عن أبي سُليمانَ مالكِ بنِ الحُوَيْرثِ رضي الله عنه، قال:أَتَينا النبيَّﷺ ونحن شَبَبةٌ مُتقارِبون، فأقمْنا عنده عِشرين ليلةً، فظنَّ أنَّا اشتَقْنا أهْلَنا، وسألَنا عمَّن ترَكْنا في أهلنا، فأخبرناه، وكان رفيقًا رحيمًا، فقال: «ارْجِعوا إلى أهلِيكم،فعلِّموهم ومُروهم،وصلُّوا كما رأيتموني أُصلِّي،وإذا حضَرتِ الصلاةُ، فلْيُؤذِّنْ لكم أحدُكم، ثم لِيَؤُمَّكم أكبَرُكم»

Kutoka kwa Abu Sulaiman Malik bin Al-Huwairith, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, amesema:

1. Tulikuja kwa Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) tukiwa vijana tukikaribiana, tukakaa kwake siku ishirini, akadhani tumetamani familia zetu, akatuuliza kuhusu tuliowaacha katika familia zetu, tukamwambia. 2. na Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) Alikuwa ni mpole mwenye huruma, akasema: “Rudini kwa ahali zenu. 3. Wafundisheni na waelekezeni. 4. na swalini kama mlivyoniona nikiswali, 5. Na ukifika wakati wa Swala, mmoja wenu aadhini, kisha awaongoze mkubwa wenu”

Miradi ya Hadithi