عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ «مَنْ نَفَّسَ عَنْ مُؤْمِنٍ كُرْبَةً مِنْ كُرَبِ الدُّنْيَا، نَفَّسَ اللهُ عَنْهُ كُرْبَةً مِنْ كُرَبِ يَوْمِ الْقِيَامَةِ، وَمَنْ يَسَّرَ عَلَى مُعْسِرٍ، يَسَّرَ اللهُ عَلَيْهِ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِمًا، سَتَرَهُ اللهُ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ، وَاللهُ فِي عَوْنِ الْعَبْدِ مَا كَانَ الْعَبْدُ فِي عَوْنِ أَخِيهِ،  وَمَنْ سَلَكَ طَرِيقًا يَلْتَمِسُ فِيهِ عِلْمًا، سَهَّلَ اللهُ لَهُ بِهِ طَرِيقًا إِلَى الْجَنَّةِ،  وَمَا اجْتَمَعَ قَوْمٌ فِي بَيْتٍ مِنْ بُيُوتِ اللهِ، يَتْلُونَ كِتَابَ اللهِ، وَيَتَدَارَسُونَهُ بَيْنَهُمْ، إِلَّا نَزَلَتْ عَلَيْهِمِ السَّكِينَةُ، وَغَشِيَتْهُمُ الرَّحْمَةُ، وَحَفَّتْهُمُ الْمَلَائِكَةُ، وَذَكَرَهُمُ اللهُ فِيمَنْ عِنْدَهُ، وَمَنْ بَطَّأَ بِهِ عَمَلُهُ، لَمْ يُسْرِعْ بِهِ نَسَبُهُ».

Kutoka kwa Abu Hurayrah, amesema:

Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie amesema: 1. “Mwenye kumuondolea Muumini dhiki za kidunia, Mwenyezi Mungu atamwondolea moja ya dhiki za Siku ya Kiyama. 2. Na mwenye kumfanyia wepesi aliyesongwa na mambo, Mwenyezi Mungu atamfanyia wepesi duniani na akhera. 3. Na mwenye kumsitiri Muislamu, Mwenyezi Mungu atamsitiri duniani na Akhera. 4. Na Mungu humsaidia mja maadamu mja anamsaidia ndugu yake. 5. Na anaye pita njia kwa ajili ya kutafuta ilimu, Mwenyezi Mungu atamsahilishia njia ya kwenda Peponi. 6. Kila watu wanapokusanyika katika moja ya nyumba za Mwenyezi Mungu wakisoma Kitabu cha Mwenyezi Mungu. na wakisomeshana wao kwa wao, amani huwashukia. Na rehema huwafunika, Malaika huwazunguka, na Mwenyezi Mungu huwataja miongoni mwa walio pamoja Naye. 7. Na mwenye kucheleweshwa na vitendo vyake, nasaba yake haitamharakisha.”]



Abd al-Rahman ibn Sakhr al-Dawsi

MSIMULIZI: Ni: Abd al-Rahman ibn Sakhr al-Dawsi, al-Azdi, al-Yamani, anayejulikana sana kwa lakabu yake, “lakabu ni jina la kupewa tu kwa utani” na hili ndio jina mashuhuri zaidi ya majina yote yaliyosemwa juu yake na jina la baba yake. Ni sahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amanizimshukie. Alikuwa akienda naye popote aendapo, na alikuwa miongoni mwa masahaba walio hifadhi na kusimulia hadithi nyingi sana kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani ziwe juu yake, “kama alivyosema Al-Bukhari, Zaidi ya hadithi mia nane zilipokewa kutoka kwake –kati ya masahaba na matabiiy. Umar bin Al-Khattab aliMtumia kama gavana wa Bahrain, kisha akarudi na kuishi Madina na alikuwa ameshughulika na kusimulia hadithi na kuwafundisha watu kuhusu dini yao, na alikufa Madina mwaka wa (58 AH) [1]

Marejeo

  1. Rejea historia yake katika vitabu vifuatavyo: “Maarifaat al-Sahaba” na Abu Nu’aym (4/1846), “Alastieab Fi Maerifat Al'ashabi” na Ibn Abd al-Bar (4/1770), “Asad al-Ghaba” na Ibn al-Atheer (3/357), “Al-Isbah fi Tamazu al-Sahaba” cha Ibn Hajar al-Asqalani (4/267).


Miradi ya Hadithi