عن أبي هريرة رضي الله عنه، قال: قال رسولُ الله ﷺ: «مَن لم يَدَعْ قولَ الزُّورِ والعَمَلَ به والجهلَ، فليس لله حاجةٌ في أن يَدَع طعامَه وشَرَابَه».

Kutoka kwa Abu Huraira Mwenyezi Mungu awe radhi naye amesema:

Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie: “Yeyote asiyeacha maneno ya uwongo na kuyafanyia kazi na ujinga, basi Mwenyezi Mungu hana haja naye kwa kuacha chakula na kinywaji chake.”


Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake amesema kuwa lengo kuu la funga ni uchamungu na kuhifadhi ulimi na viungo. Mwenyezi Mungu anasema:

“Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Saumu, kama waliyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allah ”

[Al-Baqarah: 183]

. Anayefunga chakula na vinywaji, na viungo vyake havijiepushi na kusema uwongo na kuufanyia kazi - ambayo ni maneno ya uwongo, na ni pamoja na kusema uwongo, kusengenya, kuteta na mengineyo katika maafa ya  ulimi. Na hakuacha upumbavu, uzembe, kutokuwa na huruma, na yanayofungamana na hayo, kama mapigano, vurugu, na makelele yaliyoharamishwa kwa kauli yake, amani iwe juu yake. "Na ikiwa ni siku ambayo mmoja wenu amefunga, basi asifanye uchafu au kupiga kelele, na kama mtu akimtukana au akampiga, basi na aseme: Mimi ni nimefunga ."  = Saumu yake haikubaliwi na haizingatiwi. [1]

Na Mtume, amani iwe juu yake, alieleza kwa kusema: "Mwenyezi Mungu hana haja" kuashiria kutokuiangalia, kutojali na ktokuikubalika, kama unavyosema: Sina haja ya fulani na fulani. Vinginevyo Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, amejitosheleza na walimwengu, na wala hahitaji chochote kutoka kwao. Akasema, Utukufu ni Wake:

“Enyi watu! Nyinyi ndio wenye haja kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujitosha, Mwenye kusifiwa”.

[Fatir: 15]

Mwenyezi Mungu Mtukufu ameharamisha uwongo kwa kusema:

“Basi jiepusheni na uchafu wa masanamu, na jiepusheni na kusema uwongo”

[Hajj: 30].

Aliwasifu waja wake ambao hawashuhudii uwongo; Hawasemi, msiifanyie kazi, wala msikae katika mkusanyiko wake.” Akasema Mwenyezi Mungu:

“Na wale ambao hawatoi ushahidi wa uwongo, na pindi wapitapo penye upuuzi, hupita kwa hishima yao”.

[Al-Furqan: 72]

Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake ametaja kuwa uwongo ni miongoni mwa madhambi makubwa zaidi, basi akasema: “Je, nikujuze dhambi kubwa katika madhambi makubwa? Mara tatu walisema: Ndio, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, amesema: “Kumshirikisha Mwenyezi Mungu, kuwaasi wazazi, Na alikuwa ameegemea akakaa, na akasema: Tambueni! Na maneno ya uwongo.” Akasema: Akaendelea kurudia mpaka tukasema: Laiti angenyamaza” [2]

Kinachomaanishwa na uwajibu na sheria ya kufunga si kupata njaa na kiu; Bali, makusudio ni kupatikana hali ya kuyavunja matamanio, kuzima hasira, na kunyenyekea nafsi ambayo inaamrisha nafsi tulivu. Endapo mfungaji hakuifikia hali hiyo, na nafsi yake haikuathirika kwa kufunga isipokuwa kwa njaa na kiu, Kwani Mtume, amani iwe juu yake, amesema: “Huwenda mfungaji hana chochote katika saumu yake isipokuwa njaa, na Huwenda aliyesimama kusali usiku hana chochote isipokuwa kukesha” [3] Wakati huo, ndio Mwenyezi Mungu hajali kufunga kwake, na haangalii kwa kukubali; ni kwa sababu Hakufikia lengo la saumu yake [4]

MAFUNDISHO

  1. Iwapo Mwenyezi Mungu Mtukufu amebainisha malipo ya saumu, na akajulisha kwa kauli yake yeye aliye tukuka : “Kila amali ya mwana wa Adamu ni yake, isipokuwa saumu; Ni yangu”  [5] , ikionyesha ukubwa wa malipo yake na hadhi yake ya juu, kisha mja  anatamka neno la kumchukiza Mwenyezi Mungu, linakuwa sababu ya kuharibu malipo haya yote na kumkatisha tamaa; Huu ni ushahidi wa hatari ya maneno na vitendo vya uwongo, na kwamba ni moja ya adhabu na balaa inayomsababishia mwanadamu hasara ya dunia na Akhera, hivyo Muislamu ajihadhari na dhambi hii, na ajiweke mbali na kuilinda kazi yake.

  2. Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwataka waja wake wamche, wamtii, na waepuke makatazo yake, na wala hakutaka kuwabana kwa kuacha kula, kunywa na kujamiiana. Bali, alitaka watii amri zake na kuepuka makatazo yake; Ili swaumu hiyo iwe shule ambayo wanazoea kuacha yaliyoharamishwa na kutekeleza majukumu.

  3. Makusudio ya Saumu ni kuivunja nafsi na kuacha yale yaliyoharamishwa, na si kuacha chakula na vinywaji tu vinavyojuzu [6]

  4. Jua kwamba haiwezekani kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kuacha matamanio haya yanayoruhusiwa ukiwa hauko katika saumu isipokuwa baada ya kujikurubisha Kwake kwa kuacha yale aliyoharamisha Mwenyezi Mungu kwa kila hali, kama uwongo, dhulma na uadui dhidi ya watu. kwa damu zao, pesa, na heshima [7].

  5. Mwenyezi Mungu Mtukufu ameharamisha maneno ya uwongo kama vile alivyoharamisha kuyafanyia kazi, na hayo ni pamoja na kusengenya, kuteta, kutega watu, kuamrisha maovu na kukataza mema, na mambo mengine ya uwongo.

  6. Mshairi alisema:

Ewe ambaye uliyefunga chakula = ni bora kwako ungalifunga kudhulumu

Je, kufunga kunamnufaisha mtu dhalimu = haliyakuwa Utumbo wake umejaa dhambi

7. Wengine walisema:

Ichunge saumu yako kwa kunyamaza kutokana na porojo = na ufunike macho yako kwa kope

Usitembee kwa watu ukiwa na nyuso mbili = mtu muovu zaidi ni yule mwenye nyuso mbili.


Marejeo

1. Imepokewa na Al-Bukhari (1904) na Muslim (1151), kwa kutoka kwa Abu Hurayrah (ra) .

2. Imepokewa na Al-Bukhari (2654) na Muslim (87).

3.  Imepokewa na Al-Nasa’i katika “Al-Sunan Al-Kubra” (3236) na Ibn Majah (1690).

4. “Tuhfat Al-Abrar Sharh Misbah Al-Sunnah” cha Al-Baidawi (1/497).

5. Imepokewa na Al-Bukhari (1904) na Muslim (1151).

6. “Al-Mafetah fi Sharh Al-Masabih” cha Al-Mazhari (3/24). 

7. “Latif al-Maaref” cha Ibn Rajab (uk. 155).


Miradi ya Hadithi