عن أبي هُريرة رضي الله عنه:أن رسول الله ﷺ دخل المسجد فدخَل رجلٌ، فصلَّى، فسلَّم على النبيِّ ﷺ، فرَدَّ وقال: «ارجِعْ فصَلِّ؛ فإنَّكَ لم تُصَلِّ»،فرجَعَ يُصَلِّي كما صَلَّى، ثم جاء، فسلَّمَ على النبيِّ ﷺ، فقال: «ارجِعْ فصَلِّ؛ فإنَّكَ لم تُصَلِّ» ثلاثًا، فقال: والذي بعَثَكَ بالحقِّ ما أُحسِنُ غَيرَه، فعَلِّمْني، فقال: «إذا قُمْتَ إلى الصلاةِ فكَبِّرْ،ثم اقرَأْ ما تَيسَّرَ معَكَ منَ القرآنِ، ثم اركَعْ حتى تَطمئِنَّ راكعًا، ثم ارفَعْ حتى تَعدِل قائمًا، ثم اسجُدْ حتى تَطمئِنَّ ساجِدًا، ثم ارفَعْ حتى تَطمئِنَّ جالسًا، وافعَلْ ذلك في صلاتِكَ كلِّها»

Kutoka kwa Abu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake  amesimulia kuwa:

1. siku moja Mtume aliingia Msikitini, akaingia mtu fulani akaswali, kisha akamsalimia Mtume Rehema na Amani zimshukie, akajibu salamu na kusema: “Rudi ukaswali kwani hukuswali.” 2. Akarudi akaswali vile alivyoswali mwanzoni, kisha akaja akamsalimia Mtume (saw), akasema: “Rudi ukaswali kwani hukuswali.” Mara tatu, akasema Mtu yule: “Naapa kwa yule aliyekutuma kwa haki, mimi sifahamu kufanya vizuri kuliko hivi, basi naomba unifundishe. 3. Akasema Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake) : “ukisimama kwa ajili ya Swala, basi toa takbira. 4. kisha soma aya nyepesi kwako katika Qur’ani . 5. Kisha rukuu mpaka utulizane katika rukuu, kisha inuka mpaka usimame sawasawa, kisha sujudu mpaka utulizane ukiwa umesujudu, kisha inuka mpaka utulie katika kikao, na ufanye hivyo katika Swala yako yote

Vitendawili vya Qur'ani Vinavyohusiana

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu

﴾ Basi ni kwa sababu ya rehema itokayo kwa Mwenyezi Mungu ndio umekuwa laini kwao. Na lau ungeli kuwa mkali, mwenye moyo mgumu, bila ya shaka wangeli kukimbia.﴿

[Al Imran: 159].

Amesema Mwenyezi Mungu mtukufu

﴾ Hakika amekwisha kujieni Mtume kutokana na nyinyi wenyewe; yanamhuzunisha yanayo kutaabisheni; anakuhangaikieni sana. Kwa Waumini ni mpole na mwenye huruma. 128﴿

[At-Tawbah: 128].

Amesema Mwenyezi Mungu mtukufu

﴾Na waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo.﴿

[Twaha: 132].

﴾ Waite waelekee kwenye Njia ya Mola wako Mlezi kwa hikima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora.﴿

[An-Nahl: 125].

Miradi ya Hadithi