عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنهما قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ«مَا مِنْ أَيَّامٍ الْعَمَلُ الصَّالِحُ فِيهَا أَحَبُّ إِلَى اللَّهِ مِنْ هَذِهِ الْأَيَّامِ» يَعْنِي أَيَّامَ الْعَشْرِ، قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ، وَلَا الْجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللَّهِ؟ قَالَ: «وَلَا الْجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللَّهِ، إِلَّا رَجُلٌ خَرَجَ بِنَفْسِهِ وَمَالِهِ، فَلَمْ يَرْجِعْ مِنْ ذَلِكَ بِشَيْءٍ».


Kutoka kwa Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu awe radhi nao, ambaye amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimfikie: 1- “Hakuna siku ambazo matendo mema hupendwa zaidi na Mwenyezi Mungu kuliko siku hizi,” yaani siku kumi. 2- Wakasema Maswahaba: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hata jihadi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu? 3- Akasema Mtume: “Hata jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, isipokuwa mtu atoke na nafsi yake na mali yake, wala kisirudi chochote


Ni Abuu Al-Abbasi, Abdallah Ibn Abbasi Ibn Abdul Al-Muttalib

Ni Abuu Al-Abbasi, Abdallah Ibn Abbasi Ibn Abdul Al-Muttalib, Al-Qurashiy, Al-Hashimiy, Al-Madaniy, alizaliwa kwenye shi’bi ya banii hashim kabla ya kuhama Mtume (s.a.w) kwenda madina kwa miaka mitatu, nayeye (r.a) ndio wino (yaani mwanazuoni mkubwa)  wa ummat Muhammad(s.a.w) na mkalimani wa qur’ani, na mtoto wa ammiyake Mtume (s.a.w), na alikuwa akiitwa bahari kwa wingi wa elimu aliyokuwa nayo, hakika Mtume alimwombea dua kwa kusema: “ Ewe Mwenyezi Mungu mpe ufahamu katika dini ” ([1]) na yeye ni katika maswahaba waliopokea hadithi kwa wingi sana, aliingia katika uislamu akiwa mdogo, na aliishi na Mtume (s.a.w), baada ya

Marejeo

1. Sahihi Al-Bukhari (143) nani tamko lake, na Sahihi Muslim (2477).

Miradi ya Hadithi