عن حُمْرَانَ، مَوْلَى عُثْمَانَ، أَنَّ عُثْمَانَ بْنَ عَفَّانَ رضي الله عنه دَعَا بِوَضُوءٍ فَتَوَضَّأ،َ فَغَسَلَ كَفَّيْهِ ثَلَاثَ مَرَّاتٍ، ثُمَّ مَضْمَضَ وَاسْتَنْثَرَ، ثُمَّ غَسَلَ وَجْهَهُ ثَلَاثَ مَرَّاتٍ، ثُمَّ غَسَلَ يَدَهُ الْيُمْنَى إِلَى الْمِرْفَقِ ثَلَاثَ مَرَّاتٍ، ثُمَّ غَسَلَ يَدَهُ الْيُسْرَى مِثْلَ ذَلِكَ، ثُمَّ مَسَحَ رَأْسَهُ، ثُمَّ غَسَلَ رِجْلَهُ الْيُمْنَى إِلَى الْكَعْبَيْنِ ثَلَاثَ مَرَّاتٍ، ثُمَّ غَسَلَ الْيُسْرَى مِثْلَ ذَلِكَ،ثُمَّ قَالَ: رَأَيْتُ رَسُولَ اللهِ ﷺ تَوَضَّأَ نَحْوَ وُضُوئِي هَذَا،ثُمَّ قَالَ رَسُولُ اللهِ ﷺ: «مَنْ تَوَضَّأَ نَحْوَ وُضُوئِي هَذَا، ثُمَّ قَامَ فَرَكَعَ رَكْعَتَيْنِ لَا يُحَدِّثُ فِيهِمَا نَفْسَهُ، غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ»، وزاد مسلم في رواية: «وَكَانَتْ صَلاَتُهُ وَمَشْيُهُ إِلَى الْمَسْجِدِ نَافِلَةً»

Kutoka kwa Humran, mawlaa wa Uthman,

1- Amesimlia kwamba Othman bin Affan, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, aliomba maji ya kutawadha, na akatawadha, akaosha vitanga vyake viwili vya mikono mara tatu, kisha akaweka maji mdomoni mwake na kupandisha maji katika pua yake, kisha akaosha uso wake mara tatu, Kisha akaosha mkono wake wa kulia hadi kwenye kiwiko mara tatu, kisha akaosha mkono wake wa kushoto vivyo hivyo, kisha akapangusa kichwa chake, Kisha akaosha mguu wake wa kulia hadi vifundoni mara tatu, kisha akauosha wa kushoto vivyo hivyo.
2- Kisha akasema: Nilimuona Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam anatawadha kama mimi.
3- Kisha akasema Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam: “Mwenye kutawadha kama udhuu wangu huu, kisha akasimama na kusali rakaa mbili ambazo haongei nafsini mwake, atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.”
4- Na Muslim akaongeza katika riwaya: “Na itakuwa swala yake na kutembea kwake kuelekea msikitini ni ibada”  .

Othman bin Affan

Abu Amr, Abu Abdullah, Othman bin Affan bin Abi Al-Aas bin Umayyah bin Abd Shams, Dhun-Nurayn, na mwenye hijra mbili, mmoja wa waliotangulia kusilimu, Alioa mabinti wawili wa Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam, Ruqayyah na kisha Ummu Kulthum, Malaika walimwonea haya, na akatoa pesa zake katika njia ya Mwenyezi Mungu, alishika ukhalifa baada ya kuuawa Umar, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, na wakati wa utawala wake alifungua miji ya Armenia, Khurasan, Ifriqiya na mingineyo, na akakamilisha ukusanyaji wa Qur'ani na akaufanya kwenye Mus-haf mmoja ikiwa lengo kuu ni kuwaweka watu katika usomaji wa namna moja. Aliuawa kishahidi, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, katika mwaka wa (35 AH)[1]

Marejeo

  1. Tazama ufafanuzi wake katika: “Ma’rifat al-Sahaba” na Abu Naim (4/ 1952), “Tarikh al-Islam” cha al-Dhahabi (2/ 257), “Al-Isabah fi Tamayyiz al-Sahaba” na. Ibn Hajar (7/ 102).


Miradi ya Hadithi