41 - KUJIEPUSHA NA KURTADI, UKAFIRI, NA SHIRKI KUBWA

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه أَنَّ رَسُولَ اللهِ قَالَ: «بَادِرُوا بِالْأَعْمَالِ فِتَنًا كَقِطَعِ اللَّيْلِ الْمُظْلِمِ، يُصْبِحُ الرَّجُلُ مُؤْمِنًا وَيُمْسِي كَافِرًا، أَوْ يُمْسِي مُؤْمِنًا وَيُصْبِحُ كَافِرًا، يَبِيعُ دِينَهُ بِعَرَضٍ مِنَ الدُّنْيَا» 

Kutoka kwa Abuu Hurairah, hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na

Amani ziwe juu yake) amesema: “Jitahidini kufanya matendo mema, kwa sabubu kuna fitina kama kiza cha usiku totoro, Mtu anaamka akiwa ni muumini, jioni anakuwa kafiri, au jioni anakuwa ni muumini, asubuhi kafiri, Anaiuza dini yake kwa mapambo ya Dunia.


Muhtasari wa Maana

Mtume (Rehma na Amani ziwe juu yake) anawaelekeza maswahaba wajitahidi kutenda mema kabla fitina ambayo inampoteza mtu na kushusha Imani haijaenea. Ndani ya muda mfupi mtu anakuwa kafiri na Imani ilikuwa imekita katika moyo wake

Miradi ya Hadithi