39 - KUMUABUDU MWENYEZI MUNGU KATIKA UPENDO NA CHUKI, NA KUPENDA NA KUCHUKIA KWA AJILI YAKE

عَن أَنَسٍ رضي الله عنه، عن النَّبيِّ قال:«ثَلاثٌ مَن كُنَّ فيه وجَدَ حَلاوةَ الإِيمانِ:أَنْ يكونَ اللهُ ورَسُولُه أحَبَّ إلَيهِ ممَّا سِواهُما،وأَنْ يُحِبَّ المَرْءَ لا يُحِبُّه إلا للهِ، وأَنْ يَكْرَهَ أنْ يَعودَ في الكُفْرِ كما يَكْرَهُ أنْ يُقْذَفَ في النَّارِ»

Kutoka kwa Anasi (r.a), kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema:

1. “Mambo matatu yakiwepo kwa mtu atapata ladha ya imani. 2.Ni kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mtume wake ndio wanapendeza kwake zaidi kuliko wasiokuwa hao 3.Na kumpenda mtu na asimpende isipokuwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. 4. Na achukie kurudi kwenye ukafiri kama anavyo chukia kutupwa motoni”.



baba Hamza, au baba Thumamah, Anas bun Malik

baba Hamza, au baba Thumamah, Anas bun Malik, ukoo wa Annadhwari, Answari(ni katika waislaam walio mpokea Mtume Madina) amezaliwa miaka kumi kabla ya Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) kuhamia Madina, alikuwa ni mtumishi wa Mtume mara tu alivyo ingia Madina, na Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) alimuombea dua ya kujaliwa watoto wengi, mali, umri mrefu na kusamehewa dhambi. Akawa ana watoto wengi na mali, na alikuwa ni swahaba wa mwisho kufariki kwa walio kuwa katika mji wa Basra. Amefariki mwaka (93H) [1]

Marejeo

1.  Rejea  yake ufafanuzi wake katika: “Maarifaat al-Sahaba” na Abu Nu’aym (4/1846), “aliastieab fi maerifat al'ashabi"na Ibn Abd al-Bar (4/1770), “Asad al-Ghaba” na Ibn al-Atheer (3/357), “Al-Isbah fi Tamazu al-Sahaba” cha Ibn Hajari Asqalani (4/267) .


Miradi ya Hadithi