, na akarizika na hayo.
5. Katika vitu vinavyo weza kusaidia kuondoa riya ni kukumbuka jinsi utakavyo kuwa mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, kumtegemea kiukweli na kumuomba akukinge na riya. Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) alikuwa akiwatahadharisha maswahaba zake dhidi ya riya, na kuwaamrisha wamuombe Mwenyezi Mungu awakinge.
Kutoka kwa Abuu Musa al Ash’ariy (Radhi za Mwenyezi ziwe juu yake), amesema:
siku moja Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) alituhutubia, akasema: “Enyi watu, ogopeni huu ushirikina, kwa sababu umejificha kuliko vishindo vya sisimizi” mtu mmoja aliye kadiriwa na Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu; tutaiepuka vipi na hali ya kuwa imejificha kuliko kishindo cha sisimizi? Akasema: “semeni: “Eh Mwenyezi Mungu hakika sisi tunakuomba utuhifadhi tusikushirikishe na chocho tunacho kijua, na tunakuomba msamaha kwa tusicho kijua”[8]
6. Mja anaweza akafanya ibada yoyote kwa ikhlaas, kisha watu wakamuona na kumsifia, akafurahi. Hii haitii dosari ibada yake, na haizingatiwi kuwa ni riya, madamu aliifanya kwa ikhlaas.
Kutoka kwa Abuu Dharri, amesema:
Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) aliulizwa: inakuaje mtu akifanya amali njema watu wakamsifia? Akasema: “hiyo ni bishara ya mapema iliyo njema kwa muumini”[9].
7. Si katika riya mtu kuhamasika kwa kuwepo watu wema, au kuona aibu na kuacha maasi, au akajitahidi kufanya baadhi ya ibada bila kukusudia sifa zao. Hizo ni katika faida za kuwa karibu na watu wema.
8. Mwenye kufanya riya lau angelitizama kwa makini, angeliona kwamba wote anao fanya ili wamuone, hawaoni thamani ya anacho kifanya, wanamsahau baada ya kumaliza, au huenda wakatizama jinsi anavyo fanya riya wakamdharau kwa kuzidisha, au Mwenyezi Mungu kumuazibu kwa fedhea, njia bora ya kuokoka ni kumkusudia Mwenyezi Mungu pekee.
9.Amesema mshairi:
Amepata hasara mwenye kufanya ibada bila kumkusudia Mola wake***anafanya kwa unafiki, hivi kuna unafiki baada ya riya?!
Utapata ulicho tanguliza na kukiwekeza***kama ulivyo fanya, tambua kwamba malipo ni kama ulivyo fanaya.
10.Amesema mwingine:
Eh nafsi usisahau fadhila za Mwenyezi Mungu***kukupa nguvu ni ufalme kwangu na kuniacha ni kuangamia kwangu. Kishindo cha sisimizi juu ya mwamba katika giza***hakijajificha sana kuliko riya na ushirikina
Marejeo
- Tazama: “Al-Tawhiyd” cha Ibn Rajab (uk.: 23), “Sherh ya Kashf al-Shubahat, ikifuatiwa na Sharh al-Usul al-Sittah” na Ibn Uthaymiyn (uk.: 115)
- .Tazama: “Fath Dhu’l-Jalal wa-Ikram sherh Buloogh Al-Maram” cha Ibn Uthaymiyn (6/357)
- .Muslim (2985), kutoka kwa Abu Hurairah
- .Muslim (2986), kutoka kwa Ibn Abbas, Mungu amuwiye radhi
- .Tazama: “Sharh Sahih Muslim” cha Al-Nawawi (18/116), na linganisha: “Fath Al-Bari” cha Ibn Hajar (11/345)
- .Muslim (1905), kutoka kwa Abu Hurairah
- ."Sayd al-Khater" cha Ibn al-Jawzi (uk. 292)
- .(Ahmad (19109
- .Muslim (2642).
Unafiki ni katika maradhi hatari yanayo mpata mtu mmjo mmoj na jamii kwa ujumla, ndio maana uislam ukatadharisha sana na kubainisha sifa za wanafiki, ili muumini achukue taahadhari, na ajichunge asije kusifika kwa tabia zao.
1.Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) amewatajia maswahaba zake sifa nne ambazo hasifiki nazo mwislam, bali ni za mnafiki, mtu anapo kuwa nazo zote, nakuwa mnafiki kikamilifu.
Unafiki; ni mtu kudhihirisha kinyume na alicho nacho moyoni, na unagawanyika mara mbili; unafiki wa itikadi; ni mtu kudhihirisha uislam na kuficha ukafiri, huu unamtoa katika uislam.
Na hao Mwenyezi Mungu amewasema katika kauli yake:
““Hakika wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa Motoni, wala hautowapatia yeyote wa kuwanusuru (145) Isipo kuwa wale walio tubu, na wakatengeneza na wakashikamana na Mwenyezi Mungu, na wakaitakasa Dini yao kwa Mwenyezi Mungu. Basi hao watakluwa pamoja na Waumini. Na Mwenyezi Mungu atakuja wapa Waumini ujira mkubwa” .”
[An-Nisa: 145, 146]
. aina nyingine ni unafiki wa matendo; kama uongo na kusaliti, kama ilivyo tajwa kwenye Hadithi. Huu haumtoi mtu katika Uislam, lakini ana kuwa na sifa miongoni mwa sifa za kinafiki, na mwenye nazo anafanana na wanafiki na ameahidiwa adhabu ya Moto
akesema:
“jiepusheni na uongo kwani uwongo unampelekea katika uchafu na uovu, na uovu unapelekea kuingia Moto, na mtu atasema uongo mpaka aandikwe kwa Mwenyezi Mungu kuwa ni mwongo."[3]”.
Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) aliona katika ndoto mtu anavuta mdomo wake mpaka kwenye kisogo na kuujeruhi, na pua lake mpaka kwenye kisogo na kulijeruhi na macho yake mpaka kwenye kisogo na kuyajeruhi, akauliza, akaambiwa: ni mtu anaeongea uongo unachukuliwa mapaka unaenea sehemu mbali mbali”[4].
5.Sifa ya tatu: ni kusaliti makubaliaono. Anapo weka ahadi ya makubaliano na mtu anamhadaa kwa kumsaliti. Mwenyezi Mungu ameharamisha usaliti na ameukataza sehemu zaidi ya moja katika Qur`ani.
Amesema Mtukufu:
““Na timizeni ahadi ya Mwenyezi Mungu mnapo ahidi, wala msivunje viapo baada ya kuvithibitisha, ilihali mmekwisha mfanya Mwenyezi Mungu ndiye mdhamini wenu. Hakika Mwenyezi Mungu anayajua myatendayo” ”.
[An-Nahl: 91]
Na akesema Mtukufu:
“Na timizeni ahadi. Kwa hakika ahadi itaulizwa”
[Al-Isra: 34]
6.Sifa ya nne: ni mtu kuiacha haki katika ugomvi, na kutumia hila kuirudisha na kujaribu kuchukua ambacho si haki yake, hasa anapokuwa na uwezo wa kuongea na kusimamishaa hoja.
Mwenyezi Mungu amewaamrisha waja wake uadilifu katika kila jambo, na akawazuia wasisukumwe na chuki za ugomvi wakadhulumu upande fulani
amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
“Enyi mlio amini! Kuweni wasimamizi madhubuti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mkitoa ushahidi kwa haki. Wala kuchukiana na watu kusikupelekeeni kutofanya uadilifu. Fanyeni uadilifu. Hivyo ndio kuwa karibu mno na uchamngu”
[Al- Maaidah: 8].
Na Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) ameeleza hatima mbaya ya anae chukua haki ya mwenzake kwa dhuluma, akasema: “hakika nyinyi mnashtakiana kwangu, huenda baadhi yenu wakawa na ufasaha wa uwasilishaji wa hoja zao kuliko wengine, nikahukumu kuwa ameshinda kwa mujibu wa nilivyo sikia, yeyote ambaye nitampa haki ya mwenzake hata kidogo, basi asiichukue, nitakua namkatia sehemu katika Moto”[5] Mambo haya manne yanakusanya misingi ya unafiki, na kuna sifa nyingine ambazo zinatokana na hizi, kama kutotekeleza ahadi[6]. Alama za unafiki na sifa zao ni nyingi, asili yake ni hizo, inatakiwa mwislam ajitahidi asiwe na sifa yoyote katika hizo.
MAFUNDISHO
1.Miongoni mwa njia nzuri za Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) za kufundishia, ni kusogeza mukusudio kwa kutumia njia mbali mbali, kama vile idadi. Mwislam anapo sikia kwamba sifa zitakazo tajwa ni nne, anapata hamu ya kuzisikia na kuzikalili. Inatakiwa wasomi na wanao lingania watumie njia kama hizi wakiwa wanazungumza na watu
2.Unafiki ni sifa mbaya sana, na kila sifa yake pia ni mbaya, aliye mkweli na ana anajitambua hujiepusha na sifa hizo na wala hajitakasi, amesema Ibun abii Mulaikah -miongoni mwa wanafunzi wa maswahaba-: “niliwadiriki maswahaba thelathini wa Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake), wote wanaogopa unafiki usije ukawapata, hayupo anae sema: yeye ana Imani kama ya Jibril na Mikael”[7].
3.Inatakiwa ewe mwenye majukumu, uwe makini na amana unazo kabidhiwa. Sawa sawa kutoka kwa wazazi au wakubwa wako kazini, au marafiki zako, ukihitajia kuandika ili usisahau, au usipoteze, basi andika. Baadhi ya wema walio tangulia walikuwa wakidhibiti kila amana hata kama ni kalamu, au pesa ndogo ya mtoto.
4.Kutekeleza amana ni miongoni mwa sifa nzuri, washirikina katika mji wa Makka walikuwa wakimuita Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) Muaminifu, kwa sababu ni jambo linalo hitaji kujikaza, umakini na kupupia, jitahidi uwe hivyo.
5.Jizoeshe kuwa mkweli hata kama ni katika mambo madogo, tabia ya ukweli ni mazoea, usiseme uongo kwa kisingizio cha mzaha, au kuliwazana, au maslahi, jambo hili halihitaji vitu kama hivyo. Mtu anakuwa na tabia ya uongo mpaka inakita katika damu yake, inakuwa ni kazi kuiacha, kiasi cha kujulikana kwa tabia hiyo katika jamii. Inasimuliwa kwamba Abuu Sufiyaan alitaka kumndanganya Hiraqil kuhusu Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake), lakini aliacha, na alikuwa bado ni kafiri.
6.Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) ameamrisha kutekeleza ahadi hata kama ni washirikina tena katika kipindi cha vita. Hudhaifa bun Yamaan na baba yake, walikuja kwa Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) katika kipandi cha vita ya Badri, wakasema kwamba washirikina waliwachukuwa na kuwauliza, je mnataka kwenda kwa Muhammadi ili mshiriki nae vita?, wakajibu; hapana, sisi tunaenda Madina. Wakachua ahadi ya makubaliano kwamba waende Madina na wala wasishiriki vita na Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake). Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) akawambia: “ondokeni, tunatekeleza makubaliano yao, na tunamuomba Mwenyezi Mungu msaada”[8]. Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) hakuwaamrisha washiriki nae vita kuwapiga makafiri kwa ajili ya kutekeleza ahadi
7.Msaliti asifurahi kwa kufaulu, wala matarajio anayo yatarajia kwa usaliti wake, atambue kwamba mwisho wake ni fedheha kubwa.
Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) amesema:
“kila msaliti anabendera, itasimikwa kwa ajili ya usaliti wake siku ya Kiyama”[9].
Hata kama Msaliti akijua namna ya kupangilia na kuratibu mambo yake, ili asifedheheshwe mbele ya watu, je ataenda wapi siku ya Kiyama na bendera imesimikwa kuonyesha usaliti wake mbele ya viumbe wote?!
8.Usijitafutie sababu ya kufanya hiyana, au uongo , au usaliti, au kuvuka mipaka katika ugomvi, hata kumfanyia aliye kufanyia, tambua kwamba mwislam anafuata maamrisho ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na wala si matamanio yake.
Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) amesema:
“Tekeleza amana kwa aliye kuamini, na wala usimfanyie hiyana aliye kufanyia hiyana”[10].
9.Amesema mshairi
Achana na tabia za watu wasio kuwa na tabia njema***shikamana na tabia za watu bora na wenye adabu
Ukiombwa ufanye usaliti au ukiamrishwa***kimbia ujiokoe kukimbia kwa milele.
10.Akasema mwingine:
Ukweli anauzoea mkarimu mwenye matarajio ya kukutana na Mwenyezi Mungu*** na uongo anauzoe dhalili aliye feli. Achana na muongo, na usimfanye kuwa rafiki yako***hakika muongo ni rafiki mbaya.
Marejeo
- Ufafanuzi wa Al-Nawawi juu ya Muslim (2/47)
- .""Fasihi ya Kinabii"" cha Muhammad Abdul Aziz al-Khouli (uk. 18)
- .Al-Bukhari (6094), na Muslim (2607), kutoka kwa Ibn Masoud
- .Al-Bukhari (6096), kutoka kwa Samra bin Jundab
- .Al-Bukhari (2680), na Muslim (1713), kutoka kwa Ummu Salamah, Mungu amuwiye radhi
- .Al-Bukhari (33), na Muslim (59), kutoka kwa Abu Hurairah
- .Al-Bukhari akielezea, Kitabu cha Imani, Sura: Hofu ya Muumini juu ya matendo yake kubatilika bila kujua
- .Muslim (1787)
- .Al-Bukhari (3188) na Muslim (1735)
- .Abu Daawuud (3534).
Hadithi hii ni miongoni mwa Hadith muhimu za Sharia, ambazo zimebeba hukumu nyingi na kanuni za ulimwengu, na ndio maana Imam Ahmad – Mwenyezi Mungu amrehemu – akasema: “Misingi ya Uislamu ni Hadith tatu: Hadithi: “Vitendo vitalipwa kwa kuzingatia nia,” na Hadiyth: “Mwenye kuingiza kitu katika mambo yetu kisichokuwamo, basi hatapokelewa.” Na Hadithi: “Halali iko wazi na haramu iko wazi. [1]Katika Hadithi hii, Mtume rehma na amani zimshukie anataja kwamba kufuata ni sharti la kukubaliwa matendo; Mwenye kuzua jambo lisilo na msingi wowote katika dini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na Sunnah za Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie; linakataliwa na kurudishiwa mwenye nalo, na hatalipwa ujira wala thawabu, bali hiyo ni aina ya kughushi kwa kupinga muongozo wa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake.
Na uzushi ni: kufanya jambo ambalo limezushwa bila ya ushahidi wa kisharia, sawa sawa liwe la kiitikadi - kama kukataa qadar, na kuamini kuwa maiti wananufaisha - au katika ibada, ambayo ni kuabudu kwaa njia ambayo hakuifundisha Mtume rehma na Amani zimshukie, kama vile kusherehekea siku ya kuzaliwa Mtume na kuzua nyiradi na dua zisizo na msingi katika kitabu na Sunnah. Na kuchagua masiku maalumu kwa kuyahuisha, Kama vile kuswali usiku wa katikati ya Sha’ban, na mambo mengine yanayosababishwa na kutojua sheria, bali ni kufuata matamanio, kuwaiga wasiokuwa Waislamu, na kutanguliza akili juu ya Sharia.
Mwenyezi Mungu Mtukufu ameonya dhidi ya kufuata matamanio na uzushi katika dini;
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
“Wala msiwe kama wale waliofarikiana na wakakhitalifiana baada ya kuwajia hoja zilizo wazi, na hao watapata Adhabu kali na chungu”.
[Al Imran: 105]
Amesema Qatada, Mwenyezi Mungu amrehemu: “Wale waliofarakana na kukhitalifiana ni watu wa bidaa.” Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, amesema: “Nyuso za watu wa Sunnah zitakuwa nyeupe. na nyuso za watu wa uzushi zitakuwa nyeusi.”[2]
Na Mwenyezi Mungu amewalaumu washirikina kwa uchambuzi wao na kuharamisha kwao bila ya amri kutoka kwake, na ametakasika
Mwenyezi Mungu aliyesema:
“Sema: je, mnaonaje riziki alizo kuteremshieni Mwenyezi Mungu, kisha mkajaalia miongoni mwake halali na zingine haramu. Sema uwaambie: je, Mwenyezi Mungu amekuruhusuni kufanya hivyo, au mnamzushia Mwenyezi Mungu uongo” .
[Yunus: 59]
Na Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na Amani zimshukie alikuwa akisema katika utangulizi wa khutba zake: “Mwongozo ulio bora kabisa ni uwongofu wa Muhammad, na mambo mabaya zaidi ni mambo yenye kuzuka, na kila uzushi ni upotofu. ”[3]
Na akawausia maswahaba zake, akasema Mtume amani iwe juu yake:
“Mshikamane na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa waongofu. Mzishikilie vilivyo na kuziuma kwa magego, jiepushe na kuzusha katika dini, uzushi wowote ni upotevu, na kila jambo la kuzuka ni mbaya [4]
Bali Mtume rehma na Amani zimshukie alitahadharisha dhidi ya uzushi katika dini kwa kuwa mataifa yaliyopita yaliangamizwa kwa sababu hiyo. Mayahudi na Wakristo walibadilisha sheria na kudai kuwa Uzair na Masihi ni wana wa Mungu, na wakasema: Sisi ni wana na vipenzi vya Mwenyezi Mungu. Na wakaipotosha Taurati na Biblia, wakapuuza mipaka, na wakaidanganya Sharia kwa akili zao.
Hadithi hii inawakanusha wale wanaodai kuwa baadhi ya uzushi ni mzuri. Mtume, amani iwe juu yake, aliamuru kwamba kila kitendo kilichoundwa hivi karibuni kitakataliwa, na hii inajumuisha uzushi na vitendo vipya vilivyo zushwa. Ama kauli ya Umar Mwenyezi Mungu awe radhi naye “uzushi mzuri ndio huu” pale watu walipokusanyika katika swala ya tarawehe nyuma ya imamu mmoja, ambaye ni Ubayy bin Ka’b Mwenyezi Mungu amuwiye radhi [5]; Alitaka tu iwe bid’ah kwa maana ya kilugha, na ni kila jambo lililozuliwa hivi karibuni, liwe lina msingi katika dini au la. Kufanya kwake Ka’b Mwenyezi Mungu amuwiye radhi hakutokani na uzushi; kwani Mtume rehma na Amani zimshukie aliwaongoza watu kuswali kwa siku nyingi, kisha akaiacha kwa kuhofia kuwa italazimishwa kwa Waislamu. Mtume rehma na Amani zimshukie alipokufa na kukatika wahyi, yale aliyoyaogopea yaliondoka, na kitendo cha Umar kilikuwa kwa mujibu wa Sunnah zake, amani iwe juu yake [6].
Na Mtume, Rehema na amani ziwe juu yake, alibainisha uzushi kwa kusema: “Katika jambo letu hili” alimaanisha dini, inaashiria kuwa uzushi na uvumbuzi katika mambo ya dunia sio wa kulaumiwa wala haramu; Uvumbuzi na uundaji wa mashine ni jambo la kupongezwa ambalo hurahisisha watu kutimiza masilahi yao.
MAFUNDISHO
1.Hadithi hii ni kanuni kubwa katika misingi ya Uislamu, nayo ni sawa na mizani ya kupima matendo, sawa na Hadithi isemayo: “Matendo hulipwa kulingana na niyah” ni mizani ya kupima matendo kwa ndani. Kisha yanakataliwa kwa mwenye kuzusha, na kila anayezusha katika Dini asiyoidhinisha Mwenyezi Mungu na Mtume wake, uzushi si lolote katika dini [7]. Muislamu lazima azihukumu Hadith hizi mbili katika matendo yake yote; akiangalia mwonekano wake, je inakubaliana na Sharia? Na katika sehemu yake ya ndani kabisa: Je, alitaka radhi za Mwenyezi Mungu kwa hilo au la?
2- Katika Hadithi, ni dalili kwamba ibada yoyote lazima iwe chini ya masharti ya Sharia, na masharti ya Sharia ndio yanaiongoza iwe ni amri au katazo. Na masharti ya sharia yanaisimamia kwa amri yake na uharamu wake, basi mwenye kufanya ibada kwa kuichunga sharia na kuafikiana nao atakubaliwa, na aliye nje ya hayo anakataliwa [8]
3-Muislamu asiipime sheria kwa akili yake, na wala asiruhusu haramu wala asikataze halali kwa matakwa yake; Sheria ni kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu na Sunna ya Mtume, amani iwe juu yake.
4.Kuhuisha Sunnah ni utiifu mkubwa ambao Muislamu anastahiki kuongezewa katika wema wake ujira wa wale wote wanaomfuata katika utiifu, kama vile kuzua katika dini na kuwalingania watu katika uzushi ni mzigo mkubwa na ni mzigo maradufu. mwenye kuibeba mizigo yote ya wale wanaomfuata humo
Imepokewa kutoka kwa Abu huraira radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani amesema:
“Mwenye kulingania uwongofu Atapata ujira sawa na ujira wa wanao mfuata bila ya kuwapunguzia ujira wao hata kidogo. Na anayelingania upotevu atapata dhambi sawa na dhambi za wale wanaomfuata bila ya kuwazuilia dhambi zao hata kidogo.” [9].
5.Al-Fudayl-Mwenyezi Mungu amrehemu-
amesema:
Katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Ambaye ameumba mauti na uhai, ili akujaribuni ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri zaidi”
[Al-Mulk: 2]
na fanyeni vitendo vyema. Na akasema: Ikiwa kitendo hicho ni cha ikhlasi halafu kikawa hakiko katika mafundisho ya Mtume basi hakitakubaliwa, na ikiwa kiko katika mwongozo lakini hakina ikhlas nacho hakitakubaliwa mpaka kiwe safi na sahihi. Akasema: Na ikhlasi ikiwa ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na sawa ikiwa ni juu ya Sunnah [10].
6.Hakuna suala katika Dini lisilokuwa na msingi katika Kitabu na Sunnah ambalo linaweza kupimwa na hukumu yake ikatoka humo, kwa hivyo ni lazima kuwauliza wenye elimu bila ya kuzua uzushi katika Dini, Abdullah bin Masoud, Mungu amuwiye radhi, amesema: ““Fuateni wala msizue, kwani mmetoshelezwa, na kila jambo lililozushwa upya ni uzushi, na kila uzushi ni upotevu” [11]
7.Salaf walikuwa watu wenye shauku kubwa ya kufuata Sunnah za Mtume (Rehma na Amani zimshukie) na maswahaba zake. Ibraahiym Al-Nakha’i – Mwenyezi Mungu amrehemu – amesema: “Lau ningefahamishwa juu yao – yaani maswahaba – ya kwamba hawakupita kutawadha kwa ukucha nisingeli vuka walipo ishia, na inatosha kwa watu kupata dhambi kwa kupinga kwao matendo ya maswahaba wa Mtume wao Swalla Allaahu alayhi wa sallam)..” [12]
8.Omar bin Abdul-Aziz-Mwenyezi Mungu amrehemu- amesema: “Simama pale watu waliposimama, na useme kama walivyosema, na nyamaza waliponyamaza, kwani wamesimama na elimu, na kwa macho ya hatari wakaacha, na walikuwa na nguvu zaidi katika kuidhihirisha, na walistahili fadhila kama kungekuwa na fadhila ndanimwe [13].
9.Hakuna njia ya kujiepusha na fitna isipokuwa kwa kushikamana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah za Mtume wake, amani iwe juu yake. Kitabu cha Mwenyezi Mungu, mwenye kushikamana nacho, kinamtosheleza, kinamuongoa na kumlinda, na Sunna ya Mtume wake, rehema na amani ziwe juu yake, ni nuru ya njia siku ambayo giza la mitihani litakapo fika. Na katika riwaya iliyotoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu Amani iwe juu yake amesema:
“Mtaziona tofauti kali baada yangu, basi shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa Waongofu. Kwani kila uzushi ni upotofu” [14].
10.Amesema Mshairi:
Viumbe huishi, na majaribu huwavuta kwenye upotofu.
Watu wenye hila wanawafuata kwa hila zao = ili kuwaondoa katika njia sahihi
Hawachoki kufuata njia ya matamanio = haijalishi ni ugumu kiasi gani wanaokutana nao
Wamezielekeza nafsi zao kwenye majaribu na madhara = na wakajikita zaidi katika upotofu na ufisadi.
Marejeo
- Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/ 71, 72)
- Aliaetisam (1/75)
- Imepokewa na Muslim (867)
- Imepokewa na Abu Daawuud (4607), Al-Tirmidhiy (2676), na Ibn Majah (42)
- Imepokewa na Al-Bukhari (2010)
- Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/177)
- Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/177)
- Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/177)
- Imepokewa na Muslim (2674)
- “Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/ 71, 72)
- Tazama “Iielaamul muqiein A`n Rabi Alealamina" cha Ibn al-Qayyim (4/115)
- Tazama “Iielaamul muqiein A`n Rabi Alealamina" cha Ibn al-Qayyim (4/115)
- Tazama “Iielaamul muqiein A`n Rabi Alealamina" cha Ibn al-Qayyim (4/115)
- Imepokewa na Abu Daawuud (4607), al-Tirmidhiy (2676), na Ibn Majah (42)
1.Ametaja Mtume Rehema na Amani zimshukie kuwa Dini ya kweli ya Kiislamu ina sifa ya wepesi katika hukumu zake na urahisi wa gharama zake, kwa hiyo haimshindi mwanadamu, na wala haina gharama nzito ambazo zilikuwepo katika sheria zilizopita; Ilikua kwa Wana wa Israili mtu akifanya dhambi, toba yake kumuua. Na nguo haiwi safi ikipatwa na najisi ila kwa kukata sehemu ya najisi, na ndio maana Mwenyezi Mungu Mtukufu akasema katika kumuelezea Mtume Rehma na Amani zimshukie:
“Na Mtume Muhammad anawaondolea mizigo yao ya madhambi na minyororo iliyo kuwa juu yao.”.
[Al-A'raf: 157]
Na wepesi wa Dini ya Kiislamu ni kwamba imeweka masharti ya kuweza
Mtume amani iwe juu yake amesema:
“Niliyokukatazeni jiepusheni, na niliyokuamuruni, fanyeni kadiri muwezavyo” [1]
. si wajibu kwa masikini wenye mahitaji kutoa zaka, bali kwa tajiri ambaye ana miliki kiwango maalumu. Hijja si wajibu ila kwa sharti la kuweza katika fedha, afya na njia, pamoja na swala. Ambapo mtu asiyeweza kusimama anaswali kwa kukaa au kuegemea au apendavyo. Msafiri na mgonjwa hufungua saumu yake kwa ugonjwa unaotegemewa kupona na kisha kuzilipa siku ambazo hakuzifunga, na mgonjwa asiyeweza kufunga kwa vyovyote vile hufungua saumu yake na kumlisha masikini mmoja kwa kila siku, na ndivyo ilivyo katika masuala yote ya kisheria.
Uislamu ndio unaowarahisishia wenye udhuru, kama vile kuhalalisha swala ya khofu kwa wale walio katika vita, kufupisha Swalah na kuunganisha Sala mbili kwa msafiri, na kupangusa viatu kwa muda wa masaa ishirini na nne tu kwa mkazi na kwa msafiri siku tatu mchana na usiku, na mengineyo [2].
2.Hakuna atakayekuwa mkali katika hukumu za Dini na akaacha upole ndani yake na kuwa mkaidi na kujilazimisha asiyoyaweza; Isipokuwa hushindwa. Haijalishi atajidhibiti kiasi gani kwa kutumia nguvu zake na kuwa mvumilivu kwa kile alichojitolea, kuna muda atarudi nyuma na atachoka na kurudi kwenye urahisi. Mwongozo ulio bora kabisa ni uwongofu wa Mtume Rehma na Amani zimshukie na ndio maana aliposema Abdullah bin Amru bin Al-Aas: “Nitakesha usiku na kufunga mchana maadamu ni hai,” Mtume Rehma na Amani zimshukie alipewa habari hiyo, na akamkataza na akamuamrisha kufunga siku tatu za kila mwezi, na kuamka na kulala, lakini Abdullah alikataa kwa kujivunia nguvu na kwamba anaweza kustahimili zaidi, Akasema Mtume Rehma na amani ziwe juu yake: “Funga siku moja na ufungue siku mbili.” Akasema Abdullah bin Amru bin Al-Aas: “Mimi nina uwezo wa kufanya zaidi ya hayo.” Akasema Mtume Rehma na amani ziwe juu yake: “Funga siku moja na ufungue siku moja." Anasema Abdullah bin Amr, Mwenyezi Mungu awe radhi nao wote wawili, na baada ya kuwa mzee na kushindwa kushika saumu yake, alisema: “ningezikubali siku tatu alizosema Mtume wa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu amfikishie rehema na amani, ingependeza kwangu kuliko familia yangu na mali”. [3] ni kwa sababu hakupenda kubadilisha chochote kwa kutengana na Mtume, rehema na amani ziwe juu yake.
3.Ndio maana ni lazima kuwa kati na kati katika ibada, ambayo ni ukati kati ya kupita kiasi na kuzembea, na njia ya kufanya kazi, ambayo ni kwamba ikiwa hatuwezi kuchukua ukamilifu, basi tujitahidi kufanya ibada tuziwezazo kwa karibu zaidi” [4]
Hii ni amri kutoka kwa Mtume (Rehma na Amani zimshukie) ya kuwa na utaratibu mzuri katika kuabudu bila ya kutia kuzidisha wala kuzembea. Iwapo mtu hana uwezo wa kufanya ibada iliyo bora zaidi, basi afanye ibada yoyote iliyo karibu na yaliyo bora zaidi. Kwa sababu kile ambacho hakipatikani kikamilifu, basi hakiachwi kikamilifu. [5]wakashindwa kufanya ibada kwa njia iliyo bora, Mwenyezi Mungu Mtukufu amewaandalia malipo makubwa bila ya kuwapunguzia ujira wao
4.Kisha Mtume Rehema na Amani zimshukie akawabashiria Ummah wake; Hata wakipungukiwa na vitendo vyao.
5.Na Mtume Rehema na Amani zimshukie alipojua kwamba watu kamwe hawawezi kudumu katika ibada, akawausia kutumia muda wao wa kufanya ibada katika kuMuabudu Mwenyezi Mungu na kuchunga utiifu wake ambao ndio mwanzo. wa mchana na mwisho wake, na pia akawahimiza kuabudu katika nyakati zinazopendwa na bora zaidi, nayo ni ibada ya mwisho wa usiku [6] .
MAFUNDISHO:
1.Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, alitumia herufi “Innaa” ya kufuta, kuashiria uthibitisho na kusadikika kwa maneno yake. Hii ni mojawapo ya mbinu za wasemaji na walinganiaji ambazo walinganiaji wanapaswa kutumia.
2.Iwapo mtu atatafakari juu ya masuala ya kisheria na kuona urahisi na wepesi wake, na ruhusa zinazo patikana kwa wagonjwa na wasiojiweza; Hapo atajua kiwango cha rehema na fadhili za Mwenyezi Mungu kwa waja wake, kwa hiyo atazidisha upendo wake kwake na kumridhia kwa kumtii.
3.Hadithi imeeleza kuwa kutokutumia fursa katika kipindi cha dharura kunapelekea mtu kushindwa na kupata hasara, hivyo mja anapohitaji fursa ya ruhusa basi jambo bora na la Sunnah ni kuitumia fursa hiyo na si kujipa uzito, Kila inapokuwa vigumu kwa msafiri kufunga basi afungue saumu, na mgonjwa anapochoka kusimama kuswali basi na aketi, hivyo umasikini na njaa kali ikimpelekea mtu kufikia kula mzoga na vitu vingine ili kuiokoa nafsi yake basi afanye hivyo ili asije kufa [7].
4.Haifai kwa mtu kujitesa katika dini ya Mwenyezi Mungu na kujiwekea uzito kwa kufanya ambayo Mwenyezi Mungu hakumlazimisha, kwa hivyo kujiwekea uzito katika ibada ni kujichosha.
5.Maana ya Hadithi sio kwamba mwenye kujitahidi katika utiifu ni mbaya, lakini jambo baya ni mtu kujiwekea ibada nyingi asizoweza kustahimili.
6.Kushikamana na Sunnah za Mtume (Rehma na Amani zimshukie) ni bora kuliko kuzidisha, kwani kufunga, kula mchana, kusimama usiku kusali na kulala ni bora kuliko kufunga milele na kusimama, na ndio maana Mtume amani iwe juu yake, aliwaambia watu waliosema ibaada ya Mtume (Rehma na Amani zimshukie) na kutaka kuizidisha kwa kusema:
“Wallahi mimi ndio mchamungu wenu na ninaemuogopa Mwenyezi Mungu zaidi kuliko ninyi, lakini pamoja na hayo kuna muda ninafunga na ninakula mchana, na ninasimama usiku na ninalala, na ninaoa wanawake, basi mwenye kujiepusha na Sunnah yangu si katika mimi” [8].
7.Katika Hadithi kuna ushahidi kwamba kufuata sheria ni kuabudu katika mfumo mzuri wa kati na kati; Kwa sababu kujitia uzito na kujitia ngumu kunapelekea kuacha kila aina ya ibada, na dini ni nyepesi, na hakuna atakaye jitilia uzito katika dini isipokuwa itamshinda, na Sharia iliyotakasika imeegemezwa juu ya usahilishaji na kuto kujitenga [9].
8.Inafaa zaidi kwa mfanyakazi kutojituma kwa namna ambayo atashindwa kudumu katika ibada; Badala yake, anatakiwa kufanya ibada kwa upole ili ibada yake idumu na isikatishwe, na katika hadithi:
“Ibada ipendezayo kwa kwa Mwenyezi Mungu Aliye Juu Sana, ni ile inayodumu, hata kama ni ndogo” [10].
9.Kinachotakiwa kwa mja ni kufanya juhudi katika kumtii Mwenyezi Mungu na kutaka kuufikia ukamilifu kadiri awezavyo, anapaswa kujitahidi kuwa mnyenyekevu katika sala, na kuikamilisha ibada kikamilifu, na kuelewa masomo yake yote, na kukaa mbali na dhambi zote na kutekeleza amri zote. Ikiwa, baada ya kujitahidi dhidi ya nafsi yake, atayapata yote, basi ni mwenye kutukuzwa na kulipwa.
10.Sunnah ni msingi wa kati ya vitu viwili ninavyokinzana. Kupindukia na kupita kiasi. Mtu hatakiwi kuzidisha na kutilia ngumu katika ibada, wala asipuuze au kuzembea katika kuacha maamrisho na kufanya mambo ya haramu.
11.Ni katika Sunnah mlinganiaji na faqihi wampe mja mwema bishara ya neema ya Mwenyezi Mungu na malipo ya utiifu wake, na kwamba asikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu.
12. Ni lazima mtu achague nyakati nzuri katika kuMuabudu na kumtii Mwenyezi Mungu. Ikiwa anahisi uvivu au kutojali, anapaswa kulala na kupumzika, kisha aanze tena wakati anapokuwa na nguvu na kuimarika. Atafanya hivyo katika ibada, utiifu, kazi za kidunia, kutafuta elimu, na kadhalika.
13.Jambo zuri ni kuzipangilia ibada kwa mzunguko wa siku nzima ili mtu apate muda mzuri wa utiifu na ibada kuliko kukusanya ibada nyingi kwa saa moja inayochosha mwili.
14.Kutokana na rehema za Mwenyezi Mungu juu yetu, hakutulazimisha kusali swala za usiku, wala hakutuhimiza kuswali usiku mzima, bali Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, amesema katika Hadith: “Na kusinzia kidogo” ili kupunguza na kurahisisha ugumu wa ibada ya usiku, vinginevyo angesema: “Na usiku.”[11]
15.Kutoka kwa Aisha, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwamba Mtume, rehma na amani zimshukie, alikuwa akijiwekea mkeka nyakati za usiku, na anasali usiku. Kisha mkeka huo anaukunjua mchana na kukalia juu yake, hivyo wakawa watu wanashindana kwa wingi kuja kwa Mtume, rehma na amani zimshukie na kusali nyuma yake, Kisha Mtume akaja na kusema: “Enyi watu! fanyeni ibada mnazoziweza, kwani Mwenyezi Mungu hachoki mpaka mchoke, na matendo yanayopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu ni yenye kudumu hata yakiwa machache."[12]
16.Aliingia Mtume rehma na Amani zimshukie na akaona kamba iliyonyoshwa baina ya nguzo mbili,
akasema Mtume: “Ni kamba gani hii?” Wakasema Maswahaba: Hii ni kamba ya Zainab, na akilegea anaiegemea, basi Mtume rehma na Amani zimshukie akasema: “La, itoweni ili kila mtu afanye ibada kwa uchangamfu wake, na endapo atachoka, mwacheni aketi.” [13].
Marejeo
- Imepokewa na Muslim (1337)
- Manar Al-Qari Sharh Mukhtasar Sahih Al-Bukhari” cha Hamza Muhammad Qasim (1/121, 122).
- Imepokewa na Al-Bukhari (1131) na Muslim (1159)
- Fath al-Bari cha Ibn Hajar (1/95)
- Manar Al-Qari Sharh Mukhtasar Sahih Al-Bukhari" cha Hamza Muhammad Qasim (1/123)
- Fath al-Bari cha Ibn Hajar (1/95)
- Tazama: Fath al-Bari cha Ibn Hajar (1/ 94, 95)
- Imepokewa na Al-Bukhari (5063) na Muslim (1401), kwa kutoka kwa Anas
- Nailu al-Awtar" cha al-Shawkani (6/123)
- Imepokewa na Al-Bukhari (6464) na Muslim (783), kutoka kwa Mama wa Waumini, Aisha,Mwenyezi Mungu amuwiye radhi
- Al-Tafsir Lashrh Al-Jami’ Al-Sahihah” cha Ibn Al-Mulqin (3/87)
- (Imepokewa na Al-Bukhari (5861) na Muslim (782
- Imepokewa na Al-Bukhari (1150) na Muslim (784), kwa kutoka kwa Anas Mwenyezi Mungu amuwiye radhi.
1. Mmoja wa Mabedui aliingia akitokea eneo la Najd - Ni uwanda unaoenea kutoka Hijaz upande wa mashariki hadi Al Yamaamah upande wa magharibi, sasa inajumuisha Riyadh, Qassim na Aflaaj [1] – kwa Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), akiwa amekaa na maswahaba zake, na huyo bedui alikuwa na nywele zilizo chakaa, asiyejali muonekano wake, akiwa anaita kwa mbali na kusema kwa sauti kubwa, sauti yake inasikika, na anachosema hakieleweki, Alipokaribia mkusanyiko ule, walielewa maneno yake, kumbe alikuwa anauliza kuhusu sheria za Uislamu[2].
2. Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), akamuelezea faradhi ya swala, kwamba ni nguzo ya pili ya Uislamu baada ya shahidi mbili, na kuna Swalah tano juu yake mchana na usiku, nazo ni Fajr, Dhuhr, Asr, Maghrib na Isha. Bedui akamuuliza: Je, ni wajibu kwangu kufanya jambo jengine iwapo nitazitekeleza swalah hizi na kutekeleza nguzo, wajibaat na kwa kusali kama ipasavyo? Nabii akajibu (Rehema na amani ziwe juu yake), si wajibu kwake isipokuwa Swalah hizo, ila kwa kujitolea.
Kujitolea: Ni kwamba mja ajikurubishe kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa njia ya ibada ambayo si lazima kwake, kwa kutamani kupanda daraja Siku ya Kiyama, haya ni matendo yaliyohimizwa yafanywe, mwenye kuyafanya analipwa, na asiyeyafanya hataadhibiwa[3].
3.Kisha Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) akataja swaumu ambayo ni nguzo ya nne ya Uislamu, na maana yake ni; kujiepusha na vyakula, vinywaji, na mambo mengine yote yanayofungua saumu, kuanzia mapambazuko ya alfajiri ya kweli hadi kuzama kwa jua, kwa nia ya kutafuta malipo kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu[4]. Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), akamwambia kwamba ni lazima afunge mwezi wa Ramadhani, Bedui akamuuliza Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake): Je, inanilazimu kufunga tofauti na mwezi huu? Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) pia akamjibu kuwa si wajibu kufunga isipokuwa Ramadhani, ila kufunga kwa hiari katika siku zingine ambazo si lazima kufanga.
4.Kisha Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) akamueleza Zaka, ambayo ni nguzo ya tatu ya Uislamu baada ya shahada mbili na swala, akamwambia kuwa ni wajibu, na akambainishia hukumu zake.
Zaka: Ni kumuabudu Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutoa sehemu ambayo ni wajibu kisheria juu ya mali maalum kwa ajili ya watu au kazi maalumu[5]. Bali, iliitwa zakat kwa sababu inaitakasa nafsi na kuisafisha kutokana na dhambi.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:
“Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo”
[At-Tawbah: 103].
Basi yule mtu akamuuliza Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake): Je, ni lazima nitoe pesa zangu zaidi ya ile Zaka iliyofaradhishwa? Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake): akasema: Hapana, isipokuwa kujitolea na kutoa pesa zako kwa njia za kusaidia katika mambo ya kheri.
5.Kisha yule mtu akaondoka na kusema: “Naapa kwa Mwenyezi Mungu, siwezi kuongeza katika haya wala kupunguza.” yaani, atatekeleza vile inavyopaswa, bila kuongeza au kupunguza, Kama unavyomwambia aliyekupangia kazi: Sitaongeza wala sitapunguza.
makusudio ya mtu huyo si kwamba atakomea kwenye amri hizo na kuacha mengine yote ambayo Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) hakutaja, kama vile kuinamisha macho, kuzilinda tupu, kutekeleza amana, kusema kweli, na mengineyo; kwa sababu huo ni uovu haifai kwake kuusema, na Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) hawezi kumkubalia jambo kama hilo, bali alimuuliza Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) juu ya matendo na faradhi zitakazomfikisha Peponi, ndio maana hakumwambia juu ya kuepuka makatazo na mengineyo.
Kama ilivyo kwa mwenye kushikamana na aliyoamrishwa kwa kiwango hiki, inapomjia amri kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu au kwa Mtume wake, basi huikimbilia kuitekeleza, na wala haiachi, iwe ni faradhi au Sunnah[6].
6.Basi Mtume, (Rehema na amani ziwe juu yake) akasema kwamba, huyo mtu akitimiza hayo na akawa mkweli, basi amefaulu na ameshinda kwa kupata kila lililo la kheri.
Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) hakuzitaja shahada mbili; kwa sababu alijua kwamba anazijua, au kwa sababu alikuja kumuuliza kuhusu sheria za kivitendo za Uislamu, vile vile hakumbainishia Hija kwa sababu ilikuwa bado haijawajibishwa, au labda haikuwa wajibu kwake, au aliitaja na msimuliaji akaifupisha hadith[7].
MAFUNDISHO
1.Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), alivumilia ukali wa Bedui huyo na kumpandishia sauti, katika hili yapo mafunzo kwa mlinganiaji, mwalimu na mlezi kwamba inatakiwa awe na subira na kuvumilia taabu za Da’wa; Anaweza kukutana na makosa au maudhi; Ni lazima awe na uvumilivu, na kufuata mfano wa Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake).
2.Mlinganiaji, msimamizi, msomi na mlezi lazima wazingatie tofauti za kiakili baina ya watu, wasitumie njia moja kuishi na watu wote, Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), hakumkosoa bedui kwa kunyanyua sauti yake, wala kumlaumu kwa hilo.
3.Mtu huyo alikuwa amependa sana kumuuliza Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), juu ya yale ambayo yatamnufaisha bila ya kuwa na haya, Kila alipomuamuru kufanya jambo fulani, alisema: “Je, ni lazima nifanye jambo lingine?”. Mtu anapaswa kuwa na bidii ya kutafuta elimu, haya au kiburi haipaswi kumzuia kuuliza.
5.Swalah za Sunna ni nyingi, za muhimu na zenye daraja ya juu zaidi ni Sunna zilizosisitizwa, zinazokuwa baada ya Swalah za faradhi, nazo ni rakaa mbili kabla ya Alfajiri, nne kabla ya Adhuhuri, mbili baada yake, mbili baada ya Almagharib, na mbili baada ya Al ishaa;
Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) amesema:
“Mwenye kuswali rakaa kumi na mbili mchana na usiku, atajengewa nyumba Peponi.[8]”
Ikiwa ni pamoja na Swala ya Duha, qiyaam al-layl (Swalah za usiku), Swala ya Witr, na Swala zingine za Sunna ambazo Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema ndani ya Hadithi tukufu:
“Haachi Mja wangu kuendelea kujikurubisha kwangu kwa Sunna mpaka nampenda, basi nikimpenda, mimi ndiyo nakuwa sikio lake ambalo hutumia kusikia, na jicho lake ambalo hutumia kuona, na mkono wake ambao hutumia kushika, na mguu wake ambao hutumia kutembea, na akiniomba, nitampa, na akiniomba kinga, nitamkinga.[9]”
6.Kujitolea kufunga ni mojawapo ya Sunna bora, Mwenyezi Mungu Mtukufu amemuandalia mwenye kujitolea kufunga malipo makubwa; Kufunga siku ya Arafah kunafuta madhambi ya mwaka uliopita na mwaka ujao[10]. Funga ya A’shuraa inafuta madhambi ya mwaka uliopita[11]. Anayefunga siku sita za Shawwal, baada ya Ramadhani ni sawa na kufunga mwaka mzima[12].
7.Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) ameitaja Zaka kwa sababu ni dalili ya imani ya mtu. Ni Muumini pekee ndiye anayetoa Zaka kwa ridhaa yake; Sababu ni kwamba nafsi inapenda mali na inafanya ubakhili kuzitoa, ikiwa itaruhusu kutolewa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, hii inaonyesha ukweli wa imani yake kwa ahadi na maonyo ya Mwenyezi Mungu. Mja hana budi kupima imani yake kwa kutoa Zaka na sadaka na kujizoesha kufanya hivyo, kwasababu yaliyopo kwa Mwenyezi Mungu ni bora na yanadumu.
8.Akasema Bedui: “Wallahi mimi siongezi juu ya haya wala sipunguzi”. Hii ni alipojua kwamba kutekeleza faradhi inatosha kuingia Peponi. Ni lazima mtu awe thabiti na mwenye bidii katika kila jema analofanya na kutarajia malipo yake, asirudi nyuma wala kukata tamaa baada ya kuanza, iwe katika matendo ya Akhera au ya Dunia. Mwanafunzi hapaswi kuwa mvivu katika kusoma masomo yake, na askari asichoke kulinda mpaka wake, na mkono wa ufanisi usikose kwa mfanyakazi na mtengenezaji wa vifaa mabalimbali hadi amalize kazi yake.
9.kauli ya Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), baada ya maneno ya mtu huyo, ni ushahidi kwamba hii sio tu kwake, bali ni kwa kila Muislamu mwenye kutekeleza mambo ya faradhi ipasavyo, na kujiepusha na yaliyo haramishwa, hayo yanatosha kuwa sababu ya kusalimika na Moto wa Jahannam na kuingia Peponi. Ieleweke kwamba, Pepo ina daraja. Daraja la juu na bora zaidi, ni mja kuwa katika kundi la manabii, mitume, wakweli, mashahidi na watu wema. Hapana shaka kwamba daraja hii haipatikani kwa kutekeleza faradhi tu, kila mtu na ibada zake! Na kila mwanadamu na yale ambayo nafsi yake inayatamani huko akhera!
10.Katika Hadithi, Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), alizingatia hali ya anaye linganiwa na muulizaji; Ndiyo maana hakumbainishia zaidi faradhi na nguzo ambazo zikikosa Uislamu wa yeyote huwezi kuwa sahihi. Mlinganiaji, mwanachuoni, na msomi, lazima awe mwerevu, amjibu muulizaji vizuri, na alinganie kwa namna inayoendana na hali mtu.
11.Mshairi amesema:
Kuinua mwito wa Swala juu ya minara = katika alfajiri ya asubuhi na usiku utulivu
wito unaoleta uhai kwa ulimwenguni = na wakazi wake, vijiji na miji
Na mwito kutoka mbinguni kwenda Ardhini = juu na ndani yake
Na kukutana baina ya Malaika na = Imani na Waumini bila ya idhini
Na kuondoka kwenye kufaulu, kheri =, haki, uwongofu, na wema.
Mshairi mwingine amesema;
Ewe mtoa sadaka mali ya Mwenyezi Mungu = katika njia za kheri, mali haipungui.
Ni kiasi gani Mwenyezi Mungu amezidisha mali kwa mmiliki wake kuzitoa = Ukarimu ni kwa hukumu ya Mwenyezi Mungu ni kupata radhi zake.
Ubahili hupelekea ugonjwa ambao hauna tiba = Mali ya bahili kesho itakuwa urithi kwa wanaoteseka. Sadaka ni furaha kwa wale wasio na uwezo = Watu wa ukarimu ukiwahitaji wanajitokeza.
Marejeo
- Tazama: "'Atlas Alhadith Alnabawi" cha Shawqi Abu Khalil (uk. 365)
- Tazama: Fath al-Bari cha Ibn Hajar (1/106)
- .Tazama: “Mughni Al-Muhtaaj” cha Al-Khatib Al-Sherbini (2/182)
- .Tazama: "Al-Sharh al-Mumti' ya Zad al-Mustaqni'" cha Ibn Uthaymiyn (3/5)
- .“Al-Sharh al-Mumti’ kwenye Zad al-Mustaqni’” cha Ibn Uthaymiyn (6/13)
- .Sherh ya Sahih Al-Bukhari cha Ibn Battal (1/104-105)
- .Tazama: Fath al-Bari cha Ibn Hajar (1/ 107)
- .Imepokewa na Muslim (728)
- .Imepokewa na Al-Bukhari (6502)
- .Imepokewa na Muslim (1162)
- .Imepokewa na Muslim (1162).
- (Imepokewa na Muslim (1164
1. Uislamu unahusika na mambo yote ya nje na ndani ya mwanadamu, ndiyo maana umebainisha muonekana wa Muislamu. Katika Hadith hii, Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) anaeleza kuhusu baadhi ya mambo ya kimaumbile, ni mambo ya Sunnah ambayo Mwenyezi Mungu amewaumbia waja na kuyaweka kuwa ni sheria, mambo hayo yakitekelezwa, uzuri wa mwili na maumbile kamili ambayo mwanadamu ameumbiwa hupatikana, wenye akili timamu wanalishuhudia hilo. Ila kuna baadhi ya mambo ya kimaumbile yanaweza kupotoshwa na kutolewa katika asili yake,
kama alivyo sema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehema na amani ziwe juu yake):
“"Kila mtoto huzaliwa akiwa na asili ya maumbile (yaani mwislaam), wazazi wake wanamfanya kuwa Myahudi, au Mkristo, au majusi. ” [1]
Si kwamba, mambo ya kimaumbile ni haya kumi tu, ambayo amebainisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehema na amani ziwe juu yake) katika Hadithi hii, bali, yametajwa katika Hadith nyingine, na wala hatukukusudia kuyataja yote hapa.
2. La kwanza katika mambo hayo ni: kukata masharubu; ni nywele zinazokua juu ya mdomo wa juu. Imeamrishwa zikatwe kwa sababu zikibaki, zinasababisha kero kwa kile kinacho toka puani, na kuingia kwenye maji wakati wa kunywa, na zinaweza kuwa na vijidudu hatari . [2]
Kukata masharubu ni Sunnah, na inatakiwa katika kuyakata, kujitahidi mpaka mdomo uonekane, na wala sio kuyanyoa.
3. Ya pili: kuacha ndevu zikue; Nazo ni nywele zinazoota kwenye kidevu na mashavu ya mwanaume. Kinacho kusudiwa katika kuacha ndevu ni kuziacha ziwe nyingi zisiguswe kwa kunyolewa au kupunguzwa.
Kuziacha ndevu zikue, ni wajibu kwa kila Muislamu, imethibiti katika Hadithi kadhaa zikibainisha hilo: "ziacheni, timizeni kwa kuziacha, ziachieni, ziacheni, ziacheni ziwe nyingi." Kwa hizi Hadithi zote, inaashiria kwambani amri ya kuacha ndevu zikuwe, na wala zsiguswe kwa kukata, kunyoa au kung'oa.
4. Ya tatu: Kutumia mswaki; Ni kijiti kinachotengenezwa kwa mti wa Arak hutumika kusafisha na kutakasa meno na kinywa, na kuondoa harufu mbaya.
Kutumia mswaki ni sheria na inapendeza kila wakati, inasisitizwa zaidi wakati wa Swala, na unapo amka kutoka usingizini, harufu ya kinywa inapobadilika na meno yanapoonekana kuwa ya njano;
Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehema na amani ziwe juu yake):
“mswaki ni kitakasa kinywa, unaridhiwa na Mola mlezi. ” [3]
5. Nne: Kupandisha maji puani; ni mtu kutia maji puani kisha ayatoe; ili kuondoa maudhi na uchafu uliomo ndani yake.
6. La tano kati ya mambo hayo: ni kukata kucha, inatakiwa mtu akate kucha ndefu; ili kuzuia uchafu na vijidudu hatari kukusanyika ndani yake.
7. Ya sita: kuosha fundo za vidole na nafasi zake zote, kwa sababu ni sehemu ambayo mara nyingi huwa zinaficha matope, najisi na vijidudu. Inaingia katika hukumu hii, sehemu zenye mikunjo katika mwili, inatakiwa pasafishwe na kuondoa uchafu uliopo.
8. Ya saba: kuondoa nywele zinazoota chini ya kwapa; kwa sababu zipo mahali ambapo jasho na uchafu hukusanyika, na kusababisha harufu mbaya.
Sunnah ni kuondoa nywele hizo kwa njia yoyote ile, iwe kwa kunyoa au kung’oa, kwa sababu lengo ni kuziondoa, na tayari litakuwa limetimia, japo kuwa kung’oa ni bora na vizuri sana kwa mwenye kuweza . [4]
9. Jambo la nane katika mambo ya kimaumbile: ni kunyoa nywele ambazo zinazokuwa sehemu za siri za mwanaume na mwanamke, kuota kwa nywele hizo ni ishara ya balehe. Uondoaji huu unaitwa isithdaad; kwa sababu hutumika chuma - ambacho ni wembe - kuzinyoa.
10. Jambo la tisa katika mambo ya kimaumbile: ni kutumia maji kwa ajili ya kujisafisha baada ya kujisaidia.
Wanazuoni wengine wakasema mtu anyunyizie maji kwenye sehemu zake za siri au nguo baada ya kutawadha; ili kuondoa wasiwasi kwamba huenda kuna matone ya mkojo yaliangukia nguo zake . [5]
11. Mmoja wa wapokezi wa Hadithi alisahau sifa ya kumi, akasema, kwa asilimia nyingi itakuwa ni kusukutua; yaani, ni mtu kuzungusha maji kinywani mwake kisha ayateme.
12. Wanazuoni wengine wakasema, bali sifa ya kumi ni tohara, ushahidi ni kwamba imetajwa katika Hadith iliyopokelewa kutoka na Abu Hurairah
Kutoka kwa Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake): amesema:
“Mambo ya kimaumbile ni matano au matano ni katika mambo ya kimaumile: tohara, kunyoa sehemu za siri, kung'oa nywele za kwapa, kukata kucha, kukata masharubu” . [6]
13. Tohara kwa wanaume ni lazima; nako ni kukata ngozi inayofunika kichwa cha sehemu za siri za mwanaume mpaka chote kiwe wazi; kwa sababu gozi hiyo humeza mkojo na kusababisha uchafu.
14. Ama kwa wanawake, tohara ni heshima na ni Sunnah. Inafanywa kwa kukata sehemu ndogo kabisa ya ngozi kwenye sehemu ya juu ya uke . [7]
15. Kimsingi, kukata masharubu, kukata kucha, kung'oa nywele za kwapa na kunyoa sehemu za siri, inapaswa viondoshwe haraka mara tu vinapo refuka, ikiwa ni ngumu basi, haipendezi kuviacha hadi siku arobaini zipite. Anas bin Malik (Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: “tuliwekewa muda wa kukata masharubu, kukata kucha, kung'oa nywele za kwapa na kunyoa sehemu za siri, visiachwe zaidi ya usiku arobaini” . [8]
MAFUNDISHO
1- Uislamu umezingatia usafi wa mwanadamu, kwa nje na ndani, na umehakikisha kuwa mtu awe katika hali nzuri
amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
“Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanao tubu na huwapenda wanao jisafisha”
[Al-Baqarah: 222]
eidha Uislam umefanya “kujitoharisha kuwa sehemu ya imani ”[9], hivyo basi Muislamu hana budi kuuweka mwili na muonekane wake safi, kama anvyo jitahidi kuzingatia usafi wa imani yake na moyo wake.
1- Mwenyezi Mungu Mtukufu ameweka sharti kwamba mja wake akitaka kusali, awe katika tohara kamili, mwenye nguo na mwili safi, tayari kwa kusimama mbele zake akiwa safi ndani ya kiwiliwili chake kwa toba, na nje kwa usafi na kujipamba, ndo maana mwenye kutawadha husema: “Ewe Mola nijaalie niwe miongoni mwa wanaotubia, na nijaalie niwe miongoni mwa wanaojitakasa.”
1- Inapendeza kwa mtu kufuata mafundisho ya Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), kwa kukata sharubu zake, na inapendeza kuanza na upande wa kulia.
1- Hairuhusiwi mtu kukata au kunyoa ndevu zake, bali kinacho ruhusiwa ni kurekebisha ambazo zimevurugika, ili ziwe na muonekano mzuri.
1. Haipendezi kwa mtu kuwa na baadhi ya sifa zilizotajwa na wanavyuoni kuhusiana na ndevu; kama vile kuzipaka rangi nyeusi kwa wasio kuwa katika jihadi (vitani), kuzipaka rangi ya manjano ili ionekane kuwa una Zuhdi (umeiacha Dunia na kuifuata Akhera), kuzitia weupe ili kuhadaa uonekane kuwa ni mzee mwenye hekima na maarifa, kunyoa, kung'oa mvi, kuweka mtindo kwa ajili ya kuwavutia wanawake na kuziacha zimevurugika ili kuonyesha kuwa una Zuhdi na kutojijali . [10]
2. Inapendeza mtu kutumia mswaki kusafisha kinywa chake na kukitia manukato ili kuondoa harufu mbaya. Ili kutimiza hilo, inaruhusiwa kutumia mswaki wa brashi, dawa ya meno, na vinginevyo ambayo vitatimiza lengo.
3. Ni Sunna kutumia mswaki kabla ya kila swala kwa kufuata yale aliyosema Mtume, (Rehema na amani ziwe juu yake):
“Lau nisingeliona kuwa ni uzito kwa Ummah wangu -au kwa watu-, ningeliwaamrisha kutumia mswaki kabla ya kila Swala. ” [11]
1- Si vibaya kutumia mswaki wakati wowote, bali kwa aliyefunga inapendeza kuutumia, kutoka kwa Amer bin Rabi’ah, (Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: “Nimemuona Mtume, (Rehema na amani ziwe juu yake) kwa idadi zisizo hesabika, akipiga mswaki hali ya kuwa amefunga ” [12]
1- Kupandisha maji puani ni miongoni mwa vitendo vinavyosafisha pua, na ndio maana Mtume (Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amemuamrisha mwenye kutawadha, akasema: "pandisha maji puani kwenda juu, isipokuwa kama umefunga. " [13]
1- Muislamu awe na pupa ya kupunguza na kukata kucha, kama inavyopaswa pia kujikagua uchafu unaoingia ndani yake kuzisafisha.
1- Inaingia katika hukumu ya kuosha vifundo na nafasi za vidole, kila sehemu inayoweza kukusanya uchafu; kama masikio, mikunjamano ya mwili na kila sehemu ambayo jasho au udongo au chochote mfano wake vinaweza jikusanya . [14]
1- Inapendeza kwa mtu kunyoa nywele zake za sehemu ya siri mara kwa mara, kusafisha maeneo yote ambayo yanaota nywele na kusafisha maeneo ya mapaja yake, na kuhakikisha kwamba maji yameingia kwenye ngozi vyema, kwa sababu maeneo hayo nivyepesi kupata magonjwa na maambukizi.
1. Bila shaka kutumia maji kusafisha mahali baada ya kujisaidia ni bora kuliko kutumia vitu tofauti na maji wakati kuna maji. Kwani kutumia maji uchafu uondolewa kabisa, na athari zake hutakaswa, na harufu yake mbaya hutolewa kutoka mahali pa najisi.
2. (11) udanganyifu na kujiona visimzuie Muislamu kutokubali haki au kusema ukweli; kwani Msimulizi wa Hadith hii alipotia shaka kuwa amesahau sifa yoyote kati ya hizo, alisema wazi; hivyo Basi kuweka wazi kosa, au kusahau na kutojua ni bora kuliko kumzulia uongo Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mtume wake, amani iwe juu yake.
3. (11) kusukutua kinywa ni miongoni mwa Sunnah za maumbile ambazo Muislamu anatakiwa kuzipupia na kudumu nazo. Ili apate radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu na malipo ya kumfuata Mtume Wake, na ili akamilishe twahara kamili.
5. Mshairi alisema:
Ulizaliwa na asili yako ambayo = ni imani na kusadikisha uwepo wa Muumba
Na umetahiniwa kwa kupewa mamlaka ya kuchagua= na mbele yako kuna njia mbili ziko wazi.
Basi ukifanya kila ulitakalo, tambua kuwa uko chini ya uangalizi = kwani wewe huwezi kufichikana mbele ya Mwenyezi Mungu Hakimu.
Marejeo
- Imesimuliwa na Al-Bukhari (1385) na Muslim (2658), kwa kutoka kwa Abu Hurayrah (ra)
- “Sharh Riyadh as-Salihin” cha Ibn Uthaymiyn (5/230).
- Imesimuliwa na Al-Nasa’i (5), na Al-Bukhari alitoa maoni ya msistizo kabla ya hadith (1934).
- Sherh Al-Nawawi alaa Muslim” (3/149).
- Sherh Al-Nawawi alaa Muslim” (3/150)
- Imepokewa na Al-Bukhari (5889) na Muslim (257).
- “Sharh Riyadh as-Salihin” cha Ibn Uthaymiyn (5/229).
- Imepokewa na Muslim (258).
- Imepokewa na Muslim (223).
- Sherh Al-Nawawi alaa Muslim (3/149, 150).
- Imepokewa na Al-Bukhari (887) na Muslim (252).
- Imepokewa na Al-Tirmidhiy (725), na amesema Hadithi nzuri, na Al-Bukhari akatoa maoni kwa kusisitiza Hadithi (1934).
- Imepokewa na Abu Daawuud (142), Al-Tirmidhiy (788), Al-Nasa’i (114), na Ibn Majah (448).
- Tazama: “sherh Al-Nawawi alaa Muslim” (3/150).
1. Mtu mmoja miongoni mwa Maswahaba, Mwenyezi Mungu awawie radhi, alimuuliza Mtume Rehema na Amani zimshukie kuhusu kutawadha kwa maji ya bahari; kwani wengi wao walikuwa wakisafiri baharini na kubeba maji kidogo, ikiwa watayatumia kutawadha basi watapatwa na kiu kwa kukosa maji safi ya kunywa, wakauliza je, inajuzu kwao - katika hali hii - kutawadha kutokana na maji ya bahari?
2. Mtume (rehema na amani ziwe juu yake) akajibu kuwa maji ya bahari asli yake ni safi na yanaweza kusafisha kitu kingine, hata ikiwa rangi na ladha yake ni tofauti na maji mengine matamu.
3. Mtume akumuongezea faida kwa kumbainishia kwamba mnyama yeyote katika wanyama wanaoishi baharini, basi inafaa kumla, ispokuwa wale waliotolewa katika hukumu hiyo, kama Mwenyezi Mungu alivosema:
" Mmeharamishiwa nyamafu,"
[Al-Ma’idah: 03].
Na mtume amesema:
" Mmehalalishiwa -kula aina mbili za visivyochinjwa- na damu mbili, ama aina mbili za visivyochinjwa ni nyangumi na nzige, na damu mbili ni ini na bandama.[1]"
MAFUNDISHO:
1.Swali la swahaba lilikuwa wazi, kwani alielezea msimamo wake kikamilifu; Kwa sababu fat-wa inaweza kutofautiana kulingana na hali na eneo, hivyo basi muulizaji ni lazima amuelezee kwa uwazi kabisa suala lake mbele ya mufti, na mufti asijibu mpaka aelewe suala hilo kikamilifu kwa vipengele vyake.
2.Swahaba huyu alikuwa anapenda sana mambo ya Dini yake, ingawa alikuwa msafiri anayeweza kuunganisha Swala au kuchelewesha Swalah mpaka mwisho wa wakati wake hadi awasili eneo anakoenda ikiwa safari yake ni fupi, lakini yeye alipenda kuuliza masuala haya, kwa kutilia maanani utendaji wa kuswali swala kwa wakati. Hivyo basi Hatupaswi kujishughulisha na mambo ya kidunia badala ya kuMuabudu Mungu Mwenyezi.
3. Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, akajibu kwa kusema: “Ni maji safi,” na hakujibu “ndiyo,”; ili isije ikafahamika kwamba inajuzu kwa mtu kutawadha maji ya bahari pale tu anaposafiri baharini na maji kidogo, na haijuzu kuosha uchafu na maji hayo. Bali alisema: “Ni maji safi” ili kuonyesha hukumu ya jumla kwamba maji ya bahari ni safi na yanatwaharisha, sawa iwe kuna maji mengine safi au la, na sawa ikiwa mtu yuko safarini au mkaazi[2] na hii inaonesha upeo katika hekima ya mwanasheria; kwani Jibu lake linapaswa kuwa wazi na lisiwe na dhana.
4.Kauli ya Mtume (rehema na amani ziwe juu yake): “Ni maji safi,” kwa kubainisha maneno hayo mawili ni uthibitisho wa hukumu; Angeweza kusema: maji ya bahari ni safi, lakini alithibitisha hilo kwa kufafanua maneno yote mawili. Hivyo basi ni lazima kwa mwanachuoni na msomi wa sheria majibu yake yawe yana uhakika na hakuna nafasi ya shaka ndani yake, vinginevyo muulizaji atabaki na sintofahamu katika kufanya kazi na fat-wa.
5. Katika hii Hadith, inajuzu kuongeza katika jibu la muulizaji kwa jambo ambalo hakuuliza, ikiwa muulizwaji ataona haja ya muulizaji kwa kile ambacho hakikuwa katika swali; Kwani muulizaji katika hadithi hii alikuwa akisafiri baharini mara kwa mara, na hili lilimlazimu kukutana na samaki waliokufa wakielea juu ya maji, basi Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) akamjulisha kuwa ni halali na inajuzu kwake kula. Hvyo basi Ni bora kwa mlinganiaji,na mwalimu na msomi wa sheria asitosheke kujibu swali la muulizaji kwa yale yaliyojumuishwa katika swali lake, ikiwa anaona kitu kingine kinachohusiana nayo ambacho muulizaji amesahau kuuliza juu yake basi yeye aongezee ili kutoa faida zaidi.[3]
Marejeo
- Imepokewa na Ibn Majah (3314).
- "Nail al-Awtar" cha al-Shawkani (1/29, 30).
- "Nail al-Awtar" cha al-Shawkani (1/30, 31).
Akasimama Othman bin Affan Allah awe radhi naye mbele ya watu akawafundisha namna ya kutawadha, akaitisha maji ya kutawadha, akaanza kwa viganja vyake na akaviosha mara tatu. kisha akachukua maji kwenye kiganja chake, akasuuza mdomo wake, na akaingiza maji puani mwake, kisha akayatoa ili kusafisha kilichomo ndani yake, akafanya hivyo mara tatu, kisha akaosha uso wake mara tatu, nao Uso ni kutoka kwenye maoteo ya nywele hadi chini ya kidevu kwa urefu, na kati ya masikio kwa upana, kisha akanawa mikono yake hadi kwenye viwiko , kuanzia na mkono wake wa kulia na kuosha mara tatu, kisha akaosha kushoto mara tatu pia, kisha akapangusa kichwa chake kwa mkono wake uliolowa mara moja, na wajibu juu ya kichwa ni kupangusa na sio kuosha. Kwa wepesi na utaratibu, kisha akaosha miguu yake na vifundoni - na kisigino mara tatu, kuanzia kulia na kisha kushoto.Msimulizi hakutaja kwamba aliosha masikio yake kwa sababu yanaoshwa - kwa nje na kwa ndani - kwa kupangusa kichwa, kama ilivyothibitishwa kutoka kwa Mtume, amani iwe juu yake .[1]
Uthman Mwenyezi Mungu awe radhi naye, amepokea katika Hadithi hii kwamba, wudhuu wa Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam ulikuwa mara tatu, na ikatajwa katika hadithi nyingine kwamba alitawadha mara moja, na mara mbili, kwa hivyo jumla ya yote yanayoashiria kuwa faradhi hukamilika kwa kuosha mara moja yenye kutwaharisha, na kwamba kinachozidi ni Sunna, isipokuwa Mtume-Swalah na salamu za Allah ziwe juu yake- hakuongeza Zaidi ya Kuoshwa mara tatu kwa kila kiungo, na akasema: “Mwenye kupita Zaidi ya idadi hii amedhulumu, amevuka mipaka na amedhulumu”[2] . Mara moja inatosha, ya pili ni Sunnah, na ya tatu ni ya juu kabisa ya ukamilifu, na hakuna zaidi ya hiyo ni dhulma.
2. Kisha Othman, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, akasema kwamba alimuona Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam anatawadha namna hii, na kwamba anataka kuwafundisha watu namna ya kutawadha alivyotawadha Mtume, rehma na Amani zimshukie, kama alivyoona.
3. Kisha Othman, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, akataja kuwa Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, alisema kuwa mwenye kutawadha mfano wa wudhuu huu kisha akaswali rakaa mbili kwa unyenyekevu na ikhlasi haongeleshi nafsi yake mambo ya kidunia. Bali ikiwa kuna jambo litamshughulisha katika yale yaliyomtokea Muislamu wakati wa swala yake, ayaondoshe na asiende mbali katika hilo, basi malipo yake ni kwamba atasamehewa madhambi yake yote yaliyopita.
Na Hadithi ilivyo dhaahiri inaashiria kuwa msamaha huu unajumuisha madhambi yote: madhambi madogo na makubwa, isipokuwa mfano wake miongoni mwa hadithi imehusisha tu madhambi madogo, sio madhambi makubwa,
kama alivyosema Mtume:
“Swala tano, na ijumaa mpaka ijumaa, na Ramadhani hadi ramadhani, hufuta madhambi yote pale atakapojiepusha na madhambi makubwa”[3]
Kwa hivyo wakafanya umaalumu huu katika madhambi haya madogo tu unazuwia kuingia madhambi makubwa hata katika hadithi zingine"[4]
4. Kwa kuwa msamaha wa madhambi unapatikana kwa kutawadha, basi kusali na kutembea kwenda msikitini kuna thawabu zaidi katika kufuta madhambi. Hivyo, kwa kutawadha na kuswali, anapata kafara ya madhambi, na pia ana thawabu ya kuswali na kwenda msikitini, bila ya kukatwa katika malipo yao. Na Mola Mlezi, Utukufu ni Wake, haridhiki na kumsamehe dhambi zake tu, bali pia humlipa kwa kusali na kutembea.
MAFUNDISHO:
Ustaarabu na kuona haya hakukumzuia Uthman, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, pamoja na hali yake inayo julikana ya kuwa na haya iliyopitiliza, kutawadha mbele ya watu ili kuwafundisha namna ya wudhuu. Aibu haikuzuii kutafuta elimu, kuieneza, kurekebisha makosa, kuamrisha mema, au kukataza maovu.
Jifunze kutokana na Hadithi hii namna ya wudhuu wa Sunnah, na uwe makini kuufuata.
Udhu bora zaidi ni kuosha mara tatutatu, basi ifuateni wala msizidishe.
Kuosha mikono ni miongoni mwa Sunnah za wudhuu ambazo Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam alikuwa akipenda sana hata kama haikutajwa ndani ya Qur’an. Basi hakikisha unakusanya Sunnah za wudhuu na mustahabu zake na uzifuate.
Kuweka maji mdomoni, na kupandisha puani, na kupangusa masikio ni wajibu katika kuoga na kutawadha, kwa sababu pua na mdomo ni sehemu ya uso, na kuosha uso ni wajibu, na masikio ni sehemu ya kichwa, hivyo lazima kuwa makini.
Mpangilio baina ya faradhi na Sunnah ni faradhi ambayo lazima izingatiwe.
Hakikisha unatawadha kwa mfululizo, basi usikatishe wudhuu wako kwa lolote kisha uendelee.
Viwiko na visigino vimejumuishwa katika wudhuu, basi hakikisha vimeenezwa kwa kuosha.
Kisigino ni mifupa miwili inayotokeza chini ya mguu, na baadhi ya watu hawaiti mwisho wa nyayo kuwa ni kisigino, kwani hiyo wanaita kisigino, sio fundo mbili.
Uthman, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, hakutamka nia kwa sababu mahala pake ni moyoni, na kuitamka ni uzushi.
kunapatikana funzo kutokana na kitendo cha Uthman, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, kwamba Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam hakusema chochote kuhusu wudhuu wake kutokana na maneno ambayo watu wanasema: na haikuhifadhiwa kutoka kwake kwamba alikuwa akisema juu ya wudhuu wake zaidi ya kutaja jina la Allah , na kila hadithi ina yotaja nyiradi za udhu ambazo husemwa katika kutawadha, basi huo ni uongo kazuliwashiwa Mtume – rehma na amani ziwe juu yake- hakuyasema, na hakuufundisha umma wake, na haikuthibiti kutoka kwake, isipokuwa kusema Bismillah tu mwanzo wa kushika udhu. na kusema kwake: "Nashuhudia ya kwamba hakuna Mola wa haki ila Allah, peke yake asiye na mshirika, na nashuhudia ya kwamba Muhammad ni mja wake na Mtume wake, Ewe Mola, nijaalie niwe miongoni mwa wanaotubia, na nijaalie niwe miongoni mwa wanaotakasika.” Haya akiyasema mwisho wa udhu wake.[5]
Mwalimu, mwenye elimu na mlinganiaji anatakiwa kukimbilia elimu ya vitendo ambayo imekita mizizi katika akili na kufikiwa na ufahamu, kama alivyofanya Othman Mwenyezi Mungu amuwiye radhi.
Mwenye kuingia katika ibada ajiepushe na mawazo yanayohusiana na mambo ya kidunia, na ajitaabishe katika hilo, kwani mtu humshughulisha katika hali ya Swala yake anayoipenda.
Maana ya mazungumzo ya nafsi ni yale yaliyokuwa yanahusiana na mambo ya dunia, lakini kufikiri juu ya Akhera na adhabu yake na neema yake, hisabu, njia na mengineyo, si katika mambo yaliyokatazwa.[6]
Iwapo akili yako imeshikamana na mambo ya kidunia wakati unaswali, yatupilie mbali, na uzingatie katika Swala yako na utafakari maana ya Aya unazosoma au kuzisikia kutoka kwa imamu. fanya hivyo, haitakudhuru na haitaathiri sala yako.
Fursa kubwa ya kusamehewa madhambi, kwa wudhuu na kusali rakaa mbili nyepesi! Je, kuna mtu anatafuta kheri hiyo?
harakisha kutawadha;
Amesema, Mtume -rehma na amani ziwe juu yake:
“Je, nisikuongozeni kwenye yale ambayo kwayo Mwenyezi Mungu hufuta madhambi na huwapandisha watu daraja? Wakasema: “Ndio, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu.” Akasema: “ Ni kutawadha vizuri wakati wa dhiki (kama kipindi cha baridi kali), na kuchukua hatua nyingi kwenda Misikitini, na kusubiri Swalah baada ya Swalah.” Basi hiyo ndiyo sababu.[7]
Uislamu ni dini ya usafi, na uzuri, kiasi kwamba usafi ni aina ya ibada, na kitendo kikubwa kabisa cha ukaribu ambacho mja anajikurubisha nacho kwa Muumba wake, Utukufu ni Wake. na juu yake inategemewa kuhalalikiwa matendo mengi ya ibada.
Hakuna muovu atakayeingia Peponi, wala hataingia peponi mwenye uchafu. Mwenye kujitakasa katika dunia hii na kukutana na Mwenyezi Mungu aliyetakasika kutokana na uchafu wake, ataingia humo bila kizuizi, na asiyejitakasa katika dunia hii, ikiwa uchafu wake ni makhsusi, kama ukafiri, hataingia humo kwa hali yoyote. na ikiwa uchafu wake ni mapato ya bahati mbaya ataingia humo baada ya kujitakasa motoni kutokana na uchafu huo, kisha atatoka humo. Hata watu wa imani wakipita watakapo ivuka (swiraatwa)njia, wanafungwa kwenye daraja kati ya Pepo na moto wa Jahannamu, kwa hiyo wanasafishwa na kutakaswa kutokana na mabaki yaliyobakia juu yao, yaliyo wazuilia kuingia peponi, na hayakuwawajibishia kuingia Motoni, mpaka watakapo safishwa na kutakaswa ndipo wataruhusiwa kuingia Peponi.[8]
Mwenyezi Mungu Mtukufu anawafadhilisha waja wake kwa kuwaghufiria madhambi yao na kuwalipa kwa ajili ya sala zao na kuiendea kwao, basi vipi mtu mwenye akili timamu apuzie neema hiyo?!
Marejeo
- “Zad Al-Ma’ad” cha Ibn Al-Qayyim (1/ 187, 188).
- Imepokewa na Abu Daawuud (135), Al-Nasa’i (140), na Ibn Majah (422).
- Imepokewa na Muslim (233).
- Ahkam al-Ahkam Sharh Umdat al-Ahkam cha Ibn Daqeeq al-Eid (1/87).
- “Zad Al-Ma’ad” cha Ibn Al-Qayyim (1/ 187, 188).
- “Umdat Al-Qari Sharh Sahih Al-Bukhari” cha Badr Al-Din Al-Ayni (3/7).
- Imepokewa na Muslim (251).
- “"'iighathat allahfan min masayid alshaytan" cha Ibn al-Qayyim (1/56).
Tayammum ni ruhusa iliyowekwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa waja wake pale wanapokosa maji au kushindwa kuyatumia ili kuwarahisishia, na Mtume, rehma na amani ziwe juu yake
alisema:
“Mwenyezi Mungu anapenda kutumiwa ruhsa zake kama anavyochukia kuasiwa."[1]
na Wanachuoni wameifafanua kuwa tayammam ni : kukusudia mchanga - vumbi – ili kupangusa uso na mikono kwa nia ya kuhalalikiwa kuswali na mfano wa hayo.[2] Ni sheria iliyothibiti katika Qur’an, na Sunnah na makubaliano ya wanazuoni, na ni ruhusa maalumu ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu ameiweka katika umma huu”[3]
1. Ammar (ra) , anasimulia kuwa Mtume, (Rehma na amani ziwe juu yake) , alimtuma katika baadhi ya majukumu yake, kisha akajiotea na akapatwa na janaba, akazungusha mwili wake mzima katika mchanga safi ambao una vumbi mpaka mchanga ukaenea mwili mzima; Ili aweze kuhalalikiwa swala na kusoma Qur’an na mengine yanayofanana na hayo, kisha aliporejea kwa Mtume, rehma na amani ziwe juu yake, akamsimulia tukio zima Ili aweze kufahamu kama alifanya sawa au alikosea.
Ammar alifanya hivyo kwa sababu aliona kwamba mchanga/udongo hutumika badala ya maji, Hivyo basi Kama maji yanavyopaswa kuenea mwili mzima katika kuosha na kujitwaharisha, hivyo hivyo ndivyo inakuwa katika tayammam kwa mtazamo wake na jitihada zake.
2.Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alimwambia kwamba ilikuwa inatosha kupiga ardhi kwa mikono yake mara moja, kisha kupangusa mikono na uso wake, kwa kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu aliposema: " Na mkiwa wagonjwa au mmo safarini, au mmoja wenu ametoka chooni au mmewagusa wanawake, na hamkupata maji, basi tayamamuni vumbi lilio safi, na mpake nyuso zenu na mikono yenu" .
MAFUNDISHO :
Kitendo cha Ammar Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kinaashiria kwamba ni wajibu kwa Muislamu asipofahamu hukumu mojawapo ya masuala fulani, ambayo hajui hukumu yake wala kauli ya wanazuoni katika hilo, na muda wa kumuuliza mtu mwingine ukawa hautoshi au yuko safarini na asiweze kupata fat-wa; basi wakati huo inabidi kujitahidi kadiri awezavyo, kisha ikiwa atampata wa kumuuliza, ili kujua hukumu sahihi ya kisheria juu ya suala hilo basi afanye hivyo.
Katika hadithi hii inaashiria kuwa mwenye kujitahidi na kufasiri maana, ikiwa atakuwa miongoni mwa watu waliokidhi vigezo vya ijtihadi na akafasiri maana ya masuala Fulani, akawa amepatia sehemu na kukosea sehemu nyingine, basi si lazima kurudia kitendo hicho, kwani Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) hakumuamuru Ammar arudie; Kwa sababu alikosea katika sheria lakini alijitahidi, lakini alifanya twahara kwa namna isiyozingatiwa.[4]
Hadithi hii inaashiria kuwa sheria ya Uislamu ina kheri nyingi na wepesi, kwani haimtwiki mtu asiyoweza kufanya, ndio maana ikaruhusu tayammam, na kuridhika na kupangusa mikono na uso.
references
- Imepokewa na Ahmad (5866).
- "Nail al-Awtar" cha al-Shawkani (1/319).
- "Nail al-Awtar" cha al-Shawkani (1/319).
- "'Iikmal Almuealim Bifawayid Muslimin"cha Qadi Iyadh (2/223).
Swala ni nguzo ya pili katika nguzo za Uislamu baada ya shahada mbili, nayo ni nguzo ya Uislamu ambayo juu yake uislamu umejengwa.
Amesema Mtume (saw) :
“Kichwa cha mambo –yote- ni Uislamu, na nguzo yake ni Swala, na kilele chake ni jihadi” [1]
na swala ni kitendo kinachopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu
imesimuliwa Kutoka kwa Abdullah bin Masoud, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, amesema:
Nilimuuliza Mtume (saw) : Ni amali gani anayoipenda zaidi Mwenyezi Mungu? Akasema: “ni kuswali swala katika wakati wake” .[2]
Ndio maana sala ilikuwa alama ya kutofautisha Waislamu. kwani mnafiki inakuwa nzito kwake,
wala haitekelezi ila kama alivyosema Mwenyezi Mungu:
{Hakika wanaafiki wanamhadaa Mwenyezi Mungu, naye anawahadaa, na wanaposimama kuswali husimama wakiwa wavivu}.
[An-Nisaa: 142]
Na kafiri hukanusha uwajibu wake na kuiacha moja kwa moja, na ndio maana Mwenyezi Mungu Mtukufu akaahidi adhabu kali kwa mwenye kuacha swala, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu.
"Kila nafsi itafungika (Motoni) kwa (amali mbovu) ilizozichuma 39. isipokuwa watu wa kuliani (watu wa kheri) 40. (Hao watakuwa) katika Mabustani, wakiulizana 41 . Juu ya watu wabaya ( wawaambie): 42. "Ni kipi kilichokupelekeni Motoni? 43· Watasema: "Hatukuwa miongoni mwa waliokuwa wakisali ".
[Al-Muddathir: 38-43]
Na Mwenyezi Mungu alisema kuhusu moto huo wa saqari:
“Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar: “Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?27 .Haubakishi wala hausazi. 28.Unababua ngozi iwe nyeusi. 29.Juu yake wapo kumi na tisa. 30."
[Al-Muddathir: 26-30]
Katika Hadithi hii, Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) ametueleza juu ya hukumu ya kupuuza Swalah, na kubainisha kuwa ni kitengenishi baina ya Muislamu na kafiri. “Baina ya mtu na ushirikina na ukafiri ni kuacha Swala ”. Na hii inafanana na kauli yake aliposema “Ahadi iliyo baina yetu na wao ni Swala, basi mwenye kuiacha amekufuru.”[3] Na Umar akasema: “Hakuna nafasi katika Uislamu kwa mtu anayepuuza Swala) [4]. Na Abdullah bin Shaqiq, Mwenyezi Mungu amrehemu, alikuwa akisema: “Maswahaba wa Muhammad (saw), hawakuona matendo yoyote kuwa ukafiri kama kuacha swala”. [5]
MAFUNDISHO
1. wanawazuoni wameafikiana kwa kauli moja kwamba mwenye kuacha Swalah kwa kukanusha wajibu wake basi huyo ni kafiri na ameritadi, na wamekhitalifiana kuhusu mwenye kuiacha kwa uvivu na uzembe. Kuna waliosema kuwa ni: kafiri, na wengine wakasema: huyo ni fasiqi-muovui alinganiwe kutubia, la sivyo atauawa, na ikasemwa kuwa: ni fasiqi asiuawe. Na Mwislamu wa kweli anayemjua Mola wake Mtukufu na kumuamini Mtume Wake, (saw), hawi katika nafasi ambayo wanazuoni wamehitilafiana baina ya kumkufurisha na ufasiq, bali atafanya haraka kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu na kuwa karibu nae kwa kutenda matendo ya juu zaidi baada ya kutekeleza wajibu.
2. Omar Ibn Al-Khattab alipochomwa mkuki ambao ilikuwa sababu ya kifo chake, na maswahaba walimuingiza nyumbani kwake, wakajaribu kumuamsha kutoka katika kuzimia kwake ikashindikana, wakasema: Swala pekee ndiyo itamuamsha, wakaita: Swala! Ewe Amirul-Muuminin! Akasema: “Ndio, na hakuna sehemu katika Uislamu kwa mwenye kupuuza Swala.” Akaswali huku damu ikichuruzika kutoka kwenye Jeraha Lake. Je! Maswahaba walikuwa na hamu ya kuswali kwa kadiri gani? [6]
3.
Imesimuliwa kutoka kwa Abdillsh bin A`mru bin al aswii, Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kutoka kwa Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) kwamba siku moja alitaja swala na kusema:
" mwenye kuhifadhi swala atakuwa na nuru na hoja – utetezi- na kuokoka siku ya kiamah, na asiyehifadhi swala hatakuwa na nuru wala hoja – utetezi- wala kuokoka, na siku ya kiamah atakuwa pamoja na Qaruun na Fir`Aun na Haaman na Ubai Bin Khalaf.) [7]"
Ibn al-Qayyim, Mwenyezi Mungu amrehemu, amesema: “katika hadithi hii Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) amewataja watu hawa wanne, kwa sababu ni vingozi wakuu wa makafiri. Na hapa kuna nukta muhimu, nayo ni kwamba mwenye kuacha kuhifadhi swala, ima anashughulishwa na mali, au ufalme, au uongozi, au biashara, hivyo basi atakueshughulishwa na mali yake na akaacha kuswali basi siku ya kiama atakuwa pamoja na Firauni, na atakaeshughulishwa na uongozi na utumishi akaacha kuswali basi atakuwa pamoja na Haman, na atakueshughulishwa na biashara yake akaacha kuswali basi atakuwa pamoja na Ubay bin Khalaf” [8]
4. Vipi mtu anaacha Swala hali ya kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ameifanya ni kafara ya dhambi na maovu ya mja?!
Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani ziwe juu yake):
“Je, mmeona lau kuna mto katika mlango wa mmoja wenu, akawa akioga ndani yake kila siku mara tano je atabakiwa na uchafu wowote?” maswahaba Wakasema: "Haitabaki chochote katika uchafu wake." Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) Akasema: huo ndio mfano wa Swalah tano, Mwenyezi Mungu hufuta dhambi kupita swalah .[9]"
5. Ibn Masoud, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, amesema kuhusiana na swala ya jamaa: “na hakika Mwenye kuacha swala tulikuwa tukimuona kuwa ni mnafiki wa wazi, na hakika mtu alikuwa akiletwa kwa kukokotwa/ kubebwa na watu wawili kisha anasimimishwa kwenye safu- ili aswali jamaa-. ”[10]
6. Mshairi alisema:
uwito wa sala juu ya minara = katika majira ya alfajiri ya asubuhi na usiku utulivu
ni uwito unaoleta uhai kwa ulimwenguni=,kwa wakazi wa vijijini na mijini
Na ni mwito kutoka mbinguni kwenda duniani = kwa walio juu ya ardhi na ndani
Na ni mkutano baina ya Malaika na imaani = na Waumini bila ya idhini
Na ni sababu ya kuelekea katika kufaulu, na kwa kheri = kisha na haki, na uwongofu, na wema.
7. mwingine alisema:
mja mwema huisahau dunia yake kwa kuidharau = na kuona wazi uhalisia wa nafsi yake
mbavu za waja wema huachana na vitanda vyao, = na kumaliza usiku wao wakiwa wamesimama kuswali na kusujudu.
Katika usiku wa kiza huiendea swala, wakichochewa na= shauku kwa mwenye nguvu na vilema.
Wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu katika mihrab yake = hadi alfajiri inakaribia kuingia
mpaka adhana inapoadhiniwa = huelekea kwa Mwenyezi Mungu mola wao.
Je umewahi kuona raha inayokuwepo wakati umesimama= mbele ya mola wako kwa unyenyekevu na heshima?!
Na uliwahi kuona waja wema wakiwa katika safu moja kwa unyeyekavu, = na wanavyotoa salamu?!
المراجع
- mepokewa na Al-Tirmidhiy (2616) na Al-Nasa’i (11330).
- Imepokewa na Al-Bukhari (527) na Muslim (85).
- Imepokewa na Al-Tirmidhiy (2621), Al-Nasa’i (463) na Ibn Majah (1079).
- Imesimuliwa na Malik katika Al-Muwatta (1/39) na Al-Daraqutni (1750).
- Imepokewa na Al-Tirmidhiy (2622).
- Imesimuliwa na Malik katika Al-Muwatta (1/39) na Al-Daraqutni (1750).
- Imepokewa na Ahmad (6576), na Shuaib Al-Arna`ut amesema: sanad yake ya upokezaji ni hasan.
- “Swala na Hukumu za mwenye kuiacha” cha Ibn Al-Qayyim (uk. 51).
- Imepokewa na Al-Bukhari (528) na Muslim (667).
- Imepokewa na Muslim (654).
1. Malik bin Al-Hawairith, Mwenyezi Mungu amuwie radhi , akiwa na kundi la maswahaba zake kutoka Bani Al-Layth walimtembelea Mtume, rehema na amani ziwe juu yake. Wote walikuwa ni vijana waliokaribiana katika umri, walikaa kwa Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) kwa muda wa siku ishirini, wakijifunza na kuifahamu Dini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alipohisi kuwa wamezitamani familia zao, akawauliza kama waliacha jamaa zao, wakamwambia waliwaacha katika jamaa zao.
2. Walipomwambia, akawaamrisha warejee kwao, na hiyo ni kwa sababu ya upole na huruma ya Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) kwa Waumini, kwani Mwenyezi Mungu alishasema kuhusu hilo. ndani yake:
" Hakika amekwisha kujieni Mtume kutokana na nyinyi wenyewe; yanamhuzunisha yanayo kutaabisheni; anakuhangaikieni sana. Kwa Waumini ni mpole na mwenye huruma" . 128
[At-Tawbah: 128].
Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) aliwaamrisha warudi kwenye familia zao, Kwa sababu hiyo ilikuwa baada ya ufunguzi wa Makka; kwani Kuhama kulikatishwa na ufunguzi wa Makka; Kwa kauli yake aliposema : “Hakuna kuhama baada ya ufunguzi wa makkah”, [1]kwa hiyo makazi ya Madina yakawa ni ya hiari, kwa aliyetaka alibaki, na anayetaka alirejea kwa watu wake baada ya kujifunza anachohitaji kutoka katika elimu na dini, na kufundisha watu wake.[2]Aliwaruhusu warudi na kuwaamuru wafanye hivyo, Kwa sababu alijua kuwa wamejifunza yale yanayowatosheleza katika mambo ya dini yao ya fiqh na tauhidi, la sivyo, asingewaacha warudi kwenye familia zao achilia mbali kuwaamuru wafundishe.
3. Ndio maana akawaamrisha wawafundishe watu wao yale waliyowafundisha katika Dini ya Mwenyezi Mungu, Bali akawaambia kuwa elimu peke yake haitoshi, basi kila mmoja anatakiwa kuamrisha familia yake na kuwachunga, kwani wao ni wenye kuulizwa na kuhesabiwa kwa familia zao,.” Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Na waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo."
[Twaha: 132].. ”
Na Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) amesema: “Kila mmoja wenu ni mchunga na anawajibika kwa kundi lake.”[3] kama ilivyo vile kufundisha ni wajibu, ndivyo ilivyo wajibu kufanyia kazi elimu.[4]
4. Kisha Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akaweka kanuni pana katika dini na hukumu zake, nayo ni kumfuata Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) na kumfuata katika swala na namna zake na hukumu zake, na yale yanayosemwa ndani yake, na yanayoibatilisha, na yanayolazimu sijda ya kusahau; kwani hakika Matendo ya Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, ni maelezo yanayobainisha kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu aliyoitaja kwa ujumla katika Qur’ani Tukufu; kwani Aayah za Qur-aan hazikuja zikifafanua kwa upana hukumu za swala, idadi ya rakaa zake, nyakati zake, nguzo zake, sunna na sura zake. Bali ilikuja zikiamrisha swala ihifadhiwe kwa muda wake, Zikiacha kauli za Mtume na matendo yake yabainishe kwa upana na uwazi, na ndio maana yeye, amani iwe juu yake, alisema: “Swalini kama mlivyoniona mimi nikiswali.”Vivyo hivyo inatumika katika sheria zote na hukumu nyinginezo, Katika Hijja, Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) anasema: “Hebu chukueni ibada zenu, kwani sijui nitahiji baada ya Hija hii” [5]na Wanazuoni wameafikiana kwamba ikiwa vitendo vya Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) ni ufafanizi kwa jambo lilokuja kwa jumla bila ufafanuzi, kama vile kuswali, kufunga na kuhiji, basi matendo hayo yatachukuliwa kama ni wajibu, isipokuwa ziwepo dalili mahususi zinaonyesha kuwa si wajibu[6]Na wajibu huu ni juu ya Ummah wote, kwa sharti ithibitike kuwa Mtume, (Rehma na amani ziwe juu yake) aliendelea na kitendo hicho maalum, basi itakuwa ni wajibu kwa Ummah wake, Ama kile ambacho hakijathibitishwa kuendelea nacho, basi si wajibu.[7]
5. Kisha Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akawausia itakapofika wakati wa swala, mmoja wao aadhini, na mkubwa wao awaswalishe.Na asili katika uimamu ni kwamba anaesoma vizuri Qur'ani ndo anapaswa kuwasalisha, kama ilivyo katika hadithi ya Abu Masoud al-Ansari, Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kwamba Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, amesema: awaswalishe watu Yule anaejua kusoma vizuri zaidi Kitabu cha Mwenyezi Mungu kuliko wote, basi ikiwa wako sawa katika kusoma, basi mjuzi zaidi yao katika Sunnah, na ikiwa ni sawa katika Sunnah, basi aliewatangulia katika kuhama, na ikiwa ni sawa katika kuhama, basi aliewatangulia katika kuingia kwenye uislamu[8],Amr bin Salamah, Mwenyezi Mungu amrehemu, aliwaswalisha watu wake wakati wa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake akiwa na umri wa miaka sita. Kwa sababu alikuwa vizuri katika usomaji wa qur`an kuliko wote,[9] Bali Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) aliwaamrisha kuwatangulia wakubwa wao, kwa sababu alijua kuwa kisomo chao kinakaribiana; kwa Ushahidi wa kauli yake katika riwaya ya Muslim: “Walikuwa wanakaribiana katika kusoma”[10] na waliingia katika Uislamu wakati mmoja, mara nyingi watu wa namna hiyo Kuna uwezekano mkubwa kwamba usomaji wao na elimu ya Sunnah ni sawa, kwahiyo ndio maaana akatangulizwa mkubwa wao.
MAFUNDISHO :
1. Katika hii hadithi kuna ubainifu kuwa Maswahaba Mwenyezi Mungu awe radhi nao, walijali sana swala la kutafuta elimu na kujifunza hukumu mbalimbali za kisheria, na kwamba waliacha familia zao na makazi yao kwa ajili hiyo, na hii ni kutokana na yale yaliyotua ndani ya nafsi zao juu ya fadhila na ukubwa Wake, hivyo basi mtu asikose ujira huo, hasa katika zama hizi ambazo kutafuta elimu kumemjia bila ya taabu wala shida za safari.
2.Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) aliwajali sana vijana na alikuwa na shauku ya kuwaelimisha kisha kuwatuma kama mabalozi na walinganizi kwa watu wao; kwa sababu Vijana ndio nguzo ya ummah huu na chanzo cha maendeleo yake, hivyo basi Maslahi yao lazima yaelekezwe kwenye kazi, na ulinganiaji na kujenga ummah.
3.Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alielewa hali za kisaikolojia za vijana na akaelewa mahitaji yao ya kihisia, na kwa sababu hiyo akawaruhusu warudi kwenye familia zao, hivyo basi inampasa mlinganiaji au mwalimu kuchunga mahitaji ya vijana na kuzingatia hali zao na kuchukuliwa tahadhari maalumu kwa ajili yao.
4.mlinganiaji, na mwalimu, na mlezi lazima awe mpole mwenye huruma, ambaye ulinganiaji wake haupingani na mahitaji ya lazima ya watu, bali awahurumie kwa kadiri inavyowezekana, na ajitahidi kutumia nyakati za uchangamfu wao katika yale yanayowanufaisha, na kuwapa faraja na nafasi inayoendana na miili na roho zao.
5.Miongoni mwa busara za mlinganiaji na mlezi ni kwamba asimtwike mtu yeyote kile asichoweza kustahimili, bali azingatie nguvu na uwezo wake wa kutekeleza yale aliyoamrisha kidogo kidogo.
6. inamampasa Mtu abaki na familia yake kadiri awezavyo, na asiwe mbali nao, ndio maana Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alimuamuru msafiri pale atakapomaliza haja yake arudi katika familia yake .[11] Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) amehusia katika hadithi hii na katika hadithi nyinginezo kufikisha ujumbe wa dini hii na kueneza ulinganiaji wake, na katika hilo kuna kauli ya Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) isemayo “fikisheni kwa niaba yangu hata kwa ayah moja”[12]; hivyo basi Mwenye kulingania ni mfikishaji kutoka kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake (Rehma na amani ziwe juu yake) anakuwa kwa watu amesimama katika cheo cha Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akiwalingania watu kwenye kheri na kuwakataza maovu na kuwaeleza sheria za kidini na kuwafahamisha hukumu zake. Je Nani asingependa kuwa katika daraja hilo?!
8.Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) ameeleza kuwa kulingania kunahitajia amri na subira katika utekelezaji, na si kubainisha maamrisho na makatazo tu, kwani kiasi Mtume rehema na amani ziwe juu yake alivumilia ili kufikisha sheria za Mwenyezi Mungu,?! Hivyo basi walinganiaji na wanachuoni wanapaswa kuwa na subira na na kuhimizana katika hilo ili kutekeleza sheria ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.
9. Ubainifu wa hukumu za Sheria umekabidhiwa kwa Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) peke yake, si kwa maneno ya watu, wala si kwa kutumia akili tu, na wala si kwa matamanio; kwani Ibada lazima itegemee matendo na maneno ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake, hakuna kuzidisha wala kupunguza katika yale aliyoyawekea sheria.
10. Kumfuata Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) katika Sunnah zake ndio njia ya uzima na uwongofu; kwani Kupitia kwayo Muislamu anajua namna sahihi ya swala, na muda wake, na hukumu zake, na nguzo zake na sifa zake, na akaweza kudhibiti hukumu za ibada nyinginezo, kama zaka, saumu, kuhiji na nyenginezo. Na lau Muislamu angeliacha kufuata Sunnah za Mtume (saw), basi atabaki ameduwaa na kupotea njia.
11. Imejumuishwa katika kumfuata Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) katika swala ni kumfuata katika kukubali kutumia ruhusa za kisheria, hivyo basi katika kumuiga Mtume vizuri ni pale mgonjwa anaposali kwa kukaa au kwa kuegemea kulingana na hali yake, na msafiri na mgonjwa wafungue saumu ikiwa watapata madhara kutokana na saumu hiyo, na msafiri aswali kwa kuunganisha, na ruhusa nyinginezo ambazo alizotumia Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) wakati wa uhai wake, na akasema: “Mwenyezi Mungu hupenda kutumiwa ruhusa zake kama anavyochukia kuasiwa[13]”
12. Hadithi hii inaelekeza kumuheshimu mkubwa na kumuweka kataka daraja na hadhi inayomfaa katika mambo yanayozingatiwa kisheria, na hiyo ni wakati ambao haitoleta uvunjaji wa sheria; kwani Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alifanya umri kuwa kigezo kuwa imaamu ikiwa watu wako sawa katika vigezo vya uimaamu, kama vile kusoma qur`an vizuri, kuwa na elimu ya sheria, na kutangulia katika Uislamu.
Marejeo
- Imepokewa na Al-Bukhari (2783) na Muslim (1353).
- Tazama: “Fath al-Bari” cha Ibn Hajar (13/ 236).
- Imepokewa na Al-Bukhari (2409) na Muslim (1829).
- Tazama: “Sharh Riyadh as-Salihin” cha Ibn Uthaymiyn (4/148).
- Imepokewa na Muslim (1297).
- Tazama: “Sharh Sahih Al-Bukhari” cha Ibn Battal (10/345), “Riyad Al-Afham fi Sharh Umdat Al-Ahkam” cha Al-Fakhani (2/167).
- Tazama: Fath al-Bari cha Ibn Hajar (13/237).
- Imepokewa na Muslim (673).
- Imepokewa na Al-Bukhari (4302).
- Imepokewa na Muslim (674).
- “Sharh Riyadh Al-Salihin” cha Ibn Uthaymiyn (4/147).
- Imepokewa na Al-Bukhari (3461).
- Imepokewa na Ahmad (5866).
Hadith hii ni moja ya hadithi muhimu sana juu ya sheria ya Swala, kwani imejumuisha nguzo na wajibu muhimu zaidi za swala, na wanazuoni wa sheria waliizingatia sana hadithi hii na wakaitumia kama ushahidi katika mambo mengi ya sheria, na ni mashuhuri sana kwa wanachuoni kama: “Hadithi ya mwenye kuswali vibaya. ”
1. Mtu mmoja aliingia msikitini akaswali, na Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alikuwa akitazama swala yake, mtu huyo alipomaliza kuswali akaja kwa Mtume (saw). na akamsalimia, kisha Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akamuamrisha kurudia na kwamba swala yake haijakubaliwa wala haifai.
Na lau ingelikuwa inafaa, asingelimuamrisha kurudia, bali angemtahadharisha tu na makosa aliyoyafanya ili kuyaepuka baada ya hayo.
2. Yule mtu akarudi na akaswali kama alivyoswali mara ya kwanza, na kwa sababu hiyo, aliporejea kwa Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akamuamuru arudie tena, basi yule mtu akaenda akaswali kama swala yake ya kwanza. na Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akamuamrisha arudie, basi mtu huyo akamwambia kuwa haboreshi zaidi ya hiyo swala, na akamuomba Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) amfundishe kuswali, Na ni makosa gani aliyoyafanya, yaliyopelekea akaharibu swala yake.
Mtume, Rehema na Amani zimshukie, hakumueleza alichokosea tangu mwanzo, labda kwa sababu Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alidhani kwamba mtu huyo anazijua hukumu za swala, na wajibu wake na nguzo zake, lakini akakiuka elimu yake, hivyo akamuamuru kurudia, pale alipomwambia mtu huyo kwamba haboreshi zadi ya hapo akamfafanulia hukumu zake, au huwenda ni kwa sababu yeye, amani iwe juu yake alidhani ikiwa atamuamrisha mtu huyo kurudia mara kwa mara, kisha akamueleza sababu ya yeye kumrejesha basi hiyo itasababisha kueleweka zaidi na asisahau Baada ya hapo kamwe. [1]
3. Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akamwambia akitaka kuswali aanze na takbira ya kufungua swala. Maana yake ni kuwa ni nguzo ambayo bila hiyo swala haifai, kwani Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alimfundisha mtu yule yanayopelekea Swala yake iwe sahihi, na hii ilikuwa sehemu ya kujifunza , si vyema kuongeza katika nguzo Sunnah na mfano wa hayo.[2]Mtume sawa hakutaja nia kwa sababu mtu huyo aliijua; kwani Moja ya misingi ya dini ambayo hakuna asiyeijua ni kwamba matendo ni kwa nia, iwe Katika swala, zaka na ibada zote.
4. Kisha akamuamrisha asome yaliyo mepesi zaidi kwake katika Qur’ani, na hii haimaanishi kuwa inajuzu kwake kusoma chochote anachotaka, Bali mchanganuo wa hayo upo katika Hadiith nyingine kwamba ni wajibu. kusoma suratul fatiha na kwamba: “Hapana Swala kwa asiyesoma Suratul Fatiha ya kwa usahihi” [3]hivyo basi Kinachokusudiwa katika mepesi ndani ya Qur’an ni Al-Fatihah, Kwa sababu Mwenyezi Mungu Mtukufu Amewarahisishia kuihifadhi wanaume, wanawake na watoto, au kinachokusudiwa baada ya Al-Fatihah katika kisomo, kwani mtu yule alikuwa anajua kuwa kusoma Al-Fatihah ni nguzo ya Swala, ndio maana akamuelekeza kusoma yale yanayofuata ikiwa anaweza kufanya hivyo.[4]
5. Kisha Mtume (rehema na amani ziwe juu yake) akamuamrisha arukuu na atulizane katika rukuu, na awe amenyooka wakati wa kuinuka, na atulizane katika kusujudu. Na makusudio ya maelekezo haya ni kubainisha kuwa kutulizana na kutokuwa na haraka katika swala ni moja ya nguzo za swala ambayo bila ya hiyo swala haisihi, na ndio maana akamuamrisha arudie tena.
Na Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) aliikosoa swala isiyo na utulivu, na akasema: “hiyo ni swala ya mnafiki; Hukaa na kulitazama jua hata likiwa baina ya pembe mbili za Shetani, hapo ndo anainuka na kuidonoa swala rakaa nne bila kumtaja Mwenyezi Mungu ndani yake ispokuwa kidogo tu.[5]” Na Maana ya kudonoa ni: kuswali kwa kasi katika rakaa zote na kutokuwa na utulivu, kama anavyodonoa kuku.
Na Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) ametaja katika hadithi hii baadhi ya nguzo za swala ambazo swala haikubaliki bila ya hizo, na akaziacha nguzo nyinginezo, kama: nia, kukaa katika tashahhud ya mwisho, na kutoa salamu; Kwa sababu mtu huyo alijua mambo haya, na Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) alimuona akiyafanya, lakini mambo mengine yalikuwa hayapo kwake, basi Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akamfundisha kufanya yale aliyokuwa hayajui.[6]
MAFUNDISHO:
1.Hadithi hii imetupa faida kuwa Muislamu akiingia msikitini na akakuta kuna watu wamekaa ndani yake basi ni vyema kwake kuswali swala inayojulikana kama maamkizi ya msikiti kwanza kisha awasalimie waliokaa.
2.Ni wajibu kwa Muislamu kujifunza elimu ya kisheria ambayo kwayo ibada yake hukubaliwa; Ili kutobatilisha ibada yake.
3.inapendeza kwa mwanachuoni, msomi na mjuzi wa sheria na mlinganiaji akae msikitini na watu wazoee kukusanyika kwake kwa ajili ya kujifunza dini yao, na akiwapa mawaidha na kuwahimiza kutenda mema, na kuwabainishia swala ya Mtume (saw) , kama ilivyo.
4.Ikhlas (yaani kumkusudia Allah) ni katika ibada na kumuiga Mtume katika sunnah zake ni sharti katika kukubaliwa matendo, kama ilivyo kukosa sharti la ikhlasi kunabadilisha matendo, vivyo hivyo kwenda kinyume na sunnah za Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) hupelekea kutokubalika matendo hata kama nia ni njema.
5.inafaa kwa mlinganiaji na msomi wa sheria kuchelewesha kubainisha jambo katika kikao cha kielimu kwa sababu maalumu; Kama vile kumfanya msikilizaji awe na shauku ya kusikia hukumu ya kisheria katika hilo jambo, au kupupia watu kukusanyika ili kusikia kutoka kwake, na kadhalika.
6. Hadithi hii inaashiria kuwa inapendeza kutoa salamu na ni wajibu kuitikia, na kwamba inapendeza kuirudia ikiwa mtakutana mara kwa mara, hata ikiwa muda mchache umepita, na kwamba ni lazima kuitikia kila wakati.
7.Katika Hadithi hii kuna ushahidi kwamba mwalimu inabidi awe mpole kwa wanafunzi na wasiojua, na kuwafundisha kwa utaratibu, na kuwabainishia masuala mbalimbali ye kielimu, na kufupisha makusudio, na kutosheka kwa kuwapa elimu kidogo kidogo, hasa kwa kuanza na mambo muhimu ambayo yanaweza kukaririka mapema, na kufanyiwa kazi.[7]
8.Ufunguo wa swala ni takbira, nayo inaashiria kwamba tayari umeshaingia kwenye swala kwa kusema: “Allah Akbar” yaan Mungu ni mkubwa,” ni haki ya kumfanya mkuwa kubwa kuliko dunia na vilivyomo ndani yake, hivyo basi hautakiwi kushughulishwa na dunia ukaacha unyenyekevu na utulivu katika swala.
9. Hadithi hii inabainisha kuwa vizuri kuwafanyia uwepesi Waislamu na wala haikugawiwa kwa yale ambayo ni magumu kwao, basi Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwamrisha mtu huyo kusoma katika lililo jepesi,hivyo ni kinyume cha sheria kudumu kwa baadhi ya maimamu katika kusoma sura ndefu katika swala na kuwatilia uzito watu, na akasema: “ Pindi mmoja wenu akiwaswalisha watu basi aifanye nyepesi swala yake, Hakika miongoni mwao wapo walio dhaifu, wagonjwa na wazee, na ikiwa mmoja wenu ataswali pekeyake basi na aifanye ndefu kiasi apendavyo.[8]”
10. Utulivu ni nguzo katika swala, bila ya utulivu swala si sahihi, na makusudio yake ni kuelewa maana ya anachokisema Muislamu ndani ya swala yake ,miongoni mwa nyiradi na dua, na sio harakati tu anazozifanya Muislamu. , kuinuka na kuinama.
11. Miongoni mwa kuusiana haki na kuamrisha mema na kukataza maovu, ni Pamoja na kuwahadharisha na kuwaelimisha wajinga
Imepokewa kutoka kwa Zaid bin Wahab Allah amrehem amesema: Hudhaifa (ra) alimuona mtu hatimizi rukuu zake wala sujuud zake,akamwambia: Wewe hujaswali, na kama utakufa katika hali hii basi utakufa katika maumbile isiyokuwa yale ambayo Allah kamuumba Muhammad Rehma na amani ziwe juu yake. Na haya ni makemeo makali sana.[9]
12. Mshairi akasema:
Unasali sala sawa isiyokuwa na moyo = inayo mfanya mtu astahiki kuadhibiwa.
Ole wako! Wajua ni nani unae msemesha hali ya kupuuza? =Na mbele ya yule unaye muinamia bila ya unyenyekevu? .
Unamsemesha kuwa wewe tu tunakuabudu hali ya kumuelekea= mwenginewe katika swala yako pasina dharura ya kufanya hivyo!.
Na kama angekujibu umsemeshae bila ya kukutizama= basi ungepasuka kwa hasira naghera juu yake.
Marejeo
- Tazama: “"Sharah Almushkat Alkashif Ean Haqayiq Alsanani"cha Al-Twibi (3/977), “Al-Tahdeh Lash-i-Sharh Al-Jami’ Al-Sahih” cha Ibn Al- Mulqin (30/313), “Fath Al-Bari” cha Ibn Hajar (2/281).
- Tazama: "'Iikmal Almuealim Bifawayid Muslimin"cha Qadhi Iyadh (2/282).
- Imepokewa na Al-Bukhari (756) na Muslim (394). Tazama: “Maalim Al-Sunan” cha Al-Khattabi (1/210), “"'Iikmal Almuealim Bifawayid Muslim” cha Al-Qadi Iyad (2/282),
- ““Al-Mufhim Limaa 'Ashakala Min Talkhis Kitab Muslimin" . ” cha Al-Qurtubi (2/29).
- Imepokewa na Muslim (622).
- Tazama: “sharh Al-Nawawi alaa Muslim” (4/ 107).
- sharh Al-Nawawi alaa Muslim (4/ 108, 109).
- Imepokewa na Al-Bukhari (703) na Muslim (467), kwa kutoka kwa Abu Hurairah (ra)
- Imepokewa na Al-Bukhari (791).
1. Ametaja Mtume Rehema na Amani zimshukie kuwa mwenye kuswali Swalah ambayo ndani yake hakusoma Al-Fatiha, ni pungufu na haijakamilika.
Upungufu huu ni ukosefu wa afya unaoathiri kukubalika kwa kazi. Kwa sababu yeye, amani iwe juu yake, amesema: “Hapana sala kwa asiyesoma Fatiha ya Kitabu”[1]
Al-Fatihah iliitwa mama wa Qur’ani kwa sababu ndio asili yake, na maana za surah zote za Qur’ani – kuanzia kumhimidi Mwenyezi Mungu, kujitolea kwake, kutia moyo, vitisho, na hadithi za waliotangulia. rejea, kama vile Makka ilivyo Ummul-Qura kwa sababu ndio asili yake[2].
2. Abu Huraira, msimuliaji wa hadithi, aliulizwa kuhusu usomaji wake kwa mtu anayeswali katika jamaa, akamwambia kwamba aisome kwa siri. Na usemi huu, ijapokuwa ulisitishwa kwa Abu Hurairah, Mwenyezi Mungu amfikishie rehema na amani, ni katika hukumu ya marfoo’; Kutoka kwa Ubada bin al-Samit, Mwenyezi Mungu amfikishie rehema na amani, amesema: Tulikuwa nyuma ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika Swala ya Alfajiri, basi Mtume wa Mwenyezi Mungu. Rehma na amani zimwendee, alisoma akakwama, kisha akatuuliza : Huenda mnasoma nyuma yangu? Tukasema: Ndio, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu.Akasema: “Msifanye hivyo ila ufunguzi wa kitabu Kitabu (yaani alhamdu); kwani Hakuna sala kwa asiyeisoma”[3]
3. Kisha Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amfikishie rehema na amani, akatoa sababu ya kusema hivyo. Na ni kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema katika Hadithi Qudus kwamba aligawanya usomaji baina yake na mja wake katika nusu mbili.
Na mgawanyiko huu ni mgawanyiko wa maana, ambayo ni kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu, amesema; Ikiwa mja atasema:
“Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote”
[Al-Fatihah: 2]
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: Mja wangu amenisifu.
Kinachomaanishwa na uainishaji huo inaweza kuwa nusu ya surah ni ibada, sifa na utukufu wa Mwenyezi Mungu, na nusu nyingine ni ombi na dua, na Mwenyezi Mungu Mtukufu ameahidi majibu yake, na mada ya uainishaji ni kauli yake.: Sentensi ya kwanza pamoja na yaliyotangulia ni sifa, sifa, utukufu na kujitolea kwa Mwenyezi Mungu, na sentensi nyingine na inayofuata ni kutafuta msaada wa Mwenyezi Mungu na kutafuta mwongozo kutoka Kwake[4]
Na kuita swala kuwa ni kusoma Al-Fatihah hii kitaalamu ni kutaja sehemu muhimu zaidi katika kitu chenye sehemu nyingi, kama vile kauli ya Mwenyezi Mungu alivyosema: Wala usitangaze Swala yako kwa sauti kubwa, wala usiifiche kwa sauti ndogo, bali shika njia ya kati na kati ya hizo. [Al-Isra: 110] na Maana ya swala hapa ni kisomo yaani “Usisome kwa sauti kubwa”[5]
4. Kisha akamjulisha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba ikiwa mja atasema:
“Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote”
[Al-Fatiha: 2],
Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “Mja wangu amenisifu.” Na ikiwa mja atasema:
“Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.”
[Al-Fatihah: 3]
Ali ni mja wangu.
” Na iwapo atasema: “Mwenye kumiliki Siku ya Kiyama”
[Al-Fatihah: 4] ]
Yeye, Ametakasika, anasema: Mja wangu amenitukuza.
Sifa na utukufu ni maneno yanayohusiana, ambayo yote yanakubali kwamba ni ya sifa na kutaja sifa. Walakini, sifa sio maalum kwa kitendo. Ndio maana akasema:
{Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote}
[Al-Fatihah: 2];
Tunamhimidi kwa sababu Yeye ni Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote. Ama sifa ni kutaja sifa za mwenye kusifiwa zinazostahiki kusifiwa. Kwa ajili hiyo Mwenyezi Mungu Mtukufu akazitaja pale mja aliposema: {Mwingi wa rehema! . Kama vile alipotaja sifa ya rehema alikutana nayo kwa sifa, na alipozungumzia Siku ya Mwisho na kwamba yeye ndiye mmiliki na mtawala wake, aliifaa hiyo habari ya utukufu ambayo ndani yake kuna kauli ya tukufu na ukuu. [6].
5. Iwapo mja atasema :
“Wewe tunakuabudu na Wewe tunakuomba msaada”
[Al-Fatihah: 5]
Mola Mtukufu amesema: “Haya ni baina Yangu na mja Wangu, na mja Wangu atapata alichokiomba”. ; Ambapo aya hiyo ilijumuisha unyonge kwa Mwenyezi Mungu na ukosefu wake, ibada ya kuMuabudu Yeye peke yake, na kutafuta msaada Wake, na ibada ni jina la kina kwa kila anachokipenda Mwenyezi Mungu na anachoridhika nacho kwa maneno na vitendo, vya nje na vya ndani, na ni pamoja na kumtukuza Mungu Mwenyezi na kuonyesha uwezo wake wa kutimiza swala lake.[7]
6.Wale ambao wameanguka katika wao: Mayahudi; Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwakasirikia walipoijua haki na wakaiendea na kuipotea, na wapotovu: Wakristo; Ambapo walikwepa ujinga na uzushi katika Dini bila ya Elimu.[8]
MAFUNDISHO:
1. Al-Fatihah ni mama wa Qur’an, na ndio asili yake, na maana zote za surah zinarejea humo. Mwenye hekima ni yule anayejua maana zao, anabainisha hukumu zao, na kubainisha siri za upendeleo wao na utaalamu wao.
2. Inawezekana kutoa katika surah hii Elimu zote za dunia na akhera; Na hiyo ni kwa sababu imesemwa: katika surah hii ni elimu ya sifa, elimu ya uungu, elimu ya uchamungu, elimu ya walimwengu, elimu ya rehema, elimu ya ufalme, elimu ya dini, elimu ya ibada, elimu ya kutafuta msaada, elimu ya uongofu, njia ya haki, elimu ya neema, na ujuzi wa hasira, na kujua nini cha kuepuka na upotofu.[9]
3. Hadith inaashiria kuwa ni wajibu kusoma Al-Fatiha katika kila rakaa ya swala; Haijuzu kwa Muislamu kuswali na kitu kingine chochote.
4. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alirudia kauli yake: “ swala hiyo ni batili" , mara tatu ili aeleweke na kukariri, na kumthibitishia msikilizaji hukumu juu ya hilo. Kurudia ni njia ya kinabii zaidi kuliko aliyoitumia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), na mlinganiaji, na mwalimu anapaswa kuizingatia na kuitumia mara kwa mara.
5. Watu walimuuliza Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amfikishie rehema na amani, kuhusu hukumu ya kusoma Al-Fatiha kwa anayeswali nyuma yake. Inaweza kuwa na kanuni yake tofauti, na ndio maana Abu Hurayrah, Allah amuwiye radhi, hakuwanyima swali lao; Muislamu hatakiwi kuona haya kuuliza juu ya asiyoyajua, na faqihi na mlinganiaji hatakiwi kuchoshwa na maswali ya muulizaji, hata kama yanarudiwa au kudokezwa katika maneno yake.
6. Mwenyezi Mungu Aliita Al-Fatihah kuwa ni sala kwa sababu ndiyo sehemu muhimu zaidi yake; Muislamu hatakiwi kuipuuza sehemu hiyo muhimu zaidi, ili aisome kwa pupa bila kutafakari na kutafakari.
7. Unaposoma Surat Al-Fatihah katika swala, tafakari mazungumzo na mazungumzo baina ya mwanadamu na Mola wake Mtukufu; Ni wajibu juu yetu kwamba nyoyo zetu ziwe katika hali ya maombi. Ili tupate kusamehewa makosa yetu, na tupate kufaidika nayo; Kwa sababu manufaa yanayotokana na swala ni juu ya Swala ya unyenyekevu na ukamilifu[10]
8. Mwenyezi Mungu Mtukufu hujisifu juu ya waja wake waumini na hufurahi juu yao; Na wakisema: {Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote}, Ametakasika! Anasema: Mja wangu amenisifu, akijifakhirisha kwa furaha, kwani ni kitendo gani kikubwa na chenye matumaini ya manufaa na malipo kuliko kitendo Mungu Mwenyezi afurahi.
9. Inafaa kwa Muislamu kutafakari juu ya kauli yake Mtukufu:
{Wewe tunakuabudu na Wewe tunakuomba msaada}. Imesemwa: Inakusanya siri ya vitabu vyote vilivyoteremshwa kutoka mbinguni. Kwa sababu watu waliumbwa ili kuMuabudu Mungu Mwenyezi. Kama alivyosema Mola Mtukufu: {Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu mimi}
[Al-Dhariyat: 56].
Kwa hiyo, neno hili lilikuwa kati ya Mungu na mtumishi wake; Kwa sababu ibada ni haki ya Mwenyezi Mungu juu ya mja wake, na nusura kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu juu ya mja wake .[11]
10. Mwenyezi Mungu Mtukufu amewaamrisha waja wake wamuombe awaongoze kwenye njia iliyonyooka wanayoifuata Mitume, wakweli na mashahidi, na mwenye kushikamana na njia hii atapata furaha katika dunia hii. na yajayo, na njia yake itanyooka Siku ya Kiyama, na mwenye kujiepusha nayo basi amemkasirikia, na yule anayeijua njia ya uwongofu na haifuati kama Mayahudi, au aliyepotea. njia ya uwongofu; Kama Wakristo na kama washirikina.[12]
11. Mwenyezi Mungu Mtukufu amewausia waja wake kumuomba uongofu wa njia iliyonyooka, na kuwaepusha na njia ya Mayahudi na Wakristo, na hili linahitaji tujiepushe na kuwafuata na kuwaiga. kuwapinga kwa kadiri tuwezavyo kwa njia.
12. Iwapo msomaji atahitimisha katika swala kisomo cha Al-Fatihah, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu anajibu dua yake na kusema: “Hii ni kwa ajili ya mja wangu, mja wangu aliyoyaomba.” Wakati huo, Malaika wanaamini. katika Swalah ya waja, hivyo imefaradhishwa kwa waja kuafikiana nao katika kusalimiana nao; Bima ni ile inayojibiwa kwayo dua.[13]
13. Amesema mshairi:
Unaswali swala isiyo na moyo ambayo kwayo = mtu anastahiki kupata adhabu.
Ole wako! Wamjua unaye msemaesha katika hali ya kupuuza? = Na mbele ya nani unainama bila ya unyenyekevu
Unamsemesha wewe tu tunakuabudu hali ya kuelekea =kwa mwengine pasina dharura yoyote.
Na lau angelikujibu unayemsemesha bila kukutizama =basi ungelipasuka kwa hasira na chuki.
Marejeo
- Imepokewa na Al-Bukhari (756) na Muslim (394).
- Tazama: "'Iikmal Almuealim Bifawayid Muslimin" cha Qadi Iyadh (2/272), ““Al-Mufhim Limaa 'Ashakala Min Talkhis Kitab Muslimin" ” cha al-Qurtubi (2/25), “Tuhfat al-Abrar Sharh Misbah al-Sunnah” cha al-Baydawi (1/286).
- Imepokewa na Abu Daawuud (823) na Al-Tirmidhiy (311).
- Tazama: “Ma’alim al-Sunan” cha al-Khattabi (1/204), “Al-Masalik fi Sharh Muwatta Malik” cha Ibn al-Arabi (2/375).
- Tazama: “Maalim Al-Sunan” cha Al-Khattabi (1/203), “Al-Maysir fi Sharh Misbah Al-Sunnah” cha Al-Torbashti (1/239).
- Tazama: “Al-Masalik fi Sharh Muwatta Malik” cha Ibn al-Arabi (2/376), “Sharh al-Nawawi alaa Muslim” (4/104).
- Tazama: “Al-Mufhim Limaa 'Ashakala Min Talkhis Kitab Muslimin" cha Al-Qurtubi (2/27), “Majmuu’ Al-Fatwa” cha Ibn Taymiyyah (10/149).
- Tazama: “Tafsir Ibn Kathir” (1/140).
- "Al'iifsah Ean Maeani al-Swahiyh na Ibn Hubayrah (8/157)
- “Sharh Riyadh as-Salihin” cha Ibn Uthaymiyn (1/355).
- Fath al-Bari cha Ibn Rajab (7/102, 103).
- Fath al-Bari cha Ibn Rajab (7/102, 103).
- Fath al-Bari cha Ibn Rajab (7/102, 103).
Katika hadithi hii, kuna ubainifu wa uwajibu wa Swala ya Ijumaa kwa Waislamu wote, na onyo dhidi ya kuipuuza, na ubainifu wa adhabu kali anayostahiki mtu hapa duniani kwa kupuuza Swala ya Ijumaa.
Maana ya Hadithi ni kuwa moja kati ya mambo mawili yatatokea bila ya shaka watu kuacha kuswali swala ya ijumaa ama sivyo Mwenyezi Mungu anazipiga muhuri nyoyo zao na kuzifunika, kwa hivyo haziongoki kwenye haki na hazitambui mema na wala hazitakemea maovu. Mpaka zinakuwa pamoja na walioghafilika, na Mwenyezi Mungu anasema:
“Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao, na juu ya macho yao pana kifuniko. Basi watapata adhabu kubwa”
[Al-Baqarah: 7].
Maana ya Hadithi hiyo inathibitishwa na kauli ya Mtume rehma na amani zimshukie: “Mwenye kuacha Swala tatu za Ijumaa kwa kupuuza, Mwenyezi Mungu atapiga muhuri juu ya moyo wake”[1]
Swala ya Ijumaa ni faradhi ya mtu binafsi kwa kila Muislamu wa kiume aliye huru. Mwenyezi Mungu anasema:
“Enyi mlio amini! Ikiadhiniwa Sala siku ya Ijumaa, nendeni upesi kwenye dhikri ya Mwenyezi Mungu, na wacheni biashara. Hayo Ni bora kwenu, lau kama mnajua”
[Al-Jumaa: 9].
Na Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema: "Kila m wenye kubaleghe lazima aende kwenye sala ya Ijumaa, na kila anayekwenda Ijumaa lazima aoge "[2]
MAFUNDISHO:
Muislamu ambaye anamwomba Mwenyezi Mungu Mtukufu uongofu na kufanya vizuri hajiingizi katika chuki na adhabu ya Mwenyezi Mungu, na anaifanya kustahiki kuandikwa kwenye moyo na kughafilika katika kumtii Mwenyezi Mungu.
Mambo makubwa yanahitaji amri ya jumla na katazo kuwekwa hadharani. Kwa ajili hiyo, makatazo ya kuacha jamaa na Ijumaa yanafaa kuwa kwenye mimbari pamoja na mkusanyiko wa watu, na kuongeza umuhimu wake.ni juu ya mlinganiaji, Mwalimu, Mwanasharia na mwenye kuelimisha aweke kila jambo mahali pake, kwani kinachofaa katika masomo kinapingana na kinachostahiki kuwa katika khutba ya Ijumaa, na kadhalika.
Ukali wa mbinu za mlinganiaji, mwalimu na mlezi hutofautiana kulingana na hali. Baadhi ya mbinu zinastahili kuonyeshwa kwa upole, zingine zinastahili ushauri, zingine zinastahili lawama na mawaidha ya upole, na zingine zinastahiki hasira na ukali.
Katika mawaidha, haijuzu kutaja majina ya watu wanao onywa hadharani, hivyo watafedheheka, na kukataza maovu kutaleta ubaya mkubwa kuliko huo, kwani Mtume Rehema na Amani zimshukie, amesema: “Watu wakome” na hakumtaja mtu hata mmoja.
Sala ya Ijumaa ni wajibu kwa kauli moja ya wanavyuoni. Mwenyezi Mungu Mtukufu amemwahidi mwenye kuiacha aina za adhabu na mateso. Jihadharini na kustahiki ghadhabu na adhabu ya Mwenyezi Mungu!
Ijumaa ni siku bora Zaidi iliyochomozewa jua. Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na Amani zimshukie: “Siku bora kabisa ya kuchomoza jua ni Ijumaa, siku hiyo aliumbwa Adam na ndani yake akaingia peponi, na siku hiyo ndio alitolewa peponi”[3] Kwa hivyo, usiiruhusu siku hiyo iwe shahidi baya kwako, bali iwe shahidi mzuri kwako .
Muislamu anatakiwa kuwa makini na mapema kuswali swalah ya Ijumaa, kuoga na kuvaa nguo bora kabisa. Malipo ya hayo ni makubwa.” Akasema Mtume rehma na amani zimshukie: “Anayeoga siku ya Ijumaa akaoga kwa uchafu, kisha akaenda zake msikitini saa ya kwanza, Ni kama ametoa kafara ya ngamia, Na mwenye kwenda katika saa ya pili ni kama amechinja ng'ombe, Na ye yote atakayekwenda saa ya tatu, ni kama amechinja kondoo dume, Na anayeenda saa nne ni kama ametoa kafara kuku, Na anayeenda saa tano ni kama ametoa yai, Basi imamu anapotokea, Malaika huhudhuria wakisikiliza ukumbusho” Mutafaqun Alayhi[4].
Mshairi amesema:
Ee siku ambayo, wema Wake umeumbwa kwake = Na nuru za uwongofu zimekusanyika siku hiyo.
Ni siku ambayo Mwenyezi Mungu ameiwekea = mpango thabiti wa kufuatwa.
Mwenyezi Mungu ameuthibitisha umoja wetu = katika mkutano wa ajabu kabisa
Kila wiki ina khutba = imamu ameongoka vipi anayeisikia
Kwa hakika ni Siku iliyo njema = Na ni siku ya taifa lililokusanyika.
Hakuna siku bora katika masiku = siku bora ni Ijumaa
Umoja wa kiislamu ni nembo inayojulisha = kuwa ummah uko kwenye kilele cha juu kabisa.
Marejeo
- Imesimuliwa na Abu Dawood (1052), al-Tirmidhi (500), an-Nasa’i katika al-Sunan al-Kubra (1668), na Ibn Majah (1125).
- Imepokewa na Abu Daawuud (342) na An-Nasa’i (1371).
- Imepokewa na Muslim (854).
- Imepokewa na Al-Bukhari (881) na Muslim (850).
Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake alipohama kwenda Madina, aliwakuta Ansari wakisherehekea na kucheza katika siku mbili maalum za mwaka ambazo Nazo ni: siku ya Nowruz na siku ya sikukuu[1] , basi Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, alilaani sherehe zao hizo. Basi wakawaambia kwamba siku mbili hizi ni sikukuu za zama za kabla ya Uislamu ambazo walikuwa wakisherehekea na kucheza. Mtume akakemea kuhusu hilo na akawaeleza kwamba Mwenyezi Mungu amewabadilishia kwa siku bora zaidi. Eid al-Fitr na Eid al-Adha.
Na Hadithi inaashiria uharamu wa kusherehekea sikukuu za makafiri na washirikina miongoni mwa Watu wa Kitabu na wengineo, na hiyo ni kanuni mojawapo ya utiifu na ukafiri, kwani ametaja Mwenyezi Mungu kuwa amewabadilishia kwa kilicho bora zaidi kuliko hizo siku mbili, na ubadilishanaji hauwezi kuwa kamili isipikuwa kwa kukiacha kile kilichobadilishwa.
Imeshuhudiwa uharamu huu kwamba sikukuu hizi mbili zimefutika katika Uislamu, kwa hivyo hakuna utajo uliobaki katika zama za Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake wala zama za Makhalifa waongofu. Na lau asingelikataza watu kucheza humo na mfano wa yale waliyokuwa wakiyafanya, basi wangebaki katika desturi hiyo. Tabia hazibadilishwi bila mbadilishaji anayeziondoa, haswa kwa vile asili ya wanawake na watoto, na watu wengi wanatazamia siku wanayoifanya kuwa sikukuu ya furaha na kucheza.[2]
MAFUNDISHO:
Hadithi imeeleza kuwa kusherehekea sikukuu na siku za makafiri hairuhusiwi kwa mujibu wa sharee’ah. Haijuzu kwa Muislamu kusherehekea sikukuu hizi, wala kuwaiga makafiri katika vyakula na vinywaji vyao siku hiyo.
Iwapo itaharamishwa kusherehekea sikukuu za makafiri ambao ibada zao zimefifia na hazitarejea mpaka mwisho wa zama, basi kusherehekea sikukuu za Mayahudi na Wakristo ni haramu zaidi. Kama alivyoeleza Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake kutokana na kuwaiga, alikataza hilo na akaonya.
Hadithi inaashiria uhalali wa tafrija na michezo katika siku za Idi. Ambapo Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake aliifanya badala ya zile siku za kijahilia walizokuwa wakicheza, na Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake aliwaacha mahabeshi wakicheza msikitini kwa mikuki siku ya Idi. Akawa mama wa waumini Aisha, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, akiwatazama mpaka akatosheka [3]
Inajuzu kwa Muislamu kufurahi na kucheza katika siku za Idi, kwa sharti kuwa hakuna haramu katika tafrija yake. Kama kucheza kamari na michezo ya kete, au kuchanganyika baina ya wanaume na wanawake, wala isimshughulishe na kumtaja Mwenyezi Mungu.
Kuonyesha furaha na faraja katika sikukuu ni miongoni mwa ibada za Uislamu, hivyo michezo, tafrija, tafrija za kutembeleana, mafungamano ya kindugu na kupanua maandalizi ya familia huwekwa kisheria, jambo ambalo hupelekea utulivu wa nafsi na faraja ya mwili.
Muislamu lazima awe na nia ya kuhuisha ibada ya furaha katika sikukuu, hivyo atalipwa kwa michezo yake, pumbao lake, chakula chake na kinywaji chake.
Imamu na mlinganiaji wanatakiwa kukagua hali za watu, desturi zao, na shughuli zao, na waeleze ni nini kinaruhusiwa na kilichoharamishwa. Pengine watu wameizoea tabia ambayo ina msingi wa kuwakataza au kuwafanya wachukie bila ya watu kujua hilo, basi jambo likidhihirika kwa imamu, mlinganiaji na mwanachuoni basi wawafahamishe watu hukumu za Mwenyezi Mungu Mtukufu na hukumu za Mtume wake, amani iwe juu yake, na watu wanatii amri yake.
Kutafuta njia mbadala ni njia bora ya kuacha yale yaliyoharamishwa. Iwapo mwenye elimu anataka kuwaondolea watoto na wanafunzi wake baadhi ya tabia mbaya au matendo, basi ni lazima atafute mbadala mzuri kwao ambao wanafurahika nao, kama alivyofanya Mwenyezi Mungu Mtukufu alipowafidia Waislamu kwa sikukuu zao za Eid al-Fitr na Eid al-Adha.
Kuzuia visingizio ni mojawapo ya kanuni za Sharia. Ndio maana Mtume Rehema na Amani zimshukie akakataza kucheza sikukuu za washirikina. Kuogopa kwamba unaweza kuongezeka hadi kufikia hatua ya kushiriki katika matambiko na ibada. Kwa ajili hiyo, ni bora kwa mwanachuoni na msomi kuzingatia kanuni hii katika hukumu na fatwa zake. Pengine anaona nia ya kukataza jambo ambalo katazo hilo halihusiani nalo lenyewe, bali ni kwa yale yanayopelekea katika suala la uasi au ukafiri.
Mshairi alisema:Hii ndiyo sikukuu, basi nafsi zifurahie = na kwa kuwa hilo ni kheri, ndani yake mna bora ya waliyo yafanya.Siku zake ni majira ya kupanda wema = na kwa Mola wangu mtu huficha alichopanda Basi wawekeeni dhamana watu, yeyote atakaye fikwa na madhara na wakawa ni wafuasi wenu wanaokutegemea.Na waondoleeni ndugu wa karibu huzuni zao kutoka kwa = Mwenyezi Mungu amehitajia hivyo na mtume wake. Muwe vizuri na waja na muwe nao katoka majumba yao = mwezi kamili ambao giza la usiku liliona, likapungua.
Marejeo
- Tazama: “Al-Mafatih fi Sharh Al-Masabih” cha Al-Mazhari (2/342).
- Tazama: “"Aqtida' Alsirat Almustaqim Limukhalafat 'Ashab Aljahimi" cha Ibn Taymiyyah (1/488).
- Imepokewa na Al-Bukhari (949, 950), na Muslim (829).
Katika Hadithi, kuna ufafanuzi juu ya fadhila za swala ya jamaa na malipo yake makubwa yameelezwa. Kwa kuwa sala ya jamaa ni bora kuliko swala ya mtu peke yake kwa daraja ishirini na saba.
Kumekuwa na hadithi nyingine zinazopingana na idadi hii, kama kauli yake Mtume: “Swala ya mtu katika jamaa ni zaidi ya mara ishirini na tano kuliko sala yake anayoisali nyumbani kwake na sokoni; Na malipo hayo atayapata endapo atatawadha vizuri, kisha akatoka kwenda msikitini, hakuna kinachomtoa isipokuwa kwa ajili ya Swalah, kwa kila hatua anayotembea anapandishwa daraja, na anafutiwa dhambi, na anaposali Malaika hawaachi kumswalia maadamu yuko mahali pake pa kuswali, ewe Mwenyezi Mungu mbariki, ewe Mwenyezi Mungu mrehemu, na mmoja wenu anaendelea kuwa katika swala maadamu anangojea swalah. ." mutafaqun alayhi.[1]
Hakuna mgongano kati ya idadi hizo mbili. Kidogo hakipingani na kikubwa, na idadi hiyo ndogo inachukuliwa kuwa ilikuwa ni mwanzo wa uislamu, kisha Mwenyezi Mungu akafadhilisha kuongezeka kutoka ishirini na tano hadi ishirini na saba, au tofauti ya daraja mbili inatofautiana kulingana na ukamilifu wa sala, na kuhifadhi sura yake, heshima yake, idadi kubwa ya mkusanyiko wake, heshima ya sehemu, na kadhalika.[2]
Wanavyuoni wameangalia sababu za kuzidiana daraja baina ya swala za jamaa, na miongoni mwa sababu hizo ni zile zilizotajwa katika Hadithi iliyotangulia, ikiwa ni pamoja na: kumjibu muadhini kwa nia ya kuswali jamaa, na kuiendea mapema mwanzoni mwa wakati. Na kwenda msikitini kwa utulivu, kuingia msikitini kwa dua, na kusali tahiyatu al masjid, na kungojea jamaa, na Malaika kumswalia na kumwombea maghfirah, na ushahidi wao kwake, na mwitikio wa makazi, na usalama kutoka kwa Shetani anapokimbia kwenye makazi, na kusimama akingojea ihramu ya imamu au kuungana naye popote atakapomkuta, na kuipata takbira ya Ihram, na kunyoosha safu na kuziba mianya yake[3]
MAFUNDISHO:
Muislamu awe na bidii katika kuswali swala ya jamaa; Kwa Kuwa Ni bora kuliko sala ya mtu peke yake, na ina thawabu na wema ambao haupaswi kupuuzwa.
Muislamu awe na bidii ya kuswali kwa jamaa. Ili ajipatie palipo ambayo Mwenyezi Mungu amewaandalia wenye kusali jamaa; Mwenyezi Mungu amewaandalia makazi Peponi wale wanaokwenda msikitini. Kutoka kwa Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kutoka kwa Mtume, rehema na amani zimshukie, amesema: “Mwenye kwenda msikitini na kurudi, Mwenyezi Mungu amemuandalia makazi yake Peponi kila anapokwenda na kurudi kutoka msikitini[4]”
Anayetaka kufuta madhambi, na kufuta makosa, na kupanda daraja Peponi, basi na awe na bidii katika kuswali jamaa. Mtume rehma na Amani zimshukie amesema: “Je, nisikuambieni kitu ambacho kwacho Mwenyezi Mungu hufuta madhambi na kunyanyua daraja? Wakasema maswahaba: tuambie, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akasema: “Kutawadha vizuri wakati inapokuwa vigumu, na kwenda misikitini mara kwa mara, Na kungojea Swala baada ya Sala, hiyo ndiyo ribat[5]”
Mwenye furaha anayechukua fursa ya ujira wa kuhudhuria jamaa msikitini, kwani alichotayarisha Mwenyezi Mungu ni kwamba Swala ya jamaa itakupa ujira wa hijja; Akasema Mtume rehma na Amani zimshukie: “Mwenye kutoka nje ya nyumba yake akiwa ametaharika na kwenda kwenye swala ya faradhi, malipo yake ni sawa na malipo ya mwenye kuhiji katika Ihram. Na anayetoka kwenda kuitakasa Swala ya Dhuha, hakuna kilichomnyanyua isipokuwa hilo, basi malipo yake ni sawa na malipo ya mwenye kuhiji Umra. Na Swalah baada ya Sala, hapana upuuzi baina ya wawili hao katika kitabu cha Illiyyin[6]”
Sala ya jamaa inashuhudiwa na Malaika, hivyo hutaki kuwa miongoni mwa wale ambao Malaika wanawasifu na kuwatolea ushuhuda kwa kuwaombea dua mbele ya Mola wao Mlezi wa walimwengu wote? Amesema Mtume rehma na amani zimshukie: “Malaika Wanabadilishana kati yenu usiku na mchana, na wanakutana katika Sala ya Alfajiri na Alasiri. Kisha wale waliokesha pamoja nanyi usiku hupanda mbinguni, na Mola wenu Mlezi anawauliza naye ndio mjuzi zaidi: Vipi mmewaacha waja wangu? Wanasema Malaika: Tumewaacha wakiwa wanaswali, na tukawafikia wakiwa wanaswali[7]”
Ibn Masoud amesema: “Yeyote anayetaka kukutana na Mwenyezi Mungu akiwa Muislamu, basi na azishike Sala hizi kila anaposikia wito wake. Hakika Mwenyezi Mungu amemuwekea Mtume wenu Rehema na amani ziwe juu yake, Sunna za uongofu, na hizi swala ni katika Sunnah za uongofu. Na lau mngeswali majumbani mwenu kama anavyoswali huyu aliyechelewa nyumbani kwake, bila shaka mtakuwa mmeacha Sunnah. Na mtakapoacha Sunnah za Mtume wenu, mtakuwa wapotevu. Na mtu yeyote aliyejisafisha na kujitwaharisha vizuri, kisha akakusudia kwenda kwenye moja ya misikiti hii. Isipokuwa kwamba Mwenyezi Mungu humwandikia wema kwa kila hatua moja, na humnyanyua daraja kwa hatua hiyo, na kwayo humfutia madhambi. Na tulijiona kuwa ni mnafiki anayejulikana mwenye kuacha jamaa. Na alikuwa akiletwa mtu huku akichechemea baina ya watu wawili mpaka akawekwa katika safu[8]”
Amesema Abdullah bin Omar Al-Qawaririy Mwenyezi Mungu amrehemu: Sikuwahi kukosa kuswali swala ya ishaa nikiwa katika jamaa, akanijia mgeni siku moja nikawa nashughulika naye, nikatoka nje kwenda kusali katika makabila ya Basra Kwa hiyo watu walikuwa wameswali na kurudi majumbani mwao, hivyo nikajiambia: Imepokewa kutoka kwa Mtume rehma na amani zimshukie: “Swala ya jamaa inaizidi swala ya mtu pekee kwa daraja ishirini na tano.” Na Ikapokewa: “Ishirini na saba.” Basi nikarudi nyumbani, nikasali ishaa mara ishirini na saba, kisha nikapitiwa na usingizi na kujiona nikiwa na watu wamepanda farasi, na mimi nimepanda farasi kama farasi wao na tunafanya biashara, nikamgeukia mmoja wao na akanambia: Usimsumbue farasi wako; Huwezi kutufikia! Nikasema: Kwa nini hivyo? Akasema: hakika sisi Tuliswali Swalah ya ishaa kwa jamaa[9]”
Hadiyth inabainisha kuwa kuchelewesha swala kwa kutaraji kusubiri kwa jamaa ni bora kuliko kuitekeleza mwanzo wa wakati peke yake, isipokuwa muislamu akikhofia kuwa muda utakwisha, basi aswali peke yake.
Mshairi amesema:Kuinua wito wa sala juu ya minara = katika alfajiri ya asubuhi na usiku uliotulia Ni wito unaoleta uhai kwa ulimwengu = na wakazi wake, vijijini na mijini Na ni wito kutoka mbinguni kwenda duniani = nje na ndani Na ni mkutano baina ya Malaika na Imani = na Waumini bila ya kuomba idhini Na ni kuondoka kwenda kwenye kufaulu, kheri = haki, uwongofu, na mazuri.
Marejeo
- Imepokewa na Al-Bukhari (647) na Muslim (649).
- Dalil Alfalhin Lituruq Riyadh Al-Salihin” cha Ibn Allan Al-Siddiqi (6/548).
- Fath al-Bari cha Ibn Hajar (2/ 133, 134).
- Imepokewa na Al-Bukhari (662) na Muslim (669).
- Imepokewa na Muslim (251).
- Imepokewa na Ahmad (22304) na Abu Daawuud (558).
- Imepokewa na Al-Bukhari (555) na Muslim (632).
- Imepokewa na Muslim (654).
- “Al-Tabsrah” cha Ibn al-Jawzi (2/221).
Amesema Mtume Rehema na Amani zimshukie kuwa misikiti ni sehemu zinazopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu. Ni nyumba ya utiifu, msingi wa uchamungu, sehemu za kumtaja mola mlezi, vyanzo vya elimu, na mahali pa kupatikana wito wa Mwenyezi Mungu.
Ndio maana Mtume Rehema na Amani zimshukie alikuwa na shauku ya kuujenga msikiti alipofika Madina mara ya kwanza, na alikuwa akibeba mawe yeye mwenyewe, amani iwe juu yake, pamoja na maswahaba zake, Mungu awe radhi nao.
Msikiti ni jengo la kwanza katika kuunda dola ya Uislamu, na kutoka humo huenezwa daawah, na ndani yake hufunzwa hukumu na sheria za Kiislamu, na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kupitia msikiti aliweza kusimamia mambo ya dola, na ndani ya msikiti aliweza kujadiliana na Maswahaba mipango ya vita na uvamizi, kupokea misafara na wajumbe, wa makampuni ya kutekeleza, kuwasuluhisha wagomvi na kadhalika.
Wanaokwenda Misikitini ni watu wa Imani na khofu, ambao Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema juu yao:
“Katika Nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameamrisha zitukuzwe, na humo litajwe jina lake, wanamtakasa humo asubuhi na jioni (36) Watu ambao biashara wala kuuza hakuwashughulishi na kumdhukuru Mwenyezi Mungu, na kushika Sala, na kutoa Zaka. Wanaikhofu Siku ambayo nyoyo na macho yatageuka”
[An-Nur: 36-37].
Aliwataja kuwa na imani kwa kusema:
“Hakika wanao imarisha misikiti ya Mwenyezi Mungu ni wale wanao muamini Mwenyezi Mungu, na Siku ya Mwisho, na wakashika Sala, na wakatoa Zaka, na wala hawamchi ila Mwenyezi Mungu. Basi huenda hao wakawa katika waongofu”
[At-Tawbah: 18].
Kwa hiyo kujitolea katika kujenga nyumba za Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiko kujitolea kwa hali ya juu zaidi, Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake amesema: “Mwenye kujenga msikiti kwa kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu atamjengea mfano wake peponi[1]”
2. Na Mtume Rehema na Amani zimshukie ametuambia kuwa sehemu zinazochukiwa zaidi duniani ni masoko. Pale ambapo kuna utata, mazungumzo ya kipuuzi, ulaghai, udanganyifu, viapo vya uwongo, miamala ya riba, kuvunja ahadi, kupuuza kumkumbuka Mwenyezi Mungu, na kadhalika. Ndio maana Salman al-Farsi Mwenyezi Mungu awe radhi naye akasema kwamba masoko ni “vita vya Shetani; na huweka bendera yake masokoni[2]”
MAFUNDISHO:
Ameeleza Mtume kuwa misikiti ni sehemu zinazopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu, na hii inapelekea kuwa kufanya ibada ndani yake ni bora kuliko kufanya ibada sehemu nyengine; Kuswali msikitini ni bora kuliko kuswali nyumbani na sokoni, na mikusanyiko ya elimu msikitini ni bora kuliko sehemu nyingine yoyote, na kujitolea kujenga misikiti ni bora na kuna thawabu zaidi kuliko kutoa sadaka katika njia zingine.
Kukua kwa Uislamu na siri ya maendeleo yake ilikuwa katika kuitumia nafasi na umuhimu wa msikiti kimalezi, kiulinganiaji na kielimu. Ikiwa tunataka kurejea kwenye njia ya ustaarabu, ni lazima tuchunge malezi sahihi na kuitambua nafasi ya msikiti katika Nyanja hiyo.
Iwapo msikiti ni sehemu inayopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu Mtukufu, basi hapana shaka kuwa kukaa humo kwa nia ya ibada na kungojea Swala kuna malipo makubwa, na Muislamu hatakiwi kuukosa kiasi hicho cha malipo kwa namana awezavyo.
Mwenyezi Mungu, aliyetakasika, amefanya kwenda Misikitini kuwa miongoni mwa matendo makubwa yanayomkurubisha mja kwa Mola wake Mlezi, Aliyetukuka, Mtukufu. Hata Mtume, amani iwe juu yake, ameeleza katika wale saba ambao Mwenyezi Mungu atawatia chini ya kivuli chake siku ambayo hakutakuwa na kivuli isipokuwa chake: "Na mtu ambaye moyo wake umeshikamana na misikiti[3]"
Misikiti ni nyumba za Mwenyezi Mungu.imewekewa adabu ambazo Muislamu anatakiwa kuzizingatia; ikiwa ni pamoja na Kuvaa nguo nzuri, na kujipamba, na kujipaka manukato kwa yale aliyo nayo, na kuacha vyakula vyenye harufu mbaya, kama vile kitunguu saumu, na mengineyo, ambayo yanawaudhi Malaika na wana Adam.
Inapendeza kwa Muislamu kuanza kuingia kwake msikitini kwa dua zilizopokelewa katika hadith; Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake amesema: “Akiingia mmoja wenu msikitini, na aseme: Ewe Mola nifungulie milango ya rehema yako, na atakapotoka aseme: Ewe Mwenyezi Mungu, nakuomba kwa fadhila Zako.[4]”
Ni Sunnah kwa mwenye kuingia msikitini asikae mpaka aswali rakaa mbili za kusalimia msikiti; Amesema Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake: “Mmoja wenu anapoingia msikitini basi asikae mpaka asali rakaa mbili[5]”
Masoko ni sehemu mbaya zaidi kwa sababu ya madhambi, uchafu, mabishano na mambo mengine yaliyomo ndani yake, na sehemu yoyote inayofanana na hiyo katika matatizo basi itachukua hukumu hiyo. Ikiwa nyumba na mahali pa kazi ya mtu hupatikana viapo vya uwongo, uasherati, kutukana, na kadhalilika; Itakuwa ni moja ya sehemu mbaya sana mbele ya Mwenyezi Mungu.
Haipendezi kwa mtu kwenda sokoni bila ya haja, lakini akienda kwa ajili ya haja kama vile kununua na kuuza haichukiwi; Hakika Yeye Aliyetukuka anasema:
“Na hatukuwatuma kabla yako Mitume ila walikula na kwenda masokoni ’’
[Al-Fuqan: 20].
Mwenye kuchochewa na haja ya kwenda sokoni asiwe wa kwanza kuingia humo, wala asiwe wa mwisho kutoka humo; Kama Salman al-Farsi Mwenyezi Mungu awe radhi naye alivyosema: “Usiwe - ukiweza - wa kwanza kuingia sokoni, wala wa mwisho kutoka humo; Ni vita vya Shetani, na hunyanyua bendera yake[6]”
Mshairi alisema:Yeyote anayeshikamanisha moyo na msikiti na haMuabudu yeyote isipokuwa mkarimu, mwenye kuneemesha Basi huyo ndiye atakuwa chini ya kivuli cha Mwenyezi Mungu wakati ambao= Hakuna kivuli ila chakwake, Aliyetakasika milele Mwenye kuogopa madhambi huja akitetemeka = na hakimbilii popote ila msikitini nyumba imara.
Basi akamtukuza Mwenyezi Mungu, akaomba, kwa unyenyekevu = katika nyumba ambayo haabudiwi kwa haki isipokuwa yeye. Inapokuwa safi roho na nafsi yake, = basi hawezi kuwa na dhulma, wala husuda moyoni.Na ni waovu wangapi walikuwa wakija huku wamezama katika maasi = akarejea alibeba mbavuni mwongozo Na ni wajinga wangapi, wamegubikwa na giza la ujunga = ukawa mwezi kamili wenye nuru ya elimu iwakayo.
Marejeo
- Imepokewa na Al-Bukhari (439) na Muslim (533).
- Imepokewa na Muslim (2451).
- Imepokewa na Al-Bukhari (660) na Muslim (1031).
- Imepokewa na Muslim (713).
- Imepokewa na Al-Bukhari (444) na Muslim (714).
- Imepokewa na Muslim (2451).
Mtume Amani iwe juu yake anafahamisha ibada tatu, atakayezifanya ameijua imani, na kaipata, na akaweza kuifanya. Alitumia ladha Kwa jambo la kimaana lisiloonekana au lisiloonjwa kwa ajili ya msisitizo, na kufananisha chakula kitamu kilichokusanya utamu na kinachouvutia moyo.Qur’ani Tukufu ilitumia njia hii kwa kutumia neno “onja” kwa mateso, kama vile Mwenyezi Mungu alivyosema:
“Hakika wale walio zikataa Ishara zetu tutawaingiza Motoni. Kila zitapo wiva ngozi zao tutawabadilishia ngozi nyengine ili waionje hiyo adhabu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima”
[An-Nisa: 56].
Na Mtume amani iwe juu yake ameitaja katika kauli yake: “Mwenye kuridhika na Mwenyezi Mungu kuwa ni Mola wake, na Uislamu ndiyo dini yake, na Muhammad kuwa ni Mtume wake, ameonja ladha ya imani[1]”
Na ladha ya imani anayo ionja mja ni kuvumilia shida katika kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu, kuridhika na hukumu na hatima Yake, na kuitanguliza Akhera kuliko dunia, na kuufungua moyo wake juu ya hayo yote.
2. Sifa ya kwanza ni tauhidi ambayo ni ibada ya Mwenyezi Mungu peke yake, ambaye hana mshirika. Ibada inajumuisha yote ambayo Mwenyezi Mungu anayapenda na anapendezwa nayo, ikijumuisha maneno na matendo ya nje na ya ndani. Kama vile mapenzi, matumaini na khofu, dua na kutafuta msaada, kuchinja na kuweka nadhiri, na kujikurubisha kwa kila aina ya sunnat na vitendo vya utiifu, kwa hivyo asifanye chochote kati ya hayo kwa ajili ya mwingine asiyekuwa Mwenyezi Mungu.
Hii ndiyo sifa ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwatuma kwayo Mitume wote; Mwenyezi Mungu anasema:
“Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipo kuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu”
[Al-Anbiyaau: 25]
Kwa hiyo mwenye kuacha tauhidi yake amemuahidi kuishi milele katika moto na kuporomosha matendo ya yeyote yule. Mwenyezi Mungu akamwambia Mtume wake rehema na amani ziwe juu yake:
“Na kwa yakini yamefunuliwa kwako na kwa walio kuwa kabla yako: Bila ya shaka ukimshirikisha Mwenyezi Mungu a'mali zako zitaanguka, na lazima utakuwa miongoni mwa wenye hasara (65) Bali muabudu Mwenyezi Mungu tu, na uwe miongoni mwa wenye kushukuru”
[Al-Zumar: 65, 66].
3. Sifa ya pili katika hizo ni kuwa mja atoe zaka ya mali yake kwa utiifu na kwa hiari, akijitakasa kwa kufanya hivyo na ikamsaidia kuilipa kila mwaka.
Alitaja zakat tu. Kwa sababu pesa hupendwa na nafsi inafanya choyo. Nafsi ikifunguka kwa kupenda na kwa utiifu, hii ni dalili ya usahihi wa imani yake. Kwa kuwa wanafiki ni wale wanaotoa kwa kusitasita na kuchukia, Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema:
“Na hawakuzuiliwa kukubaliwa michango yao ila kwa kuwa walimkataa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, wala hawaji kwenye Sala ila kwa uvivu, wala hawatoi michango ila nao wamechukia”
[At-Tawbah: 54].
4. Sifa ya mwisho inahusiana na iliyotangulia, nayo ni kuwa mja akikusudia kutoa zaka yake, hataki kuharibu au kuharibu vilivyomo ndani yake ili aitoe. Ikiwa Zakat ni faradhi kwa mifugo yake, hachagui mzee, dhaifu, au mwenye magamba, au mgonjwa, ambaye haruhusiwi kuchinjwa na ulaji wake, wala mengine yanayolaumika kutoka kwao, kama vile vilema, kukonda, sana. Kuwa ndogo, na kadhalika.
Hii haimaanishi kuwa Mwislamu ikiwa na mifugo yake yote ni wagonjwa haimtoshi kutoa hata mmoja wao, bali kinachokusudiwa ni onyo kwa wale wanaochagua ubaya wa alichonacho kuwatolea zaka. , yakithibitisha maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:
“Enyi mlio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa”
[Al-Baqarah: 267].
Muumini wa kweli ambaye anapata utamu wa imani ndani ya nafsi yake anakubaliana na kauli ya Mwenyezi:
“Kabisa Hamtafikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyo vipenda. Na kitu chochote mnacho kitoa basi hakika Mwenyezi Mungu anakijua”
[Al Imran: 92].
5. Kisha Mtume Rehema na Amani zimshukie akabainisha kuwa kinachotakiwa katika zaka ni kutoa Kati na kati ya mali, na ni wastani baina ya mipaka miwili. Hatoi kilicho bora zaidi wala kibaya zaidi katika mali aliyonayo, na Abu Bakr Al-Siddiq Mwenyezi Mungu awe radhi naye alimwandikia Anas bin Malik Mwenyezi Mungu awe radhi naye: “Wala asitowe mnyama aliyezeeka, au mwenye chongo, au mbuzi dume, isipokuwa akitaka mtoaji.[2]” yaani mtoa zaka. Alisema Mtume kumwambia Mu’adhi ibn Jabal Mwenyezi Mungu awe radhi naye Alipomtuma kwenda Yemen: “Na ogopa vilivyo bora katika mali za watu[3]” maana yake: jiepusheni navyo na usivichague.
MAFUNDISHO:
Mlinganiaji na Mlezi lazima atumie maneno na mbinu zinazovutia usikivu wa msikilizaji na kuibua usikilizaji na ufahamu mzuri wa kile kinachosemwa; Ambapo Mtume, Rehema na Amani zimshukie, alitumia sentensi ya jumla, ambapo alieleza kuhusu sifa tatu ambazo mwenye kuzitambua ana imani kamili, na hizo humtaka msikilizaji kusikiliza na kuzihesabu sifa hizo moja baada ya nyingine; bila kupoteza hata moja.
Sifa ya kwanza ni chimbuko la sifa zote zilizotajwa katika Hadithi hii na nyinginezo; Iwapo mtu ataipata tauhidi ya kweli, atakuwa na furaha na mwenye furaha katika kuabudu, na ana hakika kwamba kile ambacho Mwenyezi Mungu anacho ni bora na cha kudumu zaidi, hivyo uzito na matatizo katika Dhati ya Mwenyezi Mungu Mtukufu hupungua kwake.
Moja ya dalili za imani ambazo Muislamu anaweza kuzithibitisha katika nafsi yake ni kupenda kwake kutoa zaka na kutoa sadaka; Kwani pesa hupendwa na nafsi, hivyo mja akiitumia kwa utiifu, kwa kuridhika na kutarajia kupata thawabu, hiyo ni dalili ya ukamilifu wa imani yake.
Iweje Muumini atoe sadaka kitu kibaya na hali anajua kuwa kinaingia mikononi mwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kabla ya mikono ya masikini?
Wale waliotangulia, Mwenyezi Mungu awe radhi nao, walikuwa wanapenda kutoa katika bora ya walivyo kuwa navyo; Abu Talha Al-Ansari aliposikia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:
“Kabisa Hamtafikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyo vipenda. Na kitu chochote mnacho kitoa basi hakika Mwenyezi Mungu anakijua”
[Al Imran: 92]
, alitoa sadaka ya mali yake aipendayo sana. Na ni shamba lake la matunda liitwalo “Berha” ambalo Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiingia na kunywa maji yake[4] , na Al-Rabi` bin Khuthaim, Mwenyezi Mungu amrehemu, akipenda sukari. na alikuwa akiwapa watu sadaka; Kwa kuafikiana na kauli yake Allah Mtukufu:
“Kabisa Hamtafikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyo vipenda”
[Al Imran: 92][5]
Mshairi alisema:
Ewe mtoa sadaka kwa mali za Mwenyezi Mungu, basi mali haipungui unapoitumia katika njia za kheri,
Kiasi gani Mwenyezi Mungu amewazidishia mali wenye nazo = hakika ukarimu, kwa hukumu ya Mwenyezi Mungu, ni kupata ridhaa.
Ubahili hupelekea ugonjwa ambao hauna tiba = mali ya bahili itakuwa urithi kwa wanaoteseka.
Kutoa zaka ni furaha kwa wale walionyimwa = Wakarimu wapo ikiwa unawahitajia.
Marejeo
- Imepokewa na Muslim (34).
- Imepokewa na Al-Bukhari (1455).
- Imepokewa na Al-Bukhari (1458) na Muslim (19), kwa kutoka kwa Ibn Abbas, Mungu awe radhi nao.
- Imepokewa na Al-Bukhari (1461) na Muslim (998).
- Al-Zuhd cha Ahmad bin Hanbal (uk. 267).
Mtume, Rehema na Amani zimshukie, anafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu ni mwema na asiye na mapungufu na kasoro. Asili ya mema: usafi, na kusalimika kutokana na uchafu[1]
Kwa hiyo, Mwenyezi Mungu hakubali chochote isipokuwa matendo mema na nafsi safi. Mwenyezi Mungu hawi karibu na Mwenye roho mbaya anaye wachukia watu na vifundo, na mwenye kuwafanyia watu mambo machafu, na mwili wake ukanawirishwa kwa kula vitu vilivyoharamishwa, hatakuwa karibu na Mwenyezi Mungu.
Kadhalika Mwenyezi Mungu hakubali matendo isipokuwa yaliyo mema, wala hakubali kitendo kilichoingiwa na ushirikina na unafiki, na wala hakubali sadaka katika mali iliyochukuliwa kwa haramu. Mtume Amani iwe juu yake amesema: “Hakuna atoaye sadaka iliyo bora – na Mwenyezi Mungu hakubali kisicho bora -isipokuwa Mwingi wa Rehema huishika kwa mkono Wake wa kulia, hata ikiwa ni tende, basi hukua katika mkono wa Mwenyezi Mungu mpaka ikawa kubwa kuliko mlima, kama mmoja wenu anavyomlea na kumkuza mtoto wa farasi au kinda la ngamia wake.[2]” - na Faluw: Ni mtoto wa kiume wa farasi, na Fasil: ni mtoto wa kike wa ngamia - na akasema: "Haikubaliwi Swala bila ya kutakasika, na haikubaliwi sadaka kutoka katika mali ya wizi [3] .
Na imejumuishwa katika ubaya kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu hakubali kwamba mtu atumie kwa makusudi mali yake mbaya zaidi ili aiondoe katika zaka ya pesa yake. Amesema Mwenyezi Mungu:
“Enyi mlio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma, na katika vile tulivyo kutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyewe msinge vipokea ila ingekuwa mmefumba macho. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha na Msifiwa”
[Al-Baqarah: 267].
2. Kisha Mtume Rehema na Amani zimshukie akabainisha kuwa hakuna tofauti katika kula chakula kizuri, kinywaji na mavazi baina ya Mitume na manabii na wafuasi wao; Kama vile Mwenyezi Mungu Mtukufu alivyowaamrisha watu wote kula vitu vizuri na kutenda mema, ndivyo alivyowaamrisha Mitume wake, vivyo hivyo kila mtu ameamrishwa kutafuta halali na kuacha haramu.
3. Kisha akamjulisha Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake kuwa kula haramu ni sababu ya kutojibiwa dua pamoja na kuwepo sababu zake. Mtu anaweza kusafiri safari ya utii; Hajj, jihadi, daawa, au mfano wa hayo, athari za safari na dhiki humdhihirikia, nywele zake zimetimka na zilizochafuka, na juu ya uso wake na nguo zake kuna athari za vumbi, anainua mikono yake mbinguni. kuomba kwa haraka kwa Mwenyezi Mungu ili amjibu, lakini muda wote yuko katika haramu; Kula kwake, kunywa, mavazi na chakula vyote ni haramu. Atajibiwa vipi mtu kama huyu?!
4. Na kusema kwake: “Atajibiwa vipi” ni kuuliza kwa mshangao na kuonyesha umbali wa kujibiwa, na hauko wazi katika kutowezekana kujibu na kuzuia kabisa; Inajuzu kwa Mwenyezi Mungu kuitikia dua kwa ukarimu utokao Kwake, na anaweza kumjibia maombi kama kumpa muda na kukata hoja yake mbele ya Mwenyezi Mungu. Tunajifunza katika hadithi hii kwamba kujikita katika haramu na kujihudumia kwa vitu vya haramu ni miongoni mwa vikwazo vya kuzuia dua isijibiwe[4]
MAFUNDISHO:
Muumini ni mwema; Moyo, ulimi, na mwili wake, na hayo ni kwa imani iliyomo moyoni mwake, na yanadhihirika kwenye ulimi wake kutokana na Kumtaja Mola mlezi, na kwenye viungo vyake kwa matendo mema, ambayo ni matunda ya imani, na yanajumuishwa katika jina hilo, kwa hivyo mambo haya mema yote yanakubaliwa na Mwenyezi Mungu [5], Muislamu lazima aongezeke katika imani awe bora na nadhifu.
Mwenyezi Mungu Mtukufu anapenda kumuona mja wake akimwiga katika baadhi ya sifa zake ambazo si makhsusi Kwake; kama vile huruma, wema, msamaha, na mengineyo; Anapenda kuona mja wake akimwiga yeye katika huruma, wema na msamaha wake, na pia anapenda mja wake awe mwema na asiye na mapungufu na maovu.
Mja anapaswa kuchunguza ubora wa chakula chake, nafsi yake, na kazi yake; Ili kwamba Mwenyezi Mungu ampende na ayakubali matendo yake; Wahb ibn al-Ward, Mwenyezi Mungu amrehemu, amesema: “Ukishika nafasi ya nguzo hii [yaani msikitini], hakuna kitakachokufaa mpaka uchunguze kinachoingia tumboni mwako je nihalali au haramu[6]”.
Iwapo mwalimu na mlezi anamtaka mwanafunzi wake afanye jambo fulani, basi ni lazima amwekee mfano katika hilo, kama anavyomuamuru kujichanganya na watu, basi awe wa kwanza kuhudhuria. na ikiwa atamhimiza kujitolea ibada za sunna, ni wajibu kwa mwanafunzi wake kumuona hivyo. Ndio maana yeye, amani iwe juu yake, alituambia kuwa Mitume wameamrishwa kutafuta halali na kuacha haramu, shughuli zao ni sawa na za waumini wote, hakuna tofauti baina yao.
katika Hadith inayoinua hadhi ya Muumini; Pale ambapo Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwaelekezea yale Aliyowaamuru Mitume, wanastahiki hilo kwa sababu ya imani yao na kunyanyuliwa kwa daraja lao [7]
Mtume amani iwe juu yake alieleza kuwa safari ni moja ya sababu ya kujibiwa dua; kwakuwa anahofia kuwa roho inachoka kwa sababu ya upweke wa muda mrefu na nyumbani, kuchoka, na kuchoka ni moja ya sababu kuu za kujibiwa dua[8], Mtume amani iwe juu yake amesema: “Dua tatu zitajibiwa bila shaka: dua ya mzazi, dua ya msafiri, na dua ya aliyedhulumiwa”[9]. Muislamu akiwa safarini basi aombe sana. Kwani ni karibu zaidi kujibiwa.
Moja ya sababu ya kujibiwa dua ni kunyanyua mikono juu na kuomba kwa unyenyekevu; Amesema Mtume amani iwe juu yake: “Mola wenu Mlezi, Amebarikiwa na Ametukuka, yu Hai, Mkarimu, na Anamuonea haya mja Wake, akiinyoosha mikono yake Kwake halafu kuirudisha bure.[10] Muislamu anyooshe mkono wake kwa kuomba dua katika sehemu ambazo Mtume, Rehema na amani ziwe juu yake, alinyanyua mkono wake.
Kuomba dua mara kwa mara katika jambo ni sababu mojawapo ya kujibiwa dua, Muislamu hafanyi haraka katika dua yake, akawa anaomba dua mara moja kisha anaacha dua, bali aombe sana na kumsisitiza Mola wake Mlezi. “Mwingi wa Rehema.” Mtume Amani iwe juu yake amesema: “Mmoja wenu atajibiwa maadamu hana haraka; akasema: Niliomba na sikujibiwa.” Mutafakun alayhi[11]
Kula halali ni miongoni mwa sababu kubwa za kuitikiwa dua, na kula katika haramu ni kizuizi katika hilo. Kwa ajili hiyo, Wahb bin Munabbih, Mwenyezi Mungu amrehemu, amesema: “Mwenye kutaka Mwenyezi Mungu aitikie dua yake, basi ale chakula cha halali.” Yusuf bin Asbat, Mwenyezi Mungu amrehemu, akasema: “ Wamejulishwa kwamba dua ya mja huzuiliwa kutoka mbinguni kwa sababu ya chakula cha haramu.[12]”
Iwapo mtu anasafiri katika kitendo cha utiifu, na amejitolea, na asiitikiwe kwa sababu tu chakula chake kimeharamishwa, basi vipi kuhusu mtu ambaye anashughulishwa na dunia au katika malalamiko ya watu, au wasiojua aina za ibada na wema?![13]
Wale waliotangulia, Mwenyezi Mungu awawie radhi, walikuwa wakipenda kula chakula kizuri cha halali, na kujiepusha na kile kinachoshakiwa juu ya kuruhusiwa na kuharamishwa kwake. Kutoka kwa Mama wa Waumini Aisha, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, amesema: “Abu Bakr alikuwa na kijana ambaye alikuwa akimpa fungu fulani [yaani: alimpa kila siku kile alichojiwekea na kukiahidi juu yake. Na Abu Bakr akala kutoka kwenye fungu lake, siku moja akaleta kitu na Abu Bakr akala, basi yule kijana akamwambia: Je unajuwa hiki kimetoka wapi!?Akasema Abu Bakr: kwani ni nini? Akasema kijana: Nilimpigia ramli mtu katika zama za kabla ya Uislamu, na kiukweli nilimdanganya tu, akakutana nami na akanipa haki yangu, hiki ndicho ulichokula, basi Abu Bakr akaweka mkono wake mdomoni mwake, na akatapika kila kitu tumboni mwake.[14]”
Mshairi alisema:
Tunamuomba Mwenyezi Mungu katika kila dhiki, kisha tunamsahau inapodhihirika dhiki.
Je, tunawezaje kutumainia jibu la maombi = wakati tumeifunga njia yake kwa dhambi?!
Marejeo
- Tazama: "'Iikmal Almuealim Bifawayid Muslimin" cha Al-Qadi Iyad (3/535), “Al-Maysir fi Sharh Misbah al-Sunnah” cha Al-Turbishti (2/655).
- Imepokewa na Al-Bukhari (1410) na Muslim (1014).
- Imepokewa na Muslim (224).
- Tazama: "Almifham Lamaa 'Ashakil Min Talkhis Kitab Muslimin"Cha Al-Qurtubi (3/60), “Jami’ Al-Uloom na Al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/275).
- “Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/260).
- “Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/263).
- Tazama: “Sharh Arobaini al-Nawawi” cha al-Uthaymiyn (uk.: 142).
- “Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/269).
- Imepokewa na Abu Dawood (1536), Al-Tirmidhiy (1905), na Ibn Majah (3862).
- Imepokewa na Abu Daawuud (1488), Al-Tirmidhiy (3556), na Ibn Majah (3865).
- Imepokewa na Al-Bukhari (6340) na Muslim (2735).
- “Jami’ al-Ulum wa al-Hakam” cha Ibn Rajab (1/275).
- " Sharh Arobaini Al-Nawawi" cha Ibn Daqiq Al-Eid (uk. 41, 42).
- Imepokewa na Al-Bukhari (3842).