عَنْ مَحْمُودِ بْنِ لَبِيدٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ «إنَّ أخْوَفَ ما أخافُ عليكم الشِّركُ الأصْغَرُ»، قالوا: وما الشِّركُ الأصْغَرُ يا رسولَ اللهِ؟ قال: «الرِّياءُ؛ يقولُ اللهُ - عزَّ وجلَّ - لهم يومَ القِيامةِ إذا جُزِيَ الناسُ بأعمالِهم: اذْهَبوا إلى الذين كنتُم تُراؤون في الدُّنيا، فانظُروا هل تَجِدون عِندَهُم جزاءً؟!»

Kutoka kwa Mahmood bin Labiid amesema:

amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na Amani ziwe juu yake): 1. “Hakika ninalo ogopea kwenu zaidi ni shirki ndogo” 2. Wakasema: shirki ndogo ni nini eh Mtume wa Mwenyezi Mungu? 3. Akasema: ni riya yaani kufanya kwa kujionesha 4. Mwenyezi Mungu Mtukufu atawambia siku ya kiyama baada ya watu kulipwa kwa matendo yao: 5. “Nendeni kwa mlio kuwa mnajionesha kwao, muone je watakulipeni?!”


Muhtasari wa Maana

Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) anatahadharisha kuhusu riya na kufanya ibada bila Ikhlaas, anaeleza kwamba hatima ya riya ni Mwenyezi Mungu kutomkubalia mja ibada, na wala hatamlipa siku ya kiyama, kwasababu amefanya ushirikina.

Miradi ya Hadithi