121 - FADHILA ZA SURAT AL FALAQ NA SURAT AL NNAASI

عَنْ عُقبةَ بنِ عَامرٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ ﷺ : «أَلَمْ تَرَ آيَاتٍ أُنْزِلَتِ اللَّيْلَةَ لَمْ يُرَ مِثْلُهُنَّ قَطُّ: ﴿قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ﴾ [الفلق: 1]، و ﴿قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ﴾ [الناس: 1]»

Kutoka kwa Uqba Bin A`Amir (Radhi Za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) amesema: amesema Mtume (rehma na amani ziwe juu yake) Je haujajua ayah zilizotelemshwa usiku huu, (hakika) sijaona chochote mfano wake, Surat Al Falaq Na Surat Al Nnaasi.

Muhtasari wa Maana

Ameeleza Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) kwamba Surat Al Falaq na Surat Al Nnaasi hakuna chochote mfano wake, iwe kwenye vitabu vya Mwenyezi Mungu Mtukufu ambavyo ameviteremsha kwa Manabii wake, au katika yale watu wanayoyapupia kijikingia.

Miradi ya Hadithi