عَنِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رضي الله عنه، عَنِ النَّبِيِّ قَالَ:  «مَثَلُ القَائِمِ عَلَى حُدُودِ اللَّه وَالوَاقِعِ فِيهَا، كَمَثَلِ قَوْمٍ اسْتَهَمُوا عَلَى سَفِينَةٍ؛ فَأَصَابَ بَعْضُهُمْ أَعْلاهَا، وَبَعْضُهُمْ أَسْفَلَهَا، فَكَانَ الَّذِينَ في أَسْفَلِهَا إِذَا اسْتَقَوْا مِنَ المَاءِ مَرُّوا عَلَى مَنْ فَوْقَهُمْ، فَقَالُوا: لَو أَنَّا خَرَقْنَا في نَصِيبِنَا خَرْقًا وَلَمْ نُؤْذِ مَنْ فَوْقَنَا، فَإِنْ يَتْرُكُوهُمْ وَمَا أَرَادُوا هَلَكُوا جَمِيعًا، وَإِنْ أَخَذُوا عَلى أَيْدِيهِمْ نَجَوْا، وَنَجَوْا جَمِيعًا»

Kutoka kwa Al-Nu’man bin Bashir Mwenyezi Mungu awe radhi naye, Kutoka kwa Mtume, rehma na Amani zimshukie, amesema:

“Mfano wa mwenye kuchunga mipaka ya Mwenyezi Mungu na akashikamana nayo ni kama watu waliosongamana katika meli. Baadhi yao wakawa sehemu yake ya juu, na baadhi sehemu yake ya chini, ikawa waliokuwa chini, wanapochota maji, wanapita kwa wale walioko juu yao. Na wakasema: Afadhali tungelitoboa katika sehemu yetu, ili tusiwaudhi walioko juu, Wakiwaacha na kufanya wanavyotaka, wote wataangamia, na wakizuiliwa mikononi mwao wataokoka wote kwa ujumla” 


Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam ametoa mfano wa kuonyesha umuhimu wa kulingania kwa Mwenyezi Mungu na kunasihiana, na kwamba lau si kukemea maovu watu wote wangeangamia. Inaashiria mwenye kutii ambaye anahifadhi mipaka ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na kutii amri na makatazo yake, na muasi ambaye anapuuza hukumu za Shari’a, ambaye hutumbukia katika matamanio na starehe zake, ni kama mfano wa Watu ambao walipanda melini kwenye maji safi, kwa hivyo wakapiga kura kuwa nani atakuwa juu ya meli na ni nani atakuwa chini yake, basi hilo lilifanyika na kila mtu akakaa mahali pake.


Basi wale walioko chini, walipohitajia kunywa au kuchota maji kwa ajili ya matumizi yao, wanapanda juu ya meli, wanachota maji, kisha wanashuka, wakapendekeza wavunje sehemu ya chini ya meli ambapo ndiyo sehemu yao, shimo ambalo watatumia kuchota maji, badala ya kupanda kwenda juu na kushuka chini, ili wapate kupumzika na wasiwadhuru jirani zao waliko juu. Ikiwa wamiliki wa sehemu ya juu watawaacha kufanya chochote wanachopenda, wakidai kwamba hii ni sehemu yao, ambayo wanaweza kufanya chochote wanachotaka, basi kila mtu ataangamia kwa kuzama majini. Kwakuwa sehemu iliyotoboka ndani ya meli itazamisha meli bila shaka, na lau wangewazuia kufanya hivyo, wote wangenusurika.


Ndivyo walivyo Waumini na makafiri; Ikiwa Waumini Wakiwaacha waasi na madhambi yao bila ya kuwakemea, basi kila mtu atastahiki adhabu ya Mwenyezi Mungu. Waasi kwa maasi yao, na wengine kwa kuwanyamazia na kutowakemea, kama alivyosema Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam: "Ikiwa watu wataona uovu na wasiubadilishe, basi ni kwamba Mwenyezi Mungu atawaadhibu kwa adhabu kutoka kwake" [1]  Na Mwenyezi Mungu aliwalaani Wana wa Israili walipoacha kuamrisha mema na kukataza maovu,

basi akasema, Mola aliyetakasika.

“Walilaaniwa walio kufuru miongoni mwa Wana wa Israili kwa ulimi wa Daud na wa Isa mwana wa Maryamu. Hayo ni kwa sababu waliasi na wakawa wanapindukia mipaka (78) Walikuwa hawakatazani maovu waliyo kuwa wakiyafanya. Hakika ni maovu yalioje mambo waliyo kuwa wakiyafanya” .

[Al-Maida: 78, 79]

Mafunzo

1-    Kutoa mifano ni njia mojawapo ya ufanisi ya kulingania kwa Mwenyezi Mungu mtukufu, na kufundisha elimu, na kisha Mwalimu na Mlezi anapaswa kuleta maana za busara karibu na akili za watu kwa kuwasilisha mifano inayoonekana ambayo iko karibu na ufahamu wao. [2]

2-  Muumini wa kweli haridhiki na kujirekebisha mwenyewe; Bali anabeba shida za umma unaomzunguka, na anafanya kazi ya kubainisha hatari zinazowatishia katika dini yao na ulimwengu wao.


3-    Kuacha kuamrisha mema na kukataza maovu ni sababu ya maangamizo, na kuangamizwa jamii kwa ujumla.

Kama Mwenyezi Mungu alivyosema:

“Na jikingeni na Fitna ambayo haitowasibu walio dhulumu peke yao kati yenu. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu” .

[Al-Anfal: 25]

4-    Kamwe usifikirie kuwa kujiepusha na dhambi kunatosha kuepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu. Badala yake, lazima ukemee maovu kadiri uwezavyo.


5-   Usikuzuie kukemea uovu kwa elimu yako kuwa huyo mkemewa hatakusikiliza. Unachotakiwa kufanya ni kushauri, na Mwenyezi Mungu humwongoa amtakaye.


6-   Haijuzu kwa Muislamu kuona jambo baya na hali ana uwezo wa kulibadilisha kisha akaliacha bila ya kulibadilisha,

na amesema Mwenyezi Mungu:

“Walilaaniwa walio kufuru miongoni mwa Wana wa Israili kwa ulimi wa Daud na wa Isa mwana wa Maryamu. Hayo ni kwa sababu waliasi na wakawa wanapindukia mipaka (78) Walikuwa hawakatazani maovu waliyo kuwa wakiyafanya. Hakika ni maovu yalioje mambo waliyo kuwa wakiyafanya”

[Al-Maida: 78, 79]. 


Marejeo

  1. Imepokewa na Ahmed (1), Ibn Majah (4005), Abu Dawood (4338), na Al-Tirmidhi (3057)
  2. .Tazama: “sherh ya Riyadh as-Salihin” cha Ibn Uthaymiyn (2/433).



Miradi ya Hadithi