عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنهما، عَنْ رَسُولِ اللهِ فِيمَا يَرْوِي عَنْ رَبِّهِ تَبَارَكَ وَتَعَالَى، قَالَ: «إِنَّ اللهَ كَتَبَ الْحَسَنَاتِ وَالسَّيِّئَاتِ، ثُمَّ بَيَّنَ ذَلِكَ، فَمَنْ هَمَّ بِحَسَنَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا، كَتَبَهَا اللهُ عِنْدَهُ حَسَنَةً كَامِلَةً، وَإِنْ هَمَّ بِهَا فَعَمِلَهَا، كَتَبَهَا اللهُ عَزَّ وَجَلَّ عِنْدَهُ عَشْرَ حَسَنَاتٍ إِلَى سَبْعِمِائَةِ ضِعْفٍ إِلَى أَضْعَافٍ كَثِيرَةٍ، وَإِنْ هَمَّ بِسَيِّئَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا، كَتَبَهَا اللهُ عِنْدَهُ حَسَنَةً كَامِلَةً، وَإِنْ هَمَّ بِهَا فَعَمِلَهَا، كَتَبَهَا اللهُ سَيِّئَةً وَاحِدَةً».


Kutoka kwa Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu awawie radhi wote wawili, kutoka kwa Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam kuhusu yale aliyoyahadithia kutoka kwa Mola wake Mlezi, aliyebarikiwa na aliyetukuka amesema: 1- “Hakika Mwenyezi Mungu aliandika mema na mabaya, kisha akayabainisha. 2- Mwenye kukusudia kufanya jambo jema na asilifanye, Mwenyezi Mungu ataliandika kuwa ni wema kamili. 3- Na akikusudia kulifanya na akalitenda, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu humwandikia wema kumi, na humwongezea hadi kufikia mara mia saba, na zaidi ya hayo. 4- Ikiwa alikusudia jambo baya na akawa hakulitenda, basi Mwenyezi Mungu humwandikia jema kamili. 5- Na akikusudia kulifanya na akalitenda, Mwenyezi Mungu huliandika kuwa ni tendo moja baya.”

Ni Abuu Al-Abbasi, Abdallah Ibn Abbasi Ibn Abdul Al-Muttalib

Ni Abuu Al-Abbasi, Abdallah Ibn Abbasi Ibn Abdul Al-Muttalib, Al-Qurashiy, Al-Hashimiy, Al-Madaniy, alizaliwa kwenye shi’bi ya banii hashim kabla ya kuhama Mtume (s.a.w) kwenda madina kwa miaka mitatu, nayeye (r.a) ndio wino (yaani mwanazuoni mkubwa)  wa ummat Muhammad(s.a.w) na mkalimani wa qur’ani, na mtoto wa ammiyake Mtume (s.a.w), na alikuwa akiitwa bahari kwa wingi wa elimu aliyokuwa nayo, hakika Mtume alimwombea dua kwa kusema: “ Ewe Mwenyezi Mungu mpe ufahamu katika dini ” ([1]) na yeye ni katika maswahaba waliopokea hadithi kwa wingi sana, aliingia katika uislamu akiwa mdogo, na aliishi na Mtume (s.a.w), baada ya

Marejeo

1. Sahihi Al-Bukhari (143) nani tamko lake, na Sahihi Muslim (2477).

Miradi ya Hadithi