Mola wetu Mlezi, ametakasika, anaeleza juu ya utetezi wake kwa mawalii wake, na ukaribu wake kwa waja wake wema, na upendo wake kwao.
Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam anatueleza kuwa matendo yanayopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu Mtukufu na yaliyo karibu naye zaidi ni kuswali kwa wakati wake, kisha kuwaheshimu wazazi wawili, kisha kupigana jihadi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.
Mtume rehma na amani zimshukie anaeleza juu ya wema wa kuwasaidia watu katika mambo yao ya kidunia, na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu humsaidia mja kwa kumsaidia ndugu yake, kisha akataja fadhila ya kutafuta elimu, na kheri anazozipata mtafuta elimu kama vile amani na rehema, na Mwenyezi Mungu Mtukufu akamtaja kwa Aliye Juu. Kisha akaonyesha kwamba jambo la maana ni biashara, si ukoo.
Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, anataja baadhi ya milango ya kheri itakayotia uzito zaidi katika mizani ya mja siku ya Qiyaamah, na kwamba mafikio ya watu yamo mikononi mwao, hivyo baadhi yao huokoa nafsi zao na wengine huziangamiza.
Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam anataja makundi ya Waislamu ambao Mwenyezi Mungu atawatia kwenye kivuli chake Siku ya Kiyama, na watakuwa salama na joto la jua na uvundo wa Jahannam. Nao ni: Imamu muadilifu, kijana mtiifu kwa Allah, mwenye kushikamana na misikiti, mwenye kupendana kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, mwenye kuacha matamanio kwa ajili ya kumcha Mungu, mwenye kuficha sadaka yake, mwenye kulia katika upweke wake kwa kumcha Mungu.
Baadhi ya masahaba masikini walimlalamikia Mtume rehma na amani ziwe juu yake kwamba matajiri wamepata fadhila na vyeo vya juu kupitia sadaka zao, basi Mtume rehma na Amani zimshukie akawaambia wana kheri katika matendo yanayochukua nafasi ya ujira wa sadaka.
Matendo mema katika siku kumi za mwanzo za Dhul-Hijjah si sawa na amali njema katika siku nyingine zisizokuwa siku hizi kumi, isipokuwa mtu atatoka na pesa na maisha yake katika njia ya Mwenyezi Mungu na akauawa kishahidi.
Kuanzia na upande wa kulia ni Sunnah yenye heshima ya kinabii.
Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam alikuwa na shauku kubwa ya kuwafundisha Ummah wake dua ya istikhara, na kwamba nini wanapasswa kufanya ikiwa wamechanganyikiwa katika jambo fulani
Al-Nawwas, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, alimuuliza Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam juu ya wema na dhambi ni nini, akamwambia kuwa jambo linalo kusanya wema ni tabia njema, na dhambi ni kile unachokishuku, na hujatulizana kwayo, na unaogopa kwamba watu watajua kwamba unafanya hivyo
Katika Hadith, ipo ishara ya ukarimu wa Mwenyezi Mungu na huruma kwa waja Wake. Ambapo huwalipa kwa kutaka kufanya wema, hata wasipofanya, na kuwazidishia malipo ya utiifu kwao, vilevile huwalipa ikiwa watajiepusha na jambo baya wanalokusudia kulifanya. Wakifanya hivyo, huthibitisha kosa moja, bila ziada.
Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam anatahadharisha juu ya madhambi makubwa hatari kwa waja, ambayo ni: Shirki, uchawi, kuua pasina haki, riba, pesa ya mayatima, kukimbia vita, na kuwatukana wanawake walio safi
Al-Mughira, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, amesema kuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake alikuwa akisema utajo huu baada ya swala, na yale yaliyohifadhiwa kutoka kwake, rehema na amani ziwe juu yake; ni kuwa amekataza kuongea yasiyofaa, na kuuliza sana yasiyohitajika, na kufuja pesa katika madhambi na israfu katika mambo yanayoruhusiwa, kama vile alivyoharamisha uasi, mauaji ya watoto wa kike, na kuchukua kisichokua chako na kuzuia kile unachopaswa kutoa.
Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, anatuambia kuwa Mwenyezi Mungu, Utukufu ni wake, ameondosha kwa neema yake, yote yanayopita katika Nafsi zetu, miongoni mwa matamanio, matakwa, fikra na yanayojiri moyoni. Hatutawajibishwa kwa jambo ambalo hatukusema au kufanya kwa viungo vyetu.
Walinganiaji kwa Mwenyezi Mungu wana malipo makubwa zaidi miongoni mwa watu. Kwakuwa Wanapokea ujira wao kikamilifu na kama ujira wa wale waliowafuata kwenye wito wao. Watetezi wa ufisadi na upotofu ndio watu wabaya zaidi. Wanabeba mizigo yao na mizigo ya wale wanaowafuata.
Ikiwa mipaka na kuamrisha mema na kukataza maovu itawekwa sawa, basi watu wote wataokoka, na kama sivyo watu wote wataangamia, Muasi ataangamizwa kwa kuasi kwake, na aliyenyamaza akaacha kukemea maovu na kuamrisha mema, ataangamizwa kwa hilo.
Haifai kwa Muumini kuona uovu bila kuukemea. Akiweza kuubadilisha kwa mkono bila ya kupatikana majaribu wala madhara, atafanya, la sivyo atamkemea kwa ulimi wake na kumuusia mwenzake, la sivyo atakemea kwa moyo wake na kukasirika kwa ghadhabu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam anafahamisha kuwa Dini ya Uislamu itabakia mpaka kitakaposimama kiyama, uislamu utashikwa na wanaume miongoni mwa Waumini watakaosema kwa sauti na kuutetea, na wale wanaopinga au kupigana nao hawatawadhuru.
Kiyama Kikikaribia, njozi anazoziona Muislamu zitakuwa za kweli zaidi, na kadiri mtu anapokuwa msema kweli ndivyo Ndoto zake zinakuwa za kweli zaidi. Ndoto nzuri ni moja ya sifa za unabii, na kuna aina tatu za Ndoto; Habari njema kutoka kwa Mwenyezi Mungu, huzuni kutoka kwa Shetani, na mazungumzo ya kibinafsi. Mtu akiona kitu anachokichukia katika ndoto, basi na atie udhu na aswali kiasi anachotaka, na asimwambie yeyote kuhusu hilo, kwa sababu halimdhuru.
Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, alieleza kwamba sala, sadaka, na amali njema hufuta madhambi, na pia akasema kwamba mitihani humfuata mja. Akitumbukia humo moyo wake unakuwa mweusi kiasi kwamba hajui lililo jema na wala hatakemea mabaya, bali anakuwa mfuasi wa matamanio yake. Na akiepukana nayo, moyo wake unakuwa safi, na hakuna majaribu yatakayomdhuru.