17 - KULAZIMIANA NA KUMFUATA MTUME MUHAMMAD

عن الْمِقدامِ بنِ مَعْدِي كَرِبَ رضى الله عنه أن النبيَّ قال: «ألا هل عسى رجُلٌ يَبْلُغُه الحديثُ عَنِّي وهو مُتَّكِئٌ على أريكته، فيقول: بينَنا وبينَكم كتابُ الله، فما وجدْنا فيه حلالًا استَحْلَلناه، وما وجدْنا فيه حرامًا حرَّمناه، وإنَّ ما حرَّمَ رسولُ الله ﷺ كما حرَّمَ اللهُ». وفي لفظ أبي داودَ: «ألا إني أوتيتُ الكتابَ ومثلَه معه».


Kutoka kwa Al-Miqdaam bin Maadi Karb, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, kwamba Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam amesema:

“Je, inawezekana kwa mtu kumpa khabari ya Hadithi kutoka kwangu akiwa ameegemea kiti chake, na akasema: Baina yetu na nyinyi kuna Kitabu cha Mwenyezi Mungu, basi chochote tunachokikuta humo ni halali tunaihalalisha, na tunayoyakuta ndani yake kuwa ni haramu tunayaharamisha.Aliyoharamisha Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam nayo ni haramu kwa Mwenyezi Mungu.”Kwa kauli ya Abu Daawuud: “Nimepewa Kitabu (Qur`an)  pamoja na mfano wake ”.

Muhtasari wa Maana

Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam amekataza baadhi ya watu kukanusha hojja na dalili ya Sunnah kwa madai kuwa yaliyomo ndani ya Qur’an yanatosha. Sunnah ni wahyi kama Qur-aan.

Miradi ya Hadithi