عَنْ أَنَسِ بْن مَالِكٍ رضى الله عنه، أَنَّ النَّبِيَّ ﷺ قَالَ: «العَبْدُ إِذَا وُضِعَ فِي قَبْرِهِ، وَتَوَلَّى وَذَهَبَ أَصْحَابُهُ حَتَّى إِنَّهُ لَيَسْمَعُ قَرْعَ نِعَالِهِمْ، أَتَاهُ مَلَكَانِ، فَأَقْعَدَاهُ، فَيَقُولانِ لَهُ: مَا كُنْتَ تَقُولُ فِي هَذَا الرَّجُلِ مُحَمَّدٍ ﷺ؟ فَيَقُولُ: أَشْهَدُ أَنَّهُ عَبْدُ اللَّهِ وَرَسُولُهُ، فَيُقَالُ: انْظُرْ إِلَى مَقْعَدِكَ مِنَ النَّارِ أَبْدَلَكَ اللَّهُ بِهِ مَقْعَدًا مِنَ الجَنَّةِ، قَالَ النَّبِيُّ ﷺ: فَيَرَاهُمَا جَمِيعًا، وَأَمَّا الكَافِرُ - أَوِ المُنَافِقُ - فَيَقُولُ: لا أَدْرِي، كُنْتُ أَقُولُ مَا يَقُولُ النَّاسُ، فَيُقَالُ: لا دَرَيْتَ وَلا تَلَيْتَ، ثُمَّ يُضْرَبُ بِمِطْرَقَةٍ مِنْ حَدِيدٍ ضَرْبَةً بَيْنَ أُذُنَيْهِ، فَيَصِيحُ صَيْحَةً يَسْمَعُهَا مَنْ يَلِيهِ إِلَّا الثَّقَلَيْنِ». 

Kutoka kwa Anas bin Malik Mwenyezi Mungu awe radhi naye kwamba Mtume Rehma na Amani zimshukie amesema:

“Anapowekwa mja kaburini mwake na wakageuka na kuondoka Ndugu zake, na akasikia mchakato wa viatu vyao vikigonga.Watamuijia Malaika wawili, watamkalisha, na watamuuliza: Unasemaje kuhusu mtu huyu, yaani Muhammad Rehma na Amani zimshukie?Atasema Muumini: Nashuhudia kwamba yeye ni mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hapo ataambiwa: Tazama makazi yako ya motoni, Mwenyezi Mungu amekubadilishia kwa kukupa makazi mazuri peponi, akasema Mtume Rehma na Amani zimshukie: ataonyeshwa makazi yote mawili.Lakini kafiri - au mnafiki - atasema: Mimi sijui, nilikuwa nikisema yale waliyoyasema watu.Ataambiwa: Hukujua wala hukusoma.Kisha atapigwa nyundo ya chuma baina ya masikio yake, na atapiga ukelele utakaosikika kwa wanaomfuatia isipokuwa watu na majini.”

Anas bin Malik bin Al-Nadr bin Damdam Al-Ansari

Anas bin Malik bin Al-Nadr bin Damdam Al-Ansari, Abu Hamza, imamu, mufti, msomaji, Mbobezi katika fani ya hadithi, msimuliaji wa Uislamu, Mtumishi wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, amani iwe juu yake, na wa mwisho kufa katika masahaba huko Basra. Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuja Madina akiwa na umri wa miaka kumi, na wakati Mtume anakufa Anasi alikuwa na umri wa miaka ishirini, na alikuwa akimtumikia Mtume, rehema na amani ziwe juu yake. Alishiriki vita pamoja na Mtume zaidi ya mara moja, na alimpa ahadi ya utii chini ya mti. Alipokea kutoka kwa Mtume elimu kubwa, Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake alimwombea dua ya mali nyingi na watoto, na shamba lake la mitende lilikuwa likipamba mara mbili kwa mwaka, alifariki mwaka: (93 AH) [1]


Marejeo

1.  Rejea ufafanuzi wake katika: “Sir Al-Alam Al-Nubala” cha Al-Dhahabi (4/417-423), “Ma`rifat Al-Sahaba” cha Abu Naim (1/231), “Kamusi ya Maswahaba. ” cha Al-Baghawi (1/43), “Asad Al-Ghaba” cha Ibn Al-Atheer (1/ 151-153).

Miradi ya Hadithi