117 - FADHILA ZA KUSOMA NA KUSOMESHA QURÀNI

عَنْ أبي عبد الرحمن السُّلَمِيِّ، عن عثمانَ بنِ عفَّانَ رضي الله عنه، عن النبيِّ ﷺ قال: «خَيْرُكُمْ مَنْ تَعَلَّمَ القُرْآنَ وَعَلَّمَهُ».  

وفي رواية: «إِنَّ أَفْضَلَكُمْ مَنْ تَعَلَّمَ القُرْآنَ وَعَلَّمَهُ»

Kutoka kwa Abu Abd al-Rahman al-Sulamiy, kutoka kwa Uthman bin Affan, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kutoka kwa Mtume, rehema na amani ziwe juu yake amesema:

1. “Mbora wenu ni yule mwenye kujifunza na kufundisha Qur’an”.

2. Na Abu Abd al-Rahman alisoma zama za utawala wa Uthman, mpaka alipokuwa haji. 

3. Akasema: Na Jambo hili la kusomesha ndio limenifanya nikae kitako hapa.  

Muhtasari wa Maana

Amesema Mtume Rehma na amani ziwe juu yake kuwa watu bora zaidi ni wale wanaojifunza Qur’an kwa kuhifadhi, kusoma, kuitafsir na mambo mengine, kisha kuwafundisha watu.

Miradi ya Hadithi