عَنْ أَبِي مَالِكٍ الْأَشْعَرِيِّ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ «الطُّهُورُ شَطْرُ الْإِيمَانِ، وَالْحَمْدُ للهِ تَمْلَأُ الْمِيزَانَ، وَسُبْحَانَ اللهِ وَالْحَمْدُ للهِ تَمْلَآنِ - أَوْ تَمْلَأُ - مَا بَيْنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ، وَالصَّلَاةُ نُورٌ، وَالصَّدَقَةُ بُرْهَانٌ، وَالصَّبْرُ ضِيَاءٌ، وَالْقُرْآنُ حُجَّةٌ لَكَ أَوْ عَلَيْكَ، كُلُّ النَّاسِ يَغْدُو، فَبَايِعٌ نَفْسَهُ فَمُعْتِقُهَا أَوْ مُوبِقُهَا»

Kutoka kwa Abu Malik Al-Ash’ariy Mwenyezi Mungu awe radhi naye ambaye amesema:

Mtume rehma na Amani zimshukie amesema: 1- “Usafi ni nusu ya imani, 2- Na kusema: Alhamdulilaah (Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu) inajaza mizani. 3- Na kusema: Subhaanallah) Ametakasika Mwenyezi Mungu, na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, hujaza au huyajaza yaliyo baina ya mbingu na ardhi. 4- Sala ni Nuru. 5- Na sadaka ni Ushahidi( juu ya Imani). 6- Subira ni mwangaza. 7- Na Qur’ani ni hoja kwako au dhidi yako. 8- Watu wote huondoka asubuhi, kwa hivyo yupo anayeiuza nafsi yake na akaiacha huru na mwengine akaiangamiza.”


1. ni utakaso kwa ujumla wake ikiwa ni pamoja na kutawadha kwa ajili ya swala na kufanya ibada ni sawa na nusu ya imani. Ikiwa muumini ameamriwa kuwa msafi kwa nje na ndani, basi usafi wa nje ni nusu ya hiyo, na imani inaweza kumaanisha ibada. Kama Asemavyo Mola Mtukufu:

“Na Mwenyezi Mungu si mwenye kupoteza imani zenu”

[Al-Baqara: 143]

yaani: sala zenu, na usafi ni nusu yake kwa sababu ni sharti ndani yake sala haikubaliki bila hiyo. Utakaso ni miongoni mwa ibada kubwa kabisa ambayo kwayo mja hujikurubisha kwa Mola wake. Amesema Allah, utukufu ni wake:

“Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubu na huwapenda wanao jisafisha”

[Al-Baqara: 222]

. Tunapata dalili kuwa kutokana na hili kwamba matendo yanajumuishwa katika imani, na kwamba inaongezeka kwa utiifu na inapungua kwa uasi. 

2- Na Mtume, rehma na amani zimshukie, amesema kuwa kauli ya mja:

“Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu” itajaza mizani ya mja Siku ya Kiyama kwa malipo yake makubwa, na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu. Mizani ni kitu kilichoandaliwa na Mwenyezi Mungu, ambacho amali za waja zitapimwa siku ya Qiyama, nayo ina visahani viwili. Ikiwa mizani ya wema itazidi, atakuwa miongoni mwa washindi, la sivyo atakatishwa tamaa na kupotea, Na akasema Allah utukufu ni wake: “Na Siku hiyo kipimo kitakuwa kwa Haki. Basi watakao kuwa na uzani mzito, hao ndio watakao fanikiwa (8) Na watakao kuwa na uzani khafifu, basi hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao kwa sababu ya kuzipinga Ishara zetu” .

[Al-A’raf: 8, 9]

3- Na kauli ya mja: “Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu” - na utukufu: kumtakasa Mwenyezi Mungu kutokana na kila upungufu na kasoro - kuna ujira mkubwa kiasi kwamba kama malipo hayo yangekuwa ni mwili, basi ungejaza vilivyo kati ya mbingu na ardhi. Basi kama malipo ya kusema: “Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu” yanajaza mizani, basi mja, akiifuatishia kwa kusema: “Utukufu ni wa Mwenyezi Mungu”, hupita juu ya malipo yao mpaka yajae yaliyo baina ya mbingu na ardhi, na hiyo ni kwa sababu ya kumhimidi Mola wake kwa yale anayostahiki, na akamtakasa na kila dosari na upungufu 

4- Kisha, Mtume rehema na amani zimshukie, akaeleza kuwa swala ni nuru inayomuongoza mja kwenye haki, hivyo moyo wa mwenye kusimamisha swala hujaa nuru za hekima, uongofu na elimu, sala na uasherati havikutani kamwe. Amesema Allah mtukufu :  

“Hakika Sala inazuilia mambo machafu na maovu”.

[Al-Ankabut: 45]

5- Sadaka ni ushahidi wa uaminifu wa imani ya mja. Mtu huzaliwa akiwa na sifa ya kupenda pesa, kwa hivyo ikiwa anajitahidi kuiondoa, hii ni ishara ya imani na imani yake. Pia ni dalili na hoja kwake mbele ya Mola wake Mlezi Siku ya Kiyama atakapoulizwa juu ya fedha zake alizipataje ? 

6- Subira - kwa namna zote: katika kumtii Mwenyezi Mungu, katika kumuasi, aliyetakasika, na katika Qadari zake – ni nuru ambayo kwayo mja anapata ufahamu katika njia ya haki.

 7- Qur’an ima ni hoja kwako ambayo itakunufaisha Siku ya Kiyama mbele ya Mwenyezi Mungu. Pale ulipoisoma na ukaiamini na ukanufaika na yale yaliyomo, au ni hoja ya kukuangamiza pale utapoiacha na ukaacha kuifanyia kazi. 

8- Kisha Mtume Rehema na Amani zimshukie akamalizia maneno yake kwa kusema kuwa watu wote wanajitahidi kutimiza maslahi yao - na akataja matembezi ya asubuhi, ambayo ni matembezi ya mwanzo wa mchana ambapo watu hukimbilia riziki zao - juhudi ya mtu ikiwa sambamba na Sharia, basi huyu kaiuza nafsi yake kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na Yeye ndiye anayeikomboa na kuiokoa kutokana na adhabu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

“Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwa kuwa wao watapata Pepo”

[Al-Tawba: 111]

Ama atakayefuata matamanio yake kinyume na amri ya Mwenyezi Mungu, Utukufu ni Wake, basi huyu kaiuza nafsi yake kwa Shetani, hivyo akaiangamiza na atastahiki adhabu kwa ajili yake.

Mafunzo

1- vile jitahidi kutakasa matendo yako ya siri kutokana na unafiki na dhambi kwani ni sehemu za imani. 

2- Usafi ni mojawapo ya milango muhimu ya upendo wa Mwenyezi Mungu kwa mja, kwa hiyo tumia fursa hiyo kwa kutaka radhi zake. 

3- “Sifa njema zote ni za Mungu” ni neno ambalo ni jepesi katika ulimi, na Muislamu haoni tabu yoyote ya kulirudia, na lina ujira mkubwa ambao hakuna awezaye kuuwekea mipaka isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Usipuuze kudumu na utajo huu. 

4- Mwenyezi Mungu ameweka malipo makubwa kwa kazi nyepesi; Ili kuwarahisishia waja Wake na kuwafanyia wema. Mwenyezi Mungu, utukufu ni Wake, ni Mola Mlezi mwenye rehema, huruma na ni mpole. 

5- Mizani ni kweli, iliyotajwa katika Qur’an na Sunnah, na Muumini hatakiwi kuto kuiamini. 

6- Weka ulimi wako unyevu kwa kusema: “Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema ni za Mungu”; malipo yake ni makubwa. 

7- Dumisha sala; kwani hutia nuru katika moyo wa muumini, inayomuongoza kwenye haki na kumdhihirishia upotovu.

8- Endelea kusali kwa wakati; Kwani ni nuru inayomulika kaburi la mja, ili apate faraja siku ya upweke.

9- Usiache kusali, kwani Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam atakutambueni kwayo Siku ya Kiyama. Pale inapoonekana nuru kutoka mwilini mwako, basi anakuita kwenye beseni lake na kukuombea uombezi, Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: “Siku ya Kiyama watu wangu wataitwa weupe, wenye kung’aa kutokana na athari za kutawadha” [1]

10- Mwenye nuru zaidi miongoni mwa watu ni yule mwenye kuchunga sana swala na masharti yake, nguzo, wajibu na Sunnah zake. 

11- Angalia nafsi yako mwenyewe; ukiikuta safi katika kutoa katika njia ya Mwenyezi Mungu, basi tulia na furahi, na ujue kwamba huu ni ushahidi wa imani yako, vinginevyo pigana na matamanio yako na shetani wako. 

12- Jua kwamba utawajibika Siku ya Kiyama kwa pesa zako, umezipata wapi na umezitoa kwenye nini? Ukitumia alichokupa Mwenyezi Mungu Kwa radhi yake, hiyo itakuwa ni hoja kwako ukiulizwa. 

13- Subira ina shida na taabu, lakini inazalisha nuru inayomuongoza aliyechanganyikiwa, kumfariji mpweke, na kumfariji aliyefiwa.

14- Mshairi alisema: Uvumilivu ni kama jina lake, chungu katika ladha ... lakini matokeo yake ni matamu kuliko asali. Ijaalie Qur’ani  kuwa ni hoja kwako, basi fanya haraka kuisoma, na utafakari maana yake, na ufanyie kazi hukumu zake. Hakika itamuombea mja Siku ya Qiyaamah kwa kusema: “Nilimzuia asilale usiku, basi nikubalie uombezi wangu kwake” [2] Hakuna anayestahiki fedheha na adhabu kuliko yule ambaye Mwenyezi Mungu alimpa Qur’ani na akampa ufahamu ndani yake, kisha akarudi nyuma kwa visigino vyake na akaacha kuifanyia kazi. Unataka lipi kati ya makundi mawili: mwenye kujikomboa kwa kufuata Sharia, au mwenye kuiharibu kwa kufuata matamanio ya nafsi yake?! Ewe unaeiuza nafsi yako, chagua bei nzuri zaidi; Ama uiuze hadi kufa na kuteswa, au uiuze mbinguni na kwa radhi za Mwenyezi Mungu. 

15- Mshairi alisema: 

Soma kitabu cha Mungu na uelewe hekima yake = utapata zawadi ya Mungu kwa ukarimu Hicho Kitabu ni usemi wa kweli kwa kila mwenye akili timamu = na ni mwangaza kwa nuru yake takatifu Inaongoza kwenye uzuri wa jumla, na ni usalama wa mioyo na faraja ya miili. Qur-aan ameiteremsha na Bwana, Hafidh = ili kumfundisha mwanadamu ufasaha bora kabisa.



Marejeo

1. Imepokewa na Al-Bukhari (136) na Muslim (246).

2. Imepokewa na Ahmad (6626).


Miradi ya Hadithi