عن عمَّارِ بنِ ياسرٍ رضي الله عنهما قال:بَعَثَنِي رَسُولُ اللهِ ﷺ فِي حَاجَةٍ فَأَجْنَبْتُ، فَلَمْ أَجِدِ الْمَاءَ، فَتَمَرَّغْتُ فِي الصَّعِيدِ كَمَا تَمَرَّغُ الدَّابَّةُ، ثُمَّ أَتَيْتُ النَّبِيَّ ﷺ، فَذَكَرْتُ ذَلِكَ لَهُ، فَقَالَ: «إِنَّمَا كَانَ يَكْفِيكَ أَنْ تَقُولَ بِيَدَيْكَ هَكَذَا»، ثُمَّ ضَرَبَ بِيَدَيْهِ الْأَرْضَ ضَرْبَةً وَاحِدَةً، ثُمَّ مَسَحَ الشِّمَالَ عَلَى الْيَمِينِ، وَظَاهِرَ كَفَّيْهِ، وَوَجْهَهُ

Kutoka kwa Ammar bin Yasir, Mungu amuwiye radhi, amesema:

1- Mtume wa Mwenyezi Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) alinituma katika jukumu fulani, nikapatwa na janaba, lakini sikupata maji, nikajibiringisha katika mchanga kama mnyama, kisha nikaenda kwa Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) nikamsimulia tukio hilo. 

2- Akasema: “hakika ilikuwa inatosha kufanya kwa mikono yako hivi” kisha akapiga ardhi kwa mikono yake mpigo mmoja, kisha akapangusa mkono wa kulia kwa mkono wa kushoto, na mkono wa kushoto kwa mkono wa kulia, na nje ya viganja vyake, na uso wake.

Ammar bin Yasir

Ammar bin Yasir, Mwenyezi Mungu amuwie radhi yeye na wazazi wake, alipatwa na janaba katika baadhi ya safari zake na hakuweza kupata maji, hivyo akajizungusha kwenye udongo mpaka ili aweze kuswali. Aliporejea kwa Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) akamueleza Mtume akambainishia asili ya tayammam, na kwamba ni pigo moja katika udongo ambalo anapangusa nalo mikono na uso.

Miradi ya Hadithi