عن عمَّارِ بنِ ياسرٍ رضي الله عنهما قال:بَعَثَنِي رَسُولُ اللهِ ﷺ فِي حَاجَةٍ فَأَجْنَبْتُ، فَلَمْ أَجِدِ الْمَاءَ، فَتَمَرَّغْتُ فِي الصَّعِيدِ كَمَا تَمَرَّغُ الدَّابَّةُ، ثُمَّ أَتَيْتُ النَّبِيَّ ﷺ، فَذَكَرْتُ ذَلِكَ لَهُ، فَقَالَ: «إِنَّمَا كَانَ يَكْفِيكَ أَنْ تَقُولَ بِيَدَيْكَ هَكَذَا»، ثُمَّ ضَرَبَ بِيَدَيْهِ الْأَرْضَ ضَرْبَةً وَاحِدَةً، ثُمَّ مَسَحَ الشِّمَالَ عَلَى الْيَمِينِ، وَظَاهِرَ كَفَّيْهِ، وَوَجْهَهُ

Kutoka kwa Ammar bin Yasir, Mungu amuwiye radhi, amesema:

1- Mtume wa Mwenyezi Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) alinituma katika jukumu fulani, nikapatwa na janaba, lakini sikupata maji, nikajibiringisha katika mchanga kama mnyama, kisha nikaenda kwa Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake) nikamsimulia tukio hilo. 

2- Akasema: “hakika ilikuwa inatosha kufanya kwa mikono yako hivi” kisha akapiga ardhi kwa mikono yake mpigo mmoja, kisha akapangusa mkono wa kulia kwa mkono wa kushoto, na mkono wa kushoto kwa mkono wa kulia, na nje ya viganja vyake, na uso wake.

Vitendawili vya Qur'ani Vinavyohusiana

Enyi mlio amini! Mnapo simama kwa ajili ya Sala basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni. Na mkiwa na janaba basi ogeni. Na mkiwa wagonjwa au mmo safarini, au mmoja wenu ametoka chooni au mmewagusa wanawake, na hamkupata maji, basi tayamamuni vumbi lilio safi, na mpake nyuso zenu na mikono yenu. Hapendi Mwenyezi Mungu kukutieni katika taabu; bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema yake juu yenu ili mpate kushukuru.

[al maida: 6]

Miradi ya Hadithi