عن أبي هريرةرضي الله عنه أن رسول الله ﷺ قال: «أَحَبُّ الْبِلَادِ إِلَى اللهِ مَسَاجِدُهَا،وَأَبْغَضُ الْبِلَادِ إِلَى اللهِ أَسْوَاقُهَا»

Kutoka kwa Abu Hurayrah Mwenyezi Mungu awe radhi naye kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na Amani zimshukie amesema:

“Nyumba zinazopendwa zaidi na Mwenyezi Mungu ni misikiti yake. Maeneo yanayochukiwa zaidi na Mwenyezi Mungu ni Masoko ’’.

Muhtasari wa Maana

Mtume Rehma na Amani ziwe juu yake anaeleza kuwa sehemu anayoipenda zaidi Mwenyezi Mungu Mtukufu ni misikiti; Ndipo mahali pa kumtaja na kumuabudu, na sehemu anazozichukia zaidi ni masoko. Ambapo vimejaa viapo vya uwongo, na ulaghai, dhuluma na udanganyifu.

Miradi ya Hadithi