عَنْ أَنَسِ بْن مَالِكٍ رضى الله عنه، أَنَّ النَّبِيَّ ﷺ قَالَ: «العَبْدُ إِذَا وُضِعَ فِي قَبْرِهِ، وَتَوَلَّى وَذَهَبَ أَصْحَابُهُ حَتَّى إِنَّهُ لَيَسْمَعُ قَرْعَ نِعَالِهِمْ، أَتَاهُ مَلَكَانِ، فَأَقْعَدَاهُ، فَيَقُولانِ لَهُ: مَا كُنْتَ تَقُولُ فِي هَذَا الرَّجُلِ مُحَمَّدٍ ﷺ؟ فَيَقُولُ: أَشْهَدُ أَنَّهُ عَبْدُ اللَّهِ وَرَسُولُهُ، فَيُقَالُ: انْظُرْ إِلَى مَقْعَدِكَ مِنَ النَّارِ أَبْدَلَكَ اللَّهُ بِهِ مَقْعَدًا مِنَ الجَنَّةِ، قَالَ النَّبِيُّ ﷺ: فَيَرَاهُمَا جَمِيعًا، وَأَمَّا الكَافِرُ - أَوِ المُنَافِقُ - فَيَقُولُ: لا أَدْرِي، كُنْتُ أَقُولُ مَا يَقُولُ النَّاسُ، فَيُقَالُ: لا دَرَيْتَ وَلا تَلَيْتَ، ثُمَّ يُضْرَبُ بِمِطْرَقَةٍ مِنْ حَدِيدٍ ضَرْبَةً بَيْنَ أُذُنَيْهِ، فَيَصِيحُ صَيْحَةً يَسْمَعُهَا مَنْ يَلِيهِ إِلَّا الثَّقَلَيْنِ». 

Kutoka kwa Anas bin Malik Mwenyezi Mungu awe radhi naye kwamba Mtume Rehma na Amani zimshukie amesema:

“Anapowekwa mja kaburini mwake na wakageuka na kuondoka Ndugu zake, na akasikia mchakato wa viatu vyao vikigonga.Watamuijia Malaika wawili, watamkalisha, na watamuuliza: Unasemaje kuhusu mtu huyu, yaani Muhammad Rehma na Amani zimshukie?Atasema Muumini: Nashuhudia kwamba yeye ni mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hapo ataambiwa: Tazama makazi yako ya motoni, Mwenyezi Mungu amekubadilishia kwa kukupa makazi mazuri peponi, akasema Mtume Rehma na Amani zimshukie: ataonyeshwa makazi yote mawili.Lakini kafiri - au mnafiki - atasema: Mimi sijui, nilikuwa nikisema yale waliyoyasema watu.Ataambiwa: Hukujua wala hukusoma.Kisha atapigwa nyundo ya chuma baina ya masikio yake, na atapiga ukelele utakaosikika kwa wanaomfuatia isipokuwa watu na majini.”

Muhtasari wa Maana

Mtume Rehma na Amani zimshukie ameeleza swali la Malaika wawili waliomo kaburini; Mja ataulizwa kuhusu Mtume wake, kama alikuwa ni Muumini, ataonyeshwa makazi yake peponi na kaburi lake litakuwa pana zaidi, na akiwa kafiri ataonyeshwa makazi yake Motoni, na atateswa kaburini mwake mpaka kusimama qiyama

Miradi ya Hadithi