عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنهما، عَنْ رَسُولِ اللهِ فِيمَا يَرْوِي عَنْ رَبِّهِ تَبَارَكَ وَتَعَالَى، قَالَ: «إِنَّ اللهَ كَتَبَ الْحَسَنَاتِ وَالسَّيِّئَاتِ، ثُمَّ بَيَّنَ ذَلِكَ، فَمَنْ هَمَّ بِحَسَنَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا، كَتَبَهَا اللهُ عِنْدَهُ حَسَنَةً كَامِلَةً، وَإِنْ هَمَّ بِهَا فَعَمِلَهَا، كَتَبَهَا اللهُ عَزَّ وَجَلَّ عِنْدَهُ عَشْرَ حَسَنَاتٍ إِلَى سَبْعِمِائَةِ ضِعْفٍ إِلَى أَضْعَافٍ كَثِيرَةٍ، وَإِنْ هَمَّ بِسَيِّئَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا، كَتَبَهَا اللهُ عِنْدَهُ حَسَنَةً كَامِلَةً، وَإِنْ هَمَّ بِهَا فَعَمِلَهَا، كَتَبَهَا اللهُ سَيِّئَةً وَاحِدَةً».


Kutoka kwa Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu awawie radhi wote wawili, kutoka kwa Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam kuhusu yale aliyoyahadithia kutoka kwa Mola wake Mlezi, aliyebarikiwa na aliyetukuka amesema: 1- “Hakika Mwenyezi Mungu aliandika mema na mabaya, kisha akayabainisha. 2- Mwenye kukusudia kufanya jambo jema na asilifanye, Mwenyezi Mungu ataliandika kuwa ni wema kamili. 3- Na akikusudia kulifanya na akalitenda, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu humwandikia wema kumi, na humwongezea hadi kufikia mara mia saba, na zaidi ya hayo. 4- Ikiwa alikusudia jambo baya na akawa hakulitenda, basi Mwenyezi Mungu humwandikia jema kamili. 5- Na akikusudia kulifanya na akalitenda, Mwenyezi Mungu huliandika kuwa ni tendo moja baya.”

1- 1- Mtume, rehma na amani zimshukie, ameeleza kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu alikadiria mema na mabaya tokea awali, kwa mujibu wa ujuzi Wake, Utukufu ni Wake, kisha akawaeleza Malaika waandishi jinsi ya kuyaandika, au kwamba Mwenyezi Mungu mtukufu, Aliwaamrisha Malaika waandishi kuwaandikia waja wake mema na mabaya, kisha Akatuambia njia ya kuyahesabu na kuyaandika. 

2- 2- Iwapo mja akikusudia kufanya kitendo cha utiifu na akaazimia kukifanya, na asikifanye, basi kinahesabiwa kuwa ni amali njema kabisa. Kinachokusudiwa hapa ni dhamira na maazimio ya kutenda, si fikra tu ambayo inapita kichwani mwa mja na kutoweka bila nia ya kuifanya. Kwa kauli yake Mtume, rehema na amani ziwe juu yake: “Mwenye kukusudia kufanya jambo jema na asilifanye, basi Mwenyezi Mungu anajua kutoka kwake kwamba ameuhisi moyo wake na anauzingatia sana, huandikiwa amali njema.” [1]

3- 4- Na akifanya utiifu atalipwa kwa hayo mara nyingi. Kwa hiyo kheri ni mara kumi ya mfano wake, si chini ya hapo; Kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

“Mwenye kuleta jema atapata mara kumi zaidi yake”,

[Al-An’am: 160]

na huzidishiwa amtakaye Mwenyezi Mungu, basi hufikia hadi mara mia saba au zaidi; Amesema Mola mlezi Aliyetakasika!  

“Mfano wa wanao toa mali zao katika Njia ya Mwenyezi Mungu ni kama mafano wa mbegu iliyootesha mashoke saba katika kila shoke, kuna mbegu mia saba, na Mwenyezi Mungu Mtukufu humzidishia amtakaye, na yeye ni mwingi wa kutoa na mjuzi zaidi”.

[Al-Baqara: 261]

4- 5- Iwapo mja atanuia kutenda dhambi na akaazimia kufanya hivyo, kisha akamkumbuka Mola wake na akarejea Kwake na akajiepusha na dhambi hiyo, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu atamlipa kwa kujiepusha kwake kwa kuandika kuwa ni kheri kamili kwake. Mja analipwa hayo kwa sababu ya kupinga matamanio yake, na amemuasi shetani wake, na akakusudia kheri kwa kujiepusha na maovu, na ni kitendo cha moyo ambacho anastahiki kulipwa. Kauli yake, Mtume rehema na amani ziwe juu yake, inashuhudia: "Ni juu ya kila Muislamu kutoa sadaka." Wakasema Maswahaba: Asipofanya hivyo? Akasema Mtume: “Anapaswa kujiepusha na maovu nayo pia ni hisani” [2] Kwa hiyo, yeyote aliyekusudia kufanya dhambi lakini akaikosa, au akazuiwa kufanya hivyo, haingii katika maana ya Hadith na hastahiki malipo yaliyotajwa hapo juu. Kwani Mwenyezi Mtukufu alisema katika Hadithi Qudsi: “Aliiacha kwa hiari yangu” [3] yaani: kwa ajili yangu. 

5- 6- Mtu akitenda dhambi, Mwenyezi Mungu Mtukufu hulithibitisha kwake kuwa ni jambo moja ovu lisilozidishwa maradufu. Akasema, Mwenyezi mtukufu:

“Mwenye kutenda uovu hatalipwa ila mfano wake”

[Ghafir: 40]

. Lakini Mwenyezi Mungu anaikubali toba ya mwenye kutubia na kuifuta, na humsamehe amtakaye bila ya kutubia. Hata hivyo, matendo mabaya yanaweza kuongezeka kutokana na heshima ya mahali hapo. Kama asemavyo Mwenyezi Mungu:

“Hakika wale walio kufuru na wakazuilia Njia ya Mwenyezi Mungu na Msikiti Mtakatifu, ambao tumeufanya kwa ajili ya watu wote sawasawa, kwa wakaao humo na wageni. Na kila atakaye taka kufanya upotofu humo kwa dhulma, basi tutamwonjesha adhabu chungu”

[Al-Hajj: 25]

. Basi, Allah aliyetakasika, Amepanga adhabu chungu kwa wale waliokuwa na shauku ya kufanya dhambi. Kuongezeka kwa heshima ya wakati; Kama uasi katika miezi mitukufu, na pia huzidishwa na heshima ya mtendaji, kwani uasi kutoka kwa Mitume na mawalii ni dhambi zaidi kuliko wengine, kama Mwenyezi Mungu alivyosema:

“Na lau kuwa hatukukuweka imara ungeli karibia kuwaelekea kidogo (74) Hapo basi bila ya shaka tungelikuonjesha adhabu mardufu ya uhai, na adhabu mardufu ya kifo. Kisha usinge pata mtu wa kukunusuru nasi”

[Al-Isra: 74, 75]

, Na akasema Mola Mlezi:

“Enyi wake wa Nabii! Atakaye fanya uchafu dhaahiri miongoni mwenu, atazidishiwa adhabu mara mbili. Na hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi”

[Al-Ahzab: 30].

Mafunzo

1- Iwapo mja atatafakari jinsi Mwenyezi Mungu Mtukufu anavyowahisabu waja wake kwa vitendo vyao na akaona wema wake na rehema zake kwao, basi atazidisha mapenzi na kunyenyekea kwa Mola wake Mlezi, ametakasika na kutukuka. Bila ya fadhila na rehema zake, hakuna kiumbe chake hata kimoja ambacho kingeingia Peponi. 

2- Muislamu ni lazima aazimie kuwa mtiifu, hata kama haiwezekani kwake, kwani atalipwa kwayo hata asipoifanya. 

3- Muislamu anaweza kuvuna mema mengi bila ya uchovu au shida; Anachotakiwa kufanya ni kukusudia kufanya yale ambayo ni rahisi kwake kufanya. Akusudie kutoa sadaka ikiwa ana pesa, na akusudie kufanya jihadi ikiwezekana, na akusudie kuswali swala ya daraja la juu na kusoma Qur’ani. 

4- Akasema Mtume rehma na Amani zimshukie: Atakayelala na hali anatazamia kuswali usiku, akalala mpaka asubuhi kwa kuzidiwa na usingizi ataandikiwa malipo ya alichokusudia, na usingizi wake unakuwa ni sadaka kwake kutoka kwa Mola wake Mlezi, Mwenye nguvu na Mtukufu” [4]

5- Harakisha kufanya ibada na kujikurubisha kwa mwenyezi Mungu; Mwenyezi Mungu, Utukufu ni wake, hulipa jambo jema mara nyingi. 

6- Tazama jinsi Mwenyezi Mungu Mtukufu alivyowatayarisha waja wake kutii, kisha akawalipa kwa hilo malipo makubwa zaidi? Ametakasika kutoka kwa Mola Mlezi mwenye rehema na huruma anayejikurubisha kwa waja wake kwa baraka, na anapenda wajikurubishe Kwake kwa utiifu, na anawazidishia malipo makubwa kwa hayo. 

7- Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwafanya Malaika wa kuandika matendo, waone anachokusudia na anachofikiri mja, Je, hili halitupatii aibu kujua kwamba, Mmoja Wetu anakuwa na shauku ya kumuhofia shauku ya kumuasi Mungu Mwenyezi?!

8- Usidhani ya kuwa yatalipwa matendo ya uasi yaliyozuiliwa baina yenu na yeye. Bali hamtalipwa isipokuwa mkijiepusha kwa hiari, kutubu na kutubu. 

9- Kamwe usibebe kosa la dhambi usilolifanya; Kwa hiyo mwenye kudhamiria kufanya jambo la dhambi, na akakosa nafasi ya kulitenda, ataadhibiwa kana kwamba alilifanya. Mtume Amani iwe juu yake amesema: “Ikiwa Waislamu wawili watakutana na panga zao, basi muuaji na aliyeuawa wote wataingia Motoni.” Wakasema Maswahaba: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, muuaji huyu sawa , basi vipi kuhusu aliyeuawa? Alisema: "Alikuwa na hamu ya kumuua mwenziwe." [5]

10- Katika rehema ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kuwa ameyafanya maovu kuwa moja bila ya kuzidishwa, kama vile alivyofanya mema kuwa mengi. Mtu muasi asikate tamaa na rehema yake, wala mwenye kupita mipaka asikate tamaa na madhambi yake.

 11- Mshairi alisema: Na hakika Malaika wakarimu wanatulinda = na wamewakilishwa kwa watu wote Basi wanahesabu maneno yote ya mwana wa Adamu = na matendo yake kwa sehemu, na hakuna kitu kinachopuuzwa.

Marejeo

1. Imesimuliwa na Ahmed (19244).

2. Imepokewa na Al-Bukhari (1445) na Muslim (1008).

3. Imepokewa na Muslim (129).

4. Imepokewa na Al-Nasa’i (1787) na Ibn Majah (1344).

5. Imepokewa na Al-Bukhari (31) na Muslim (2888).



Miradi ya Hadithi