عن أبي هريرةرضي الله عنه أن رسول الله ﷺ قال: «أَحَبُّ الْبِلَادِ إِلَى اللهِ مَسَاجِدُهَا،وَأَبْغَضُ الْبِلَادِ إِلَى اللهِ أَسْوَاقُهَا»

Kutoka kwa Abu Hurayrah Mwenyezi Mungu awe radhi naye kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na Amani zimshukie amesema:

“Nyumba zinazopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu ni misikiti yake. Maeneo yanayochukiwa zaidi na Mwenyezi Mungu ni Masoko ’’.

Vitendawili vya Qur'ani Vinavyohusiana


Amesema Mola mlezi na mtukufu:

“Sema: Mola Mlezi wangu ameamrisha uadilifu, na mumuelekeze nyuso zenu kila mnapo sujudu, na muombeni Yeye kwa kumsafia Dini. Kama alivyo kuumbeni mwanzo ndivyo mtavyo rudi”

[Al-A'raf: 29].

Mwenyezi Mungu mtukufu amesema:

“Hakika wanao amirisha misikiti ya Mwenyezi Mungu ni wale wanao muamini Mwenyezi Mungu, na Siku ya Mwisho, na wakashika Sala, na wakatoa Zaka, na wala hawamchi ila Mwenyezi Mungu. Basi huenda hao wakawa katika waongofu”

[At-Tawbah: 18].

Na akasema aliyetukuka:

“Katika Nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameamrisha zitukuzwe, na humo litajwe jina lake, wanamtakasa humo asubuhi na jioni (36) Watu ambao biashara wala kuuza hakuwashughulishi na kumdhukuru Mwenyezi Mungu, na kushika Sala, na kutoa Zaka. Wanaikhofu Siku ambayo nyoyo na macho yatageuka (37) Ili Mwenyezi Mungu awalipe bora ya waliyo yatenda, na awazidishie katika fadhila zake. Na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu”

[An-Nur: 36-38].

Miradi ya Hadithi