عَنْ أَبِي ذَرٍّ رضي الله عنه أَنَّ نَاسًا مِنْ أَصْحَابِ النَّبِيِّ ﷺ قَالُوا لِلنَّبِيِّ ﷺ: يَا رَسُولَ اللهِ، ذَهَبَ أَهْلُ الدُّثُورِ بِالْأُجُورِ، يُصَلُّونَ كَمَا نُصَلِّي، وَيَصُومُونَ كَمَا نَصُومُ، وَيَتَصَدَّقُونَ بِفُضُولِ أَمْوَالِهِمْ، قَالَ: «أَوَلَيْسَ قَدْ جَعَلَ اللهُ لَكُمْ مَا تَصَّدَّقُونَ؟ إِنَّ بِكُلِّ تَسْبِيحَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَكْبِيرَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَحْمِيدَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَهْلِيلَةٍ صَدَقَةً،  وَأَمْرٌ بِالْمَعْرُوفِ صَدَقَةٌ، وَنَهْيٌ عَنْ مُنْكَرٍ صَدَقَةٌ، وَفِي بُضْعِ أَحَدِكُمْ صَدَقَةٌ»قَالُوا: يَا رَسُولَ اللهِ، أَيَأتِي أَحَدُنَا شَهْوَتَهُ وَيَكُونُ لَهُ فِيهَا أَجْرٌ؟ قَالَ: «أَرَأَيْتُمْ لَوْ وَضَعَهَا فِي حَرَامٍ، أَكَانَ عَلَيْهِ فِيهَا وِزْرٌ؟ فَكَذَلِكَ إِذَا وَضَعَهَا فِي الْحَلَالِ كَانَ لَهُ أَجْرٌ».

Kutoka Kwa Abu Dharr, Mwenyezi Mungu awe radhi naye 1- Kwamba maswahaba walimwambia Mtume rehma na Amani zimshukie: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Watu wenye mali wamekwenda na ujira wao mkubwa, wanaswali tunaposwali, wanafunga sisi tunapofunga, na wanatoa sadaka kutokana na fedha zao za ziada. 2- Akasema Mtume: Je! Mwenyezi Mungu hakukufanyieni sadaka mnazotoa? 3- Kumtakasa Mwenyezi Mungu ni sadaka, kila kumtukuza ni sadaka, kila neno la kumsifu ni sadaka, na kila tahlili ni sadaka. 4- Kuamrisha mema ni sadaka, na kukataza maovu ni sadaka. 5- Na katika ndoa ya mmoja wenu kuna sadaka. 6- Wakasema maswahaba: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, vipi mmoja wetu akidhi matamanio yake kisha apate ujira ?  Akasema Mtume: “Je, mnaonaje kama akiyaweka matamanio hayo kwenye haramu atapata dhambi ?” Basi akifanya katika halaali anapata thawabu"


Vitendawili vya Qur'ani Vinavyohusiana

Amesema Mwenyezi Mungu mtukufu: “Wote hao si sawa sawa. Miongoni mwa Watu wa Kitabu wamo watu walio simama baraabara, wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku, na pia wanasujudu (113) Wanamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na wanaamrisha mema na wanakataza maovu na wanakimbilia katika mambo ya kheri. Na hao ndio miongoni mwa watenda mema (114) Na kheri yoyote wanayo ifanya hawatanyimwa malipo yake. Na Mwenyezi Mungu anawajua wachamngu” .

[Al-Imran: 113-115]

Na akasema Mwenyezi mtukufu: “Hapana lawama kwa wanyonge, wagonjwa, na wasio pata cha kutumia, maadamu wanamsafia niya Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hapana njia ya kuwalaumu wanao fanya wema. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu (91) Wala wale walio kujia ili uwachukue ukasema: Sina kipando cha kukuchukueni. Tena wakarudi na macho yao yanamiminika machozi kwa huzuni ya kukosa cha kutoa (92) Ipo njia ya kuwalaumu wale wanao kuomba ruhusa wasende vitani na hali wao ni matajiri. Wameridhia kuwa pamoja na wanao bakia nyuma. Na Mwenyezi Mungu amewapiga muhuri juu ya nyoyo zao. Kwa hivyo hawajui” . 

[At-Tawbah: 91-93]

 

Na pia akasema mtukufu: “Mwisho wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana” .

[Al-Mutaffifien: 26]

Miradi ya Hadithi