Kutoka kwa Ibn Umar – Mwenyezi Mungu awe radhi nao wote wawili – amesema: 1. “Mtume wa Mwenyezi Mungu amani iwe juu yake amefaradhisha zakatul-Fitri. 2. Pishi ya tende, au pishi ya Dengu, 3. Juu ya Muislamu mtumwa na aliyehuru, mwanamume na mwanamke, mdogo na mkubwa. 4. Na akaamrisha itolewe kabla ya watu kutoka kwenda kuswali.

Kutoka kwa Abu Hurairah, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani zimshukie amesema: Amesema Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka: “Kila kitendo cha mwana wa Adamu ni chake isipokuwa kufunga. Funga ni yangu na nitailipa, Kufunga ni ngao. Na ikiwa ni siku ambayo mmoja wenu amefunga, basi asifanye uchafu au kupiga kelele, na mtu akimtukana au akimpiga, basi na aseme: Mimi ni nimefunga. Naapa kwa Yule ambaye nafsi ya Muhammad imo Mikononi Mwake, harufu inayotokatoka kinywani mwa mfungaji ni bora mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko harufu ya miski. Mfungaji ana furaha mbili: anapofuturu hufurahi, na atapokutana na Mola wake Mlezi hufurahia saumu yake.”

Kutoka kwa Abu Huraira Mwenyezi Mungu awe radhi naye amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na Amani zimfikie: 1. “Mwenye kufunga Ramadhani kwa imani na kwa kutaraji malipo, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia. 2. Mwenye kuswali usiku wa cheo kwa imani na kwa kutaraji malipo, basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia”  Kutoka kwa Abu Huraira Mwenyezi Mungu awe radhi naye amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na Amani zimfikie: 3. “Mwenye kuswali usiku wa cheo kwa imani na kwa kutaraji malipo, basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia”

Kutoka kwa Abu Huraira Mwenyezi Mungu awe radhi naye amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie: “Yeyote asiyeacha maneno ya uwongo na kuyafanyia kazi na ujinga, basi Mwenyezi Mungu hana haja naye kwa kuacha chakula na kinywaji chake.”

Kutoka kwa Abu Hurairah Mwenyezi Mungu awe radhi naye amesema: Amesema Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake: “Mwenye kuhiji kwenye Nyumba hii na wala asifanye uchafu au uovu, atarejea kama siku ile alipozaliwa na mama yake.” 

Kutoka kwa Abu Hurairah Mwenyezi Mungu awe radhi naye ambaye amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu Amani iwe juu yake alituhutubia na kusema: “Enyi watu, Mwenyezi Mungu amekufaradhisheni Hija; nendeni mkahiji, Akasema mtu mmoja : Je ni kila mwaka ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Alinyamaza hadi akasema mara tatu. Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na Amani zimshukie: “Lau ningesema: Ndio, ingeli kuwa ni wajibu, na msingeliweza. Kisha akasema: Niachieni katika yale ambayo sikukuambieni. Waliangamia walio kuwa kabla yenu kwa sababu ya wingi wa maswali  na kutofautiana kwao na Manabii wao .. Basi nikikuamrisheni kufanya jambo, basi lifanyeni kadiri muwezavyo, na nikikukatazeni, basi liacheni.” 

Kutoka Kwa Jaber radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie amesema: Nilimuona Mtume Rehema na Amani zimshukie, akitupa mawe akiwa juu ya kipandwa Siku ya kuchinja. Huku Akisema: “Ili mpate kujifunza taratibu zenu; Sijui huenda sitahiji baada ya Hija hii.” 

Kutoka kwa Ubayd Allah bin Muhsin al-Khatmi, kutoka kwa Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam amesema: “Mwenye kuamka asubuhi akiwa na Amani, mwenye afya njema katika mwili wake, ana chakula cha siku yake, hivyo ni kana kwamba amemilikishwa dunia.”

Kutoka Kwa Umar, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kutoka kwa Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, amesema:1.“Lau mngemtegemea Mwenyezi Mungu kwa haki ya kumtegemea, mngelipewa riziki zenu kwa urahisi kama vile ndege wanavyo pewa riziki zao.  2. Wanatoka asubuhi wakiwa na njaa, na wanarudi jioni wakiwa wameshiba” 

Kutoka kwa Jabir bin Abdullah, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwamba alimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie akisema, katika mwaka wa Ushindi, alipokuwa Makka: “Mwenyezi Mungu na Mtume wake wamekataza uuzaji wa pombe. mizoga, Na nguruwe, Masanamu, Ikasemwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, je unayaonaje mafuta ya mzoga? Kwani mafuta hayo hupakwa meli, ngozi, na watu wanayatumia kama mafuta ya taa? Akasema: Hapana, ni haramu. Kisha akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu wakati huo: “Mwenyezi Mungu amewalaani Mayahudi; Hakika Mwenyezi Mungu alipokataza mafuta yake, waliyayeyusha, kisha wakaiuza, na wakala thamani yake. 

Kutoka kwa Abu Hurairah Mwenyezi Mungu awe radhi naye, 1- Mtume rehma na amani zimshukie alipita karibu na chombo cha chakula, akaweka mkono wake ndani yake, na vidole vyake vikalowa. 2- Akasema Mtume: “Ni nini hiki ewe mwenye chakula? Akasema: kimenyeshewa na Mvua ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. 3- Akasema Mtume: Kwa nini hukukiweka juu ya chakula ili watu wapate kukiona? 4- Adanganyaye si katika mimi”. 

Kutoka kwa Jabir bin Abdullah – Mwenyezi Mungu awawie radhi wote wawili – amesema: 1-    “Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam, amemlaani 2. mwenye kula riba, mwenye kuilipa, 3. Na Wakala wa riba. 4. Na mwenye kuiandika 5. Na mashahidi wenye kushuhudia riba.” 6. Na akasema Mtume: “Wote wako sawasawa” . Imepokewa na Muslim (1598).

Kutoka kwa Abu Hurayrah, ambaye amesema: 1- “Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake, amekataza kuuza kwa kutupa kokoto.  2. Na kuuza kwa udanganyifu”

Kutoka kwa Abdullah bin Masoud, radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie amesema: Tulikuwa pamoja na Mtume, ilihali tukiwa vijana, hatuna chochote, basi Mtume wa Mwenyezi Mungu Swalla Allaahu alayhi wa sallam akatuambia: 1- “Enyi kijana, anayeweza kusimamia majukumu ya ndoa basi na aoe. Ndoa Inapunguza macho na kuimarisha uke.   2- Iwapo mtu hawezi kufanya hivyo ni lazima afunge. Hakika kufunga ni kinga.

Kutoka kwa Abu Hurayrah, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani zimshukie: “Mwanamke anaolewa kwa sifa nne, kwa pesa yake, kwa nasaba yake, kwa uzuri wake, na kwa dini yake, Basi tafuteni mwanamke aliyeshika dini, mikono yako itakuwa imepatia kuchagua!”

Kutoka kwa Aisha, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, mke wa Mtume, rehma na amani zimshukie: 1-    Kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu Swalla Allaahu alayhi wa sallam alikuwa kwa Aisha, na Aisha akasikia sauti ya mtu akibisha hodi katika nyumba ya Hafsa, : Akasema: Huyu mtu anabisha hodi nyumbani kwako, basi Mtume rehma na amani zimshukie akasema: “Ninamuona ni mtu Fulani ” kwa ami yake Hafsa kwa kunyonya sehemu moja. 2. Aisha akasema: unasemaje lau fulani angekuwa hai - ami yake kwa kunyonya – akaja nyumbani kwangu? Naye akasema: Ndiyo. Kunyonyesha kunayaharamisha yote yaliyoharamishwa kutokana na nasaba na kuzaa”

Kutoka kwa Jabir bin Abdullah, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie. 1-   “Iblisi anaweka kiti chake cha enzi juu ya maji, kisha akawatuma watu wake, nao wana daraja kubwa kuliko wao. Mmoja wao anakuja kwa Iblisi na kusema: Nilifanya hivi na hivi, na Iblisi anasema: Hujafanya lolote.  2.  Akasema: Kisha anakuja mmoja wao na kusema: Sikumuacha mpaka nilipomtenganisha yeye na mkewe. Iblisi Anasema: Atamweka karibu zaidi na kumwambia: Wewe Ndio wewe ndio

Kutoka kwa Abdullah bin Omar, Mwenyezi Mungu awawie radhi: 1. Alimtaliki mkewe akiwa katika hedhi, Kwenye wakati wa Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam kwa talaka moja, 2. Omar Ibn Al-Khattab akamuuliza Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam kuhusu hilo, 3. Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam, akakasirika. 4. kisha Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam akasema: “Mwambie amrudishe, kisha abakie nae mpaka atoharike, kisha apate hedhi, kisha atoharike, 5. kisha akitaka ataishi naye baada ya hapo, na akipenda atamwacha kabla ya kumgusa (kumwingia). 6. huo ndio utaratibu ambao Mwenyezi Mungu ameamrisha kuachwa kwao wanawake.” Wameafikiana bukhari na muslim. Imepokewa, katika riwaya ya Muslim: Ibn Umar amesema: alisoma Mtume Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam aya hii : “Ewe Mtume, ikiwa utawataliki wanawake, basi wataliki kabla ya ada yao" . 7. Na katika mapokezi ya Imamu Muslim (kwamba Mtume alisema) " Muamrishe amrudishe, kisha ampe talaka akiwa msafi au mjamzito"

Kutoka kwa Ummu Atiyah, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie, amesema: 1. “Mwanamke hakai matanga kwa kufa yoyote zaidi ya siku tatu, isipokuwa kwa kufiwa na mume atakaa miezi minne na masiku kumi.  2.Wala havai nguo iliyo tiwa rangirangi isipokuwa nguo pana ya moja kwa moja, na wala asipakae wanja, na wala asiguse manukato na marashi isipokuwa akiwa safi baada ya hedhi. Atumie kiasi kidogo cha marashi na manukato au kucha”

Kutoka kwa Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu awawie radhi wote wawili, kutoka kwa  Mtume, rehema na amani zimshukie, amesema: “gaweni mitathi kwa kufuata wajibu kwa wale wanaostahiki, na chochote kinachobakia ni haki ya mwanamume