عَنْ أَبِي مَسْعُودٍ، قَالَ النَّبِيُّ ﷺ: «إِنَّ مِمَّا أَدْرَكَ النَّاسُ مِنْ كَلاَمِ النُّبُوَّةِ: إِذَا لَمْ تَسْتَحْيِ فَاصْنَعْ مَا شِئْتَ»[1].

Kutoka kwa Abu Masoud, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, amesema Mtume rehma na Amani zimshukie:

“Katika maneno ya bishara ya utume waliyoyapata watu ni: Ikiwa hauna haya, basi fanya chochote unachotaka”

Muhtasari wa Maana

Watu walirithi kutoka kwa maneno ya Manabii waliotangulia na sheria zao, kusema kwao: “Ikiwa huna haya, basi fanya utakalo.” Yaani, staha inamzuia mwenye nayo maovu mengi, kwa hivyo asiyekuwa na staha, hakuna kitakachoweza kumzuia asifanye anachotaka.

Miradi ya Hadithi