148 - KUHIFADHI TOBA KWA KUFANYA MATENDO MEMA

عَنْ حَكِيمِ بْنِ حِزَامٍ رضي الله عنه، قَالَ: قُلْتُ: يَا رَسُولَ اللَّهِ، أَرَأَيْتَ أَشْيَاءَ كُنْتُ أَتَحَنَّثُ بِهَا فِي الجَاهِلِيَّةِ مِنْ صَدَقَةٍ أَوْ عَتَاقَةٍ، وَصِلَةِ رَحِمٍ، فَهَلْ فِيهَا مِنْ أَجْرٍ؟  فَقَالَ النَّبِيُّ : «أَسْلَمْتَ عَلَى مَا سَلَفَ مِنْ خَيْرٍ»

Kutoka kwa Hakim bin Hizam, Allah amuwiye radhi, amesema:

1- Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, unaonaje mambo niliyokuwa nikiyaahidi kabla ya Uislamu, kama vile kutoa sadaka au kuwaacha huru watumwa, kuunga udugu, je nitapata dhawabu? 

2- Akasema Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam: “Umeyasilimisha yote yaliyotangulia katika kheri” ).

Muhtasari wa Maana

Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam aliulizwa kuhusu hatima ya matendo mema kabla ya Uislamu, na akaeleza kuwa mja akiingia katika Uislamu atalipwa kwa mema aliyoyafanya kabla ya kusilimu.

Miradi ya Hadithi