عَنْ أَنَسِ بْن مَالِكٍ رضى الله عنه، أَنَّ النَّبِيَّ ﷺ قَالَ: «العَبْدُ إِذَا وُضِعَ فِي قَبْرِهِ، وَتَوَلَّى وَذَهَبَ أَصْحَابُهُ حَتَّى إِنَّهُ لَيَسْمَعُ قَرْعَ نِعَالِهِمْ، أَتَاهُ مَلَكَانِ، فَأَقْعَدَاهُ، فَيَقُولانِ لَهُ: مَا كُنْتَ تَقُولُ فِي هَذَا الرَّجُلِ مُحَمَّدٍ ﷺ؟ فَيَقُولُ: أَشْهَدُ أَنَّهُ عَبْدُ اللَّهِ وَرَسُولُهُ، فَيُقَالُ: انْظُرْ إِلَى مَقْعَدِكَ مِنَ النَّارِ أَبْدَلَكَ اللَّهُ بِهِ مَقْعَدًا مِنَ الجَنَّةِ، قَالَ النَّبِيُّ ﷺ: فَيَرَاهُمَا جَمِيعًا، وَأَمَّا الكَافِرُ - أَوِ المُنَافِقُ - فَيَقُولُ: لا أَدْرِي، كُنْتُ أَقُولُ مَا يَقُولُ النَّاسُ، فَيُقَالُ: لا دَرَيْتَ وَلا تَلَيْتَ، ثُمَّ يُضْرَبُ بِمِطْرَقَةٍ مِنْ حَدِيدٍ ضَرْبَةً بَيْنَ أُذُنَيْهِ، فَيَصِيحُ صَيْحَةً يَسْمَعُهَا مَنْ يَلِيهِ إِلَّا الثَّقَلَيْنِ». 

00:00
00:00
تحميل الملف الصوتي
00:00
00:00
تحميل الملف الصوتي

Kutoka kwa Anas bin Malik Mwenyezi Mungu awe radhi naye kwamba Mtume Rehma na Amani zimshukie amesema:

“Anapowekwa mja kaburini mwake na wakageuka na kuondoka Ndugu zake, na akasikia mchakato wa viatu vyao vikigonga.Watamuijia Malaika wawili, watamkalisha, na watamuuliza: Unasemaje kuhusu mtu huyu, yaani Muhammad Rehma na Amani zimshukie?Atasema Muumini: Nashuhudia kwamba yeye ni mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hapo ataambiwa: Tazama makazi yako ya motoni, Mwenyezi Mungu amekubadilishia kwa kukupa makazi mazuri peponi, akasema Mtume Rehma na Amani zimshukie: ataonyeshwa makazi yote mawili.Lakini kafiri - au mnafiki - atasema: Mimi sijui, nilikuwa nikisema yale waliyoyasema watu.Ataambiwa: Hukujua wala hukusoma.Kisha atapigwa nyundo ya chuma baina ya masikio yake, na atapiga ukelele utakaosikika kwa wanaomfuatia isipokuwa watu na majini.”

Vitendawili vya Qur'ani Vinavyohusiana

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

“Na anaye mpinga Mtume baada ya kumdhihirikia uwongofu, na akafuata njia isiyo kuwa ya Waumini, tutamuelekeza aliko elekea, na tutamuingiza katika Jahannamu. Na hayo ni mafikio mabaya”

[An-Nisa: 115].

Na Mwenyezi Mungu jina Lake Litukuzwe, akasema:

“Wanaonyeshwa Moto asubuhi na jioni. Na itapo fika Saa ya Kiyama patasemwa: Waingizeni watu wa Firauni katika adhabu kali kabisa”

[Ghafir: 46]

Miradi ya Hadithi