عن أنس رضي الله عنه قال: قَدِمَ رسولُ الله ﷺ المدينةَ ولهم يومانِ يَلعبون فيهما، فقال: «ما هذانِ اليومانِ؟!» قالوا: كنا نلعَب فيهما في الجاهلية، فقال رسول الله ﷺ: «إن الله قد أبدلَكم بهما خيرًا منهما؛ يومَ الأضحى، ويومَ الفِطر»

Kutoka kwa Anas amesema:

“Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie alikuja Madina na watu wa madina walikuwa na siku mbili za kucheza sikukuu, akasema Mtume: “Siku mbili hizi ni zipi?” Wakasema: Tulikuwa tukisherekea kabla ya Uislamu, basi Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani ziwe juu yake akasema: “Mwenyezi Mungu amewabadilishia kwa kilicho bora kuliko hizo siku mbili; Siku ya al-Adh-haa na siku ya al-Fitwr.”

Anas bin Malik bin Al-Nadr bin Damdam Al-Ansari

Anas bin Malik bin Al-Nadr bin Damdam Al-Ansari, Abu Hamza, imamu, mufti, msomaji, Mbobezi katika fani ya hadithi, msimuliaji wa Uislamu, Mtumishi wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, amani iwe juu yake, na wa mwisho kufa katika masahaba huko Basra. Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuja Madina akiwa na umri wa miaka kumi, na wakati Mtume anakufa Anasi alikuwa na umri wa miaka ishirini, na alikuwa akimtumikia Mtume, rehema na amani ziwe juu yake. Alishiriki vita pamoja na Mtume zaidi ya mara moja, na alimpa ahadi ya utii chini ya mti. Alipokea kutoka kwa Mtume elimu kubwa, Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake alimwombea dua ya mali nyingi na watoto, na shamba lake la mitende lilikuwa likipamba mara mbili kwa mwaka, alifariki mwaka: (93 AH) [1]


Marejeo

1.  Rejea ufafanuzi wake katika: “Sir Al-Alam Al-Nubala” cha Al-Dhahabi (4/417-423), “Ma`rifat Al-Sahaba” cha Abu Naim (1/231), “Kamusi ya Maswahaba. ” cha Al-Baghawi (1/43), “Asad Al-Ghaba” cha Ibn Al-Atheer (1/ 151-153).

Miradi ya Hadithi