عن أبي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه، قال:سَأَلَ رَجُلٌ رَسُولَ اللهِ ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللهِ، إِنَّا نَرْكَبُ البَحْرَ، وَنَحْمِلُ مَعَنَا القَلِيلَ مِنَ الْمَاءِ، فَإِنْ تَوَضَّأْنَا بِهِ عَطِشْنَا، أَفَنَتَوَضَّأُ مِنَ الْبَحْرِ؟ فَقَالَ رَسُولُ اللهِ : «هُوَ الطَّهُورُ مَاؤُهُ، الحِلُّ مَيْتَتُهُ»

Kutoka kwa Abu Hurayrah, Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake  amesema:

1.mtu mmoja alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani ziwe juu yake) akasema: “ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, sisi husafari safari za baharini, na katika safari zetu hubeba maji machache, ikiwa tutayatumia kupata udhu basi tutapata kiu – kwa kukosa maji ya kunywa- je inafaa tupate udhu kwa maji ya bahari? 

2. akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake: “maji yake ni twahara”. 

3. na kilichofia baharini ni halali"

Muhtasari wa Maana

Mtu mmoja alimuuliza Mtume (Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake) kuhusu kupata udhu kwa maji ya bahari, akamwambia kuwa maji hayo ni masafi, na kwamba mizoga yake inajuzu kuliwa.

Miradi ya Hadithi