عَنْ طَلْحَةَ بْنِ عُبَيْدِ اللهِ رضي الله عنه قَالَ:جَاءَ رَجُلٌ إِلَى رَسُولِ اللهِ مِنْ أَهْلِ نَجْدٍ، ثَائِرُ الرَّأْسِ، يُسْمَعُ دَوِيُّ صَوْتِهِ، وَلَا يُفْقَهُ مَا يَقُولُ، حتَّى دَنَا، فَإِذَا هُوَ يَسْأَلُ عَنِ الإِسْلامِ،فَقَالَ رَسُولُ اللهِ : «خَمْسُ صَلَوَاتٍ فِي اليوْمِ وَاللَّيْلَةِ»، فَقَالَ: هَلْ عَليَّ غَيْرُهَا؟ قَالَ: «لَا، إِلَّا أَنْ تَطَّوَّعَ».قَالَ رَسُولُ اللهِ : «وَصِيَامُ رَمَضَانَ»، قَالَ: هَلْ عَليَّ غَيْرُهُ؟ قَالَ: «لَا، إِلَّا أَنْ تَطَّوَّعَ».قَالَ: وَذَكَرَ لَهُ رَسُولُ اللهِ الزَّكَاةَ، قَالَ: هَلْ عَليَّ غَيْرُهَا؟ قَالَ: «لَا، إِلَّا أَنْ تَطَّوَّعَ».قَالَ: فَأَدْبَرَ الرَّجُلُ وَهُوَ يَقُولُ: وَاللهِ، لَا أَزِيدُ عَلَى هَذَا وَلا أَنْقُصُ. قَالَ رَسُولُ اللهِ : «أَفْلَحَ إِنْ صَدَقَ». وفي رِوايةٍ: «دَخَلَ الجَنَّةَ إِنْ صَدَقَ»

Kutoka kwa Talha bin Ubaydillah Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yakeamesema:

  1- Alikuja mtu mmoja katika watu wa Najd kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehema na amani ziwe juu yake), Sauti yake inasikika, lakini haeleweki anachosema, mpaka akakaribia, kumbe anauliza kuhusu Uislamu  2- Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehema na amani ziwe juu yake): "Swala tano kwa mchana na usiku", akasema: Je, ni lazima nifanye jambo lingine? Akasema: “Hapana, isipokuwa ukijitolea”.  

3- Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehema na amani ziwe juu yake): "Na Saumu ya Ramadhani", akasema: Je, ni lazima nifanye jambo lingine? akasema: “Hapana, isipokuwa ukijitolea”.  

4- (Talha bin Ubaydillah ) Akasema: Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehema na amani ziwe juu yake), akamtajia Zaka, akasema: Je, ni lazima nifanye jambo lingine? akasema: Hapana, isipokuwa ukijitolea.  

5- (Talha bin Ubaydillah ) Akasema: Basi yule mtu akageuka na kusema: Wallahi siwezi kuongeza wala kupunguza katika haya.  

6- Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehema na amani ziwe juu yake): "Atafaulu ikiwa ni mkweli." Na katika riwaya nyingine: “Ataingia Peponi ikiwa anasema kweli. 

Muhtasari wa Maana

Bedui mmoja alimuuliza Mtume (Rehema na amani ziwe juu yake), kuhusu Uislamu, alimwambia kuhusu nguzo zake zinazojulikana sana, atakayezitekeleza ipasavyo, bila ya kuongeza wala kupunguza, basi atafaulu na kuingia Peponi. 

Miradi ya Hadithi