عن أبي هُرَيرة رضي الله عنه، قال: خطَبَنا رسولُ الله ﷺ، فقال: «أيُّها الناسُ، قد فرَضَ اللهُ عليكم الحجَّ؛ فحُجُّوا»، فقال رجُلٌ: أكلَّ عامٍ يا رسولَ الله؟ فسكَتَ حتى قالها ثلاثًا، فقال رسول الله ﷺ: «لو قلتُ: نَعمْ، لوجَبتْ، ولَمَا استطعتم». ثم قال: «ذَروني ما تركتُكم؛ فإنما هلَك مَن كان قبلَكم بكثرة سؤالهم، واختلافهم على أنبيائهم، فإذا أمرتُكم بشيءٍ فأْتوا منه ما استطعتم، وإذا نَهيتكم عن شيء فدَعوه»


Kutoka kwa Abu Hurairah Mwenyezi Mungu awe radhi naye ambaye amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu Amani iwe juu yake alituhutubia na kusema: “Enyi watu, Mwenyezi Mungu amekufaradhisheni Hija; nendeni mkahiji, Akasema mtu mmoja : Je ni kila mwaka ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Alinyamaza hadi akasema mara tatu. Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na Amani zimshukie: “Lau ningesema: Ndio, ingeli kuwa ni wajibu, na msingeliweza. Kisha akasema: Niachieni katika yale ambayo sikukuambieni. Waliangamia walio kuwa kabla yenu kwa sababu ya wingi wa maswali  na kutofautiana kwao na Manabii wao .. Basi nikikuamrisheni kufanya jambo, basi lifanyeni kadiri muwezavyo, na nikikukatazeni, basi liacheni.” 

Abd al-Rahman ibn Sakhr al-Dawsi, al-Azdi, al-Yamani

hadithi mia nane zilipokewa kutoka kwake –kati ya masahaba na matabiiy. Umar bin Al-Khattab alimtumia kama gavana wa Bahrain, kisha akarudi na kuishi Madina na alikuwa ameshughulika na kusimulia hadithi na kuwafundisha watu kuhusu dini yao, na alikufa Madina mwaka wa (58 AH) [1]

Marejeo

  1. Rejea ufafanuzi wake katika : “Maarifaat al-Sahaba” cha Abu Nu’aym (4/1846), “Aliastieab Fi Maerifat Al'as-habi" cha Ibn Abd al-Bar (4/1770), “Asad al-Ghaba” cha Ibn al. -Atheer (3/357), “Al-Isbah fi Tamyiz al-Swahaba” cha Ibn hajar Asqalani (4/267).



Miradi ya Hadithi