عن أنس رضي الله عنه قال: قَدِمَ رسولُ الله ﷺ المدينةَ ولهم يومانِ يَلعبون فيهما، فقال: «ما هذانِ اليومانِ؟!» قالوا: كنا نلعَب فيهما في الجاهلية، فقال رسول الله ﷺ: «إن الله قد أبدلَكم بهما خيرًا منهما؛ يومَ الأضحى، ويومَ الفِطر»

Kutoka kwa Anas amesema:

“Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie alikuja Madina na watu wa madina walikuwa na siku mbili za kucheza sikukuu, akasema Mtume: “Siku mbili hizi ni zipi?” Wakasema: Tulikuwa tukisherekea kabla ya Uislamu, basi Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani ziwe juu yake akasema: “Mwenyezi Mungu amewabadilishia kwa kilicho bora kuliko hizo siku mbili; Siku ya al-Adh-haa na siku ya al-Fitwr.”

Muhtasari wa Maana

Zamani watu wa Madiynah walikuwa wakisherehekea siku mbili za zama za kabla ya Uislamu, Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake alipohamia kwao na kuona sherehe zao, akawauliza kuhusu hilo, wakamwambia. kwa hivyo akawakataza kusherehekea, na akawaambia kwamba Mwenyezi Mungu amewafidia siku hizo mbili kwa iliyo bora zaidi. Eid al-Fitr na Eid al-Adh-haa.

Miradi ya Hadithi