عَنْ أَبِي ذَرٍّ رضي الله عنه أَنَّ نَاسًا مِنْ أَصْحَابِ النَّبِيِّ ﷺ قَالُوا لِلنَّبِيِّ ﷺ: يَا رَسُولَ اللهِ، ذَهَبَ أَهْلُ الدُّثُورِ بِالْأُجُورِ، يُصَلُّونَ كَمَا نُصَلِّي، وَيَصُومُونَ كَمَا نَصُومُ، وَيَتَصَدَّقُونَ بِفُضُولِ أَمْوَالِهِمْ، قَالَ: «أَوَلَيْسَ قَدْ جَعَلَ اللهُ لَكُمْ مَا تَصَّدَّقُونَ؟ إِنَّ بِكُلِّ تَسْبِيحَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَكْبِيرَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَحْمِيدَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَهْلِيلَةٍ صَدَقَةً،  وَأَمْرٌ بِالْمَعْرُوفِ صَدَقَةٌ، وَنَهْيٌ عَنْ مُنْكَرٍ صَدَقَةٌ، وَفِي بُضْعِ أَحَدِكُمْ صَدَقَةٌ»قَالُوا: يَا رَسُولَ اللهِ، أَيَأتِي أَحَدُنَا شَهْوَتَهُ وَيَكُونُ لَهُ فِيهَا أَجْرٌ؟ قَالَ: «أَرَأَيْتُمْ لَوْ وَضَعَهَا فِي حَرَامٍ، أَكَانَ عَلَيْهِ فِيهَا وِزْرٌ؟ فَكَذَلِكَ إِذَا وَضَعَهَا فِي الْحَلَالِ كَانَ لَهُ أَجْرٌ».

Kutoka Kwa Abu Dharr, Mwenyezi Mungu awe radhi naye 1- Kwamba maswahaba walimwambia Mtume rehma na Amani zimshukie: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Watu wenye mali wamekwenda na ujira wao mkubwa, wanaswali tunaposwali, wanafunga sisi tunapofunga, na wanatoa sadaka kutokana na fedha zao za ziada. 2- Akasema Mtume: Je! Mwenyezi Mungu hakukufanyieni sadaka mnazotoa? 3- Kumtakasa Mwenyezi Mungu ni sadaka, kila kumtukuza ni sadaka, kila neno la kumsifu ni sadaka, na kila tahlili ni sadaka. 4- Kuamrisha mema ni sadaka, na kukataza maovu ni sadaka. 5- Na katika ndoa ya mmoja wenu kuna sadaka. 6- Wakasema maswahaba: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, vipi mmoja wetu akidhi matamanio yake kisha apate ujira ?  Akasema Mtume: “Je, mnaonaje kama akiyaweka matamanio hayo kwenye haramu atapata dhambi ?” Basi akifanya katika halaali anapata thawabu"


1- Amani zimshukie wakimlalamikia kuwa matajiri, wenye fedha, wamehodhi vyeo vya juu Peponi. Wanashiriki nao katika ibada za kimwili kama vile swala, saumu na jihadi, na wametengwa kwa ajili ya ibada ya fedha kama vile sadaka na kutumia katika haki.

Hii sio husuda kwa matajiri, wala si kupinga kudra ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, bali walikwenda kwa Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam ili awatafutie ibada itayokuwa sawa na malipo ya sadaka. Wanaweza kushindana na matajiri katika matendo mema [1]

2- Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam akawaelekeza kwenye ibada ambayo itachukua nafasi ya sadaka na inayostahiki ujira wake kutokana na kujikurubisha kwa Allah na kutenda matendo mema.

3- Basi akawaambia kwamba dhikri (kumtaja Mwenyezi Mungu mtukufu) inanafasi ya sadaka. Hivyo takbira, kumhimidi Mwenyezi Mungu, tasbihi na tahlili - ambayo ni kusema: Hapana Mola ila Mwenyezi Mungu mmoja- ni sadaka ambazo mja atalipwa. Bali hupendeza zaidi kwa Mwenyezi Mungu kuliko sadaka. Kwa kauli yake Mtume, rehma na Amani zimshukie: “Je! niwaambieni mema ya vitendo vyenu, vilivyo safi mbele ya Mola wenu Mlezi, na aliye juu katika safu zenu? Na ni bora kwenu kuliko kutoa dhahabu na fedha, na ni bora kwenu kuliko kukutana na adui yenu mkawapiga shingo zao, na wakakupigeni shingo zenu? Wakasema Maswahaba: Ndio, ewe Mtume wa Mwenyezi Munguk ,Akasema: “Kumkumbuka Mwenyezi Mungu Mtukufu” [2]

4- Kama vile kuwaamrisha watu kutenda mema na kuwaongoza kwenye haki ni sadaka, na kuwakataza maovu ni sadaka, bali ni miongoni mwa ibada za juu kabisa. Mwenyezi Mungu alivyoutofautisha ummah huo kwa ajili ya hilo; Amesema Mwenyezi Mungu Aliyetakasika:

“Nyinyi ndio Umma bora ulio tolewa kwa watu, unao amrisha mema na unakataza maovu, na unamuamini Mwenyezi Mungu” .

[Al-Imran: 110]

Vile vile kuamrisha mema na kukataza maovu ni faradhi tosha, na huenda ikawa ni lazima, lakini tasbihi, kusifu, na tahlili ni jambo la sunnah, na inajulikana kuwa malipo ya wajibu ni zaidi ya malipo ya sunnah. Kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema katika Hadithi Qudsi: “Na mja Wangu hajikurubishi Kwangu na kitu kinachopendwa zaidi Kwangu kuliko kutekeleza yale niliyowajibisha juu yake”[3] “[4]

Sadaka isiyokuwa ya mali iko sehemu mbili: Ibada ambayo inakomea kwa anaye itekeleza; kama dhikri na kutekeleza ibada za sunnah, na kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu mtukufu kuliko pita kiasi; Kama vile kuamrisha mema na kukataza maovu, na kueneza elimu, kuwanufaisha Waislamu, na kuwaepusha na madhara. Ni bora kuliko aina ya kwanza kutokana na fadhila zake za jumla.

Hili halikomei kwa yale yaliyotajwa juu ya matendo mema, bali kila anachofanya Muislamu kwa utiifu ni sadaka, na katika Hadith: “Kila tendo jema ni sadaka” [5]

5- Bali mwanamume akimwingilia mke wake basi anayo sadaka. Hiyo ni ikiwa ana nia ya kujihifadhi na zinaa, au kumhifadhi mke wake na kuishi naye kwa wema, au ikiwa anaomba mtoto mwema, au nia nyingine nzuri [6] 

6- Maswahaba, sala na salam ziwe juu yao, walishangaa. Kwani vipi mtu atatimiza matamanio yake na kupata malipo kwa hayo?! Basi Mtume rehma na amani iwe juu yake, akawaambia kwamba kama mtu anavyochuma dhambi akiweka matamanio yake katika haramu, basi atapata ujira akiiweka katika halali.

Mafunzo

1- wakishindana katika mambo ya kheri, na furaha ya ndugu zao kwa yale waliyoyafanya katika utiifu. Haya ndiyo mashindano ya kweli ambayo kila Muislamu anapaswa kuyatamani.

2- Jambo la furaha ni Muislamu kutamani vile alivyo navyo ndugu yake, na kumtakia baraka nduguye kwa alichonacho, na ni jambo zuri katika kufanya ibada, kwa sababu Mtume, rehema na amani zimshukie Amesema: Hakuna husuda ila kwa watu wawili: Mtu ambaye Mwenyezi Mungu amempa Mali, basi akawa anazitumia na kuzisalitisha katika njia sahihi, na Mtu ambaye Mwenyezi Mungu amempa elimu na hekima, na akawa anahukumu kwayo na anaifundisha”

3- Ni kutokana na rehema na uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwamba amewafanyia masikini kile ambacho kinawafikisha kwenye daraja ya matajiri. Hivyo kila Muislamu afanye hima kumtii Mwenyezi Mungu Mtukufu  kwa namna yeyote itakayo wezekana.

4- Kumdhukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu ni miongoni mwa sifa bora kabisa za waja wema. Mtu mmoja akasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, sheria za Uislamu zimenishinda, basi niambie kitu cha kushikamana nacho. Akasema: “Ulimi wako uendelee kulowa kwa kumtaja Mwenyezi Mungu” [7] 

5- Wale wanaofurahia starehe hawajafurahi kama mfano wa furaha anayokuwa nayo mwenye kumtaja Mwenyezi Mungu; Hakuna ibada ambayo ni nyepesi katika ulimi, wala kubwa katika raha, wala furaha na shangwe zaidi kwa moyo kuliko kumkumbuka Mwenyezi Mungu Mtukufu [8]

6- Kuwa na shauku ya kuamrisha mema na kukataza maovu; Ni sifa ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu amewahusisha watu wa hali ya juu katika viumbe vyake, na akalisifu taifa hilo na kulifanya kuwa taifa bora zaidi kati ya mataifa.

7- Kuamrisha mema ni pamoja na vitendo vyote vya utiifu kama vile kufundisha Qur-aan na Elimu zenye manufaa, kuwafanyia watu wema, na kutowadhuru.

8- Kwa nia njema, mtu hulipwa utiifu na wema, kwa hivyo tumia fursa hiyo katika nyanja zote za maisha yako. Basi wakati wa kula tia niya ya kutafuta nguvu ya kufanya ibada, na wakati wa kulala tia niya ya kupumzika ili kuendelea na ibada, na wakati wa kuchumbia familia na watoto: tia niya ya kutimiza haki zao na uhusiano mzuri nao, na wakati wa kusoma: uweke niya ya kutafuta elimu kwa faida ya Waislamu, na kazini: kuinua hadhi ya Waislamu. Na kwa kufanya hivyo katika kila kinachoruhusiwa, hugeuka kuwa matendo ya utiifu ambayo yatalipwa. Muadh bin Jabal Mwenyezi Mungu awe radhi naye amesema: “Nakusudia kwa usingizi kupata thawabu  kama vile ninavyo kusudia kupata thawabu wakati nikiwa macho” [9] 

9- Moja ya ukarimu mkubwa wa Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kwamba Yeye humlipa Muislamu kheri kwa matendo yake yote yanayoruhusiwa ikiwa atajiepusha na dhambi. Hulipwa thawabu kwa kula chakula kilicho halali kwa kuwa ameacha haramu, na hukidhi matamanio yake katika halali na kuyaacha matamanio ya haramu, na kupata pesa kwa halali bila ya haramu.

10- Katika Hadithi, inajuzu kumuuliza muulizaji kuhusu baadhi ya yale yaliyofichika kwenye dalili ikiwa anajua kutokana na hali ya muulizaji kuwa hatachukia hilo, na hakuna tabia mbaya ndani yake. [10]

11- Mshairi alisema:

Jitahidi kumtaja Mungu, ewe mtafutaji malipo = Ewe mwenye kutaka kheri, upendeleo, na wema

Fanya hivyo utapewa mahitajio yote = na utakingwa na matatizo na madhara.

Basi anayemtaja Mwingi wa Rehema hukaa naye = na anayemtaja Mwenyezi Mungu humlipa utajo.

Na asiye mtaja Mwenyezi Mungu, basi huyo ni rafiki yake Shetani moyoni mwake.

Na anayemsahau Mola wake Mlezi, basi Mola wake Mlezi = humsahau na hiyo ni hasara kubwa

Ibilisi akammiliki, na akamsahaulisha kumtaja Mola ambaye = Kamfanya awepo toka mwanzo.

 

Marejeo

1. Tazama: “Ufafanuzi wa Riyadh as-Salihin” cha Ibn Uthaymiyn (2/ 161).

2. Imepokewa na Ahmed (21702) na Al-Tirmidhiy (3377).

3. Imepokewa na Al-Bukhari (6502).

4. Sherh  ya An-Nawawi alaai Muslim (7/92).

5. Imepokewa na Al-Bukhari (6021) na Muslim (1005).

6. sherh ya Al-Nawawi Alaa Muslim” (7/92).

7. Imepokewa na Ahmad (18167), Ibn Majah (3793), na Al-Tirmidhiy (3375)]

8. Al-Waabil al-Saib min al-Kalim al-Tayyib” cha Ibn al-Qayyim (uk. 81).

9. Imepokewa na Al-Bukhari (4341) na Muslim (1733).

10. Ufafanuzi wa Al-Nawawi Alaa Muslim” (7/93).



Miradi ya Hadithi