عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ﷺ لِمُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ حِينَ بَعَثَهُ إِلَى اليَمَنِ: «إِنَّكَ سَتَأْتِي قَوْمًا أَهْلَ كِتَابٍ، فَإِذَا جِئْتَهُمْ، فَادْعُهُمْ إِلَى أَنْ يَشْهَدُوا أَنْ لا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، وَأَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ، فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوا لَكَ بِذَلِكَ، فَأَخْبِرْهُمْ أَنَّ اللَّهَ قَدْ فَرَضَ عَلَيْهِمْ خَمْسَ صَلَوَاتٍ فِي كُلِّ يَوْمٍ وَلَيْلَةٍ، فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوا لَكَ بِذَلِكَ، فَأَخْبِرْهُمْ أَنَّ اللَّهَ قَدْ فَرَضَ عَلَيْهِمْ صَدَقَةً تُؤْخَذُ مِنْ أَغْنِيَائِهِمْ فَتُرَدُّ عَلَى فُقَرَائِهِمْ، فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوا لَكَ بِذَلِكَ، فَإِيَّاكَ وَكَرَائِمَ أَمْوَالِهِمْ، وَاتَّقِ دَعْوَةَ المَظْلُومِ؛ فَإِنَّهُ لَيْسَ بَيْنَهُ وَبَيْنَ اللَّهِ حِجَابٌ» متفق عليه


Kutoka Ibn Abbas (r.a) amesema:

Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani ziwe juu yake, kumwambia Mua’dh ibn Jabal wakati alipomtuma kwenda yemen:

1. “Hakika wewe utawaendea watu wa kitabu 2. Utakapo waendea, walinganie kwenye shahada wakiri kwa moyo kuwa hakuna mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa yeye peke yake, na hakika Nabii Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. 3. Ikiwa watakukubalia hilo, basi waeleze kwamba hakika Mwenyezi Mungu amewafaradhishia sala tano mchana na usiku. 4. Ikiwa watakukubalia hilo, basi waeleze kuwa Mwenyezi Mungu amewafaradhishia juu yao, zaka ya mali zao, inachukuliwa kutoka kwa matajiri wao na inapelekwa kwa maskini wao.  5. Ikiwa watakukubalia hilo, basi jiepushe na kuchukua malizao bora zaidi. 6. Na ogopa duwa ya aliye dhulumiwa, kwani hakika hakuna kati yake na Mwenyezi Mungu pazia” . Imepokelewa na Bukhari na Muslimu. 

Miradi ya Hadithi