عن ابنِ عمرَ رضي الله عنهما، أن رسول الله  ﷺ قال: «صلاةُ الجماعةِ أفضَلُ من صلاةِ الفَذِّ بسَبعٍ وعشرينَ دَرجةً»

Kutoka kwa Ibn Umar, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie, amesema:

“Swala ya jamaa ni bora zaidi kuliko swala ya mtu pekee kwa daraja ishirini na saba.’’

Muhtasari wa Maana

Mtume Rehma na Amani zimshukie anafahamisha kuwa swala ya jamaa ni bora kuliko swala ya mtu peke yake kwa daraja ishirini na saba.

Miradi ya Hadithi