عن أبي هُريرةَ رضي الله عنه، قال: قال رسولُ الله ﷺ: «أيُّها الناسُ، إن اللهَ طيِّبٌ لا يَقبَل إلا طَيِّبًا،وإن اللهَ أمَر المؤمنين بما أمر به المرسَلين، فقال: {يَا أَيُّهَا الرُّسُلُ كُلُوا مِنَ الطَّيِّبَاتِ وَاعْمَلُوا صَالِحًا} [المؤمنون: 51]، وقال: {يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُلُوا مِنْ طَيِّبَاتِ مَا رَزَقْنَاكُمْ} [البقرة: 172]، ثم ذكَر الرجُل يُطِيل السَّفَرَ أَشْعَثَ أَغْبَرَ، يَمُدُّ يَدَيْهِ إلى السماء: يا ربِّ، يا ربِّ، ومطعمُه حرامٌ، ومشرَبُه حرامٌ، ومَلبسُه حرامٌ، وغُذِيَ بالحرام، فأنَّى يُستجاب لذلك؟!»

Kutoka kwa Abu Hurayra Mwenyezi Mungu awe radhi naye amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie amesema:

“Enyi watu, Mwenyezi Mungu ni mzuri na hapokei ila kizuri. Na Mwenyezi Mungu amewaamrisha Waumini yale aliyo waamrisha Mitume, akasema: “Enyi Mitume kuleni vyakula bora na mtende mema” [Al-Muuminun: 51], na akasema: “Enyi mlio amini kuleni vyakula bora tulivyo kupeni katika riziki” [Al-Baqara: 172] 3- Kisha Mtume akamtaja alie safari safari ndefu iliyechafuka na vumbi, akinyoosha mikono yake mbinguni: Ewe Mola Mlezi, Mola Mlezi, na chakula chake ni haramu, na kinywaji chake ni haramu, na nguo yake ni haramu, Alilishwa vitu vilivyoharamishwa, ni vipi atajibiwa?!”

Muhtasari wa Maana

Mtume amani iwe juu yake anatuambia kuwa Mwenyezi Mungu ni mwema na hakubali chochote isipokuwa kizuri, na ndio maana akawaamrisha watu wote kula katika vitu vizuri, na akasema kwamba kula katika haramu ni moja ya vikwazo vinavyozuia dua kujibiwa.

Miradi ya Hadithi