عن أنس رضي الله عنه قال: قَدِمَ رسولُ الله ﷺ المدينةَ ولهم يومانِ يَلعبون فيهما، فقال: «ما هذانِ اليومانِ؟!» قالوا: كنا نلعَب فيهما في الجاهلية، فقال رسول الله ﷺ: «إن الله قد أبدلَكم بهما خيرًا منهما؛ يومَ الأضحى، ويومَ الفِطر»

Kutoka kwa Anas amesema:

“Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie alikuja Madina na watu wa madina walikuwa na siku mbili za kucheza sikukuu, akasema Mtume: “Siku mbili hizi ni zipi?” Wakasema: Tulikuwa tukisherekea kabla ya Uislamu, basi Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani ziwe juu yake akasema: “Mwenyezi Mungu amewabadilishia kwa kilicho bora kuliko hizo siku mbili; Siku ya al-Adh-haa na siku ya al-Fitwr.”

Vitendawili vya Qur'ani Vinavyohusiana

Mwenyezi Mungu mtukufu amesema:

“Na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongoeni ili mpate kushukuru”

[Al-Baqarah: 185].

Amesema Mwenyezi Mungu:

“Na mtajeni Mwenyezi Mungu katika zile siku zinazo hisabiwa. Lakini mwenye kufanya haraka katika siku mbili (akarejea) si dhambi juu yake; na mwenye kukawia pia si dhambi juu yake, kwa mwenye kumchamngu. Na mcheni Mwenyezi Mungu, na jueni kwamba nyinyi mtakusanywa kwake”

[Al-Baqarah: 203].

Akasema Mtukufu:

“Wala msibadilishe kibaya kwa kizuri”

[An-Nisa: 2].

Pia akasema aliyetukuka:

“Sema: Kwa fadhila ya Mwenyezi Mungu na rehema yake! Basi nawafurahi kwa hayo. Haya ni bora kuliko hayo wanayo yakusanya”

[Yunus: 58]

Miradi ya Hadithi