عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بن مسعود ، عَنِ النَّبِيِّ ﷺ قَالَ: «عَلَيْكُمْ بِالصِّدْقِ، فَإِنَّ الصِّدْقَ يَهْدِي إِلَى الْبِرِّ، وَإِنَّ الْبِرَّ يَهْدِي إِلَى الْجَنَّةِ، وَمَا يَزَالُ الرَّجُلُ يَصْدُقُ وَيَتَحَرَّى الصِّدْقَ حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اللهِ صِدِّيقًا، وَإِيَّاكُمْ وَالْكَذِبَ، فَإِنَّ الْكَذِبَ يَهْدِي إِلَى الْفُجُورِ، وَإِنَّ الْفُجُورَ يَهْدِي إِلَى النَّارِ، وَمَا يَزَالُ الرَّجُلُ يَكْذِبُ وَيَتَحَرَّى الْكَذِبَ حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اللهِ كَذَّابًا».

Kutoka kwa Abdullah bin Masoud Mwenyezi Mungu awe radhi naye, kutoka kwa Mtume, rehma na Amani zimshukie, ambaye amesema:

1- “kuweni wakweli, kwani ukweli humpeleka mtu kwenye wema, na wema humwongoza mtu kwenye Pepo, Na mtu huendelea kusema ukweli na kujitahidi kuwa mkweli mpaka aandikishwe kwa Mwenyezi Mungu kuwa ni mkweli.  

2- Na mwache kusema uongo, kwani uongo humpeleka mtu kwenye uovu, na uovu humwongoza mtu kwenye moto, na mtu huendelea kusema uongo na kujitahidi katika uongo mpaka, anaandikwa kwa Mwenyezi mungu kuwa ni mwongo.

Muhtasari wa Maana

Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam anafahamisha kuwa ukweli ni muongozo wa kila kheri, na unaopelekea kuingia Peponi, na kwamba mtu anazoea kusema kweli mpaka anaingia katika kundi la wakweli. Kwa upande mwingine, uwongo ni mlango wa uasi na uharibifu, na ni chanzo cha kuingia Motoni, na kwamba mtu huzoea kusema uwongo hadi akapigwa muhuri wa watu waongo.

Miradi ya Hadithi