عن عبدِ الله بنِ عمرٍورضي الله عنه عن النبيِّ ، قال:«أَرْبَعٌ مَنْ كُنَّ فِيهِ كَانَ مُنَافِقًا خَالِصًا، وَمَنْ كَانَتْ فِيهِ خَصْلَةٌ مِنْهُنَّ كَانَتْ فِيهِ خَصْلَةٌ مِنَ النِّفَاقِ حَتَّى يَدَعَهَا:إِذَا اؤْتُمِنَ خَانَ،وَإِذَا حَدَّثَ كَذَبَ، وَإِذَا عَاهَدَ غَدَرَ،وَإِذَا خَاصَمَ فَجَرَ» متفق عليه

Kutoka kwa Abdullah bun Amri, kutoka kwa Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake), amesema:

1.    “Mambo manne anaye kuwa nayo anakuwa ni mnafiki halisi, na anaye kuwa na moja wapo, anakuwa na sifa ya kinafiki mpaka ayaache; 2.Anapo aminiwa, anafanya hiyana 3.Anapo ongea hudanganya 4.Anapo ahidi, husaliti 5.Anapo kosana na mtu, anavuka mipaka.


Muhtasari wa Maana

Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) anataja sifa nne miongoni mwa sifa za wanafiki ambazo haifai kwa mwislam kusifika nazo. Atakae sifika nazo zote, atakuwa ni mnafiki kabisa, na atakae sifika na moja wapo atakuwa amesifika na sifa ya kinafiki, nazo ni; hiyana, uongo, usaliti, na kuvuka mipaka katika ugimvi.

Miradi ya Hadithi