عن أبي هريرة رضي الله عنه، قال: قال رسولُ الله ﷺ: «مَن لم يَدَعْ قولَ الزُّورِ والعَمَلَ به والجهلَ، فليس لله حاجةٌ في أن يَدَع طعامَه وشَرَابَه».

Kutoka kwa Abu Huraira Mwenyezi Mungu awe radhi naye amesema:

Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie: “Yeyote asiyeacha maneno ya uwongo na kuyafanyia kazi na ujinga, basi Mwenyezi Mungu hana haja naye kwa kuacha chakula na kinywaji chake.”


Vitendawili vya Qur'ani Vinavyohusiana

Amesema Mwenyezi mtakatifu: “Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Saumu, kama waliyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allah ”

[Al-Baqarah: 183].

Na akasema Allah ambaye jina lake ni tukufu: “Basi jiepusheni na uchafu wa masanamu, na jiepusheni na usemi wa uwongo” .

[Hajj: 30]

Mwenyezi Mungu amesema: “Na waja wa Arrahman Mwingi wa Rehema ni wale wanao tembea ulimwenguni kwa staha, na wajinga wakiwasemeza hujibu kwa  kusema : Amani” .

[Al-Furqan: 63]

Amesema Allah Mtukufu : “Na wale ambao hawatoi ushahidi wa uwongo, na pindi wapitapo penye upuuzi, hupita kwa hishima yao”.

[Al-Furqan: 72]

Miradi ya Hadithi