عن أبي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه، قال:سَأَلَ رَجُلٌ رَسُولَ اللهِ ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللهِ، إِنَّا نَرْكَبُ البَحْرَ، وَنَحْمِلُ مَعَنَا القَلِيلَ مِنَ الْمَاءِ، فَإِنْ تَوَضَّأْنَا بِهِ عَطِشْنَا، أَفَنَتَوَضَّأُ مِنَ الْبَحْرِ؟ فَقَالَ رَسُولُ اللهِ : «هُوَ الطَّهُورُ مَاؤُهُ، الحِلُّ مَيْتَتُهُ»

Kutoka kwa Abu Hurayrah, Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake  amesema:

1.mtu mmoja alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na amani ziwe juu yake) akasema: “ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, sisi husafari safari za baharini, na katika safari zetu hubeba maji machache, ikiwa tutayatumia kupata udhu basi tutapata kiu – kwa kukosa maji ya kunywa- je inafaa tupate udhu kwa maji ya bahari? 

2. akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake: “maji yake ni twahara”. 

3. na kilichofia baharini ni halali"

Abd al-Rahman ibn Sakhr al-Dawsi

MSIMULIZI: Ni: Abd al-Rahman ibn Sakhr al-Dawsi, al-Azdi, al-Yamani, anayejulikana sana kwa lakabu yake, “lakabu ni jina la kupewa tu kwa utani” na hili ndio jina mashuhuri zaidi ya majina yote yaliyosemwa juu yake na jina la baba yake. Ni sahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amanizimshukie. Alikuwa akienda naye popote aendapo, na alikuwa miongoni mwa masahaba walio hifadhi na kusimulia hadithi nyingi sana kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani ziwe juu yake, “kama alivyosema Al-Bukhari, Zaidi ya hadithi mia nane zilipokewa kutoka kwake –kati ya masahaba na matabiiy. Umar bin Al-Khattab aliMtumia kama gavana wa Bahrain, kisha akarudi na kuishi Madina na alikuwa ameshughulika na kusimulia hadithi na kuwafundisha watu kuhusu dini yao, na alikufa Madina mwaka wa (58 AH) [1]

Marejeo

  1. Rejea historia yake katika vitabu vifuatavyo: “Maarifaat al-Sahaba” na Abu Nu’aym (4/1846), “Alastieab Fi Maerifat Al'ashabi” na Ibn Abd al-Bar (4/1770), “Asad al-Ghaba” na Ibn al-Atheer (3/357), “Al-Isbah fi Tamazu al-Sahaba” cha Ibn Hajar al-Asqalani (4/267).


Miradi ya Hadithi