عَنْ أَنَسٍ رضي الله عنه، عَنِ النَّبِيِّ قَالَ: «لا يُؤْمِنُ أَحَدُكُمْ حَتَّى يُحِبَّ لأَخِيهِ مَا يُحِبُّ لِنَفْسِهِ»

Kutoka kwa Anas, kutoka kwa Mtume rehma na amani zimshukie amesema:

“Hatokuwa na imani yeyote miongoni mwenu mpaka ampendelee nduguye kile anachojipendelea” 



Uislamu ulitia mapenzi katika nyoyo za waumini, wakawa ni ndugu wenye mapenzi, baadhi yao wanafurahia anapofurahi ndugu yao, na wanahuzunika kwa maumivu ya ndugu yao, kama alivyosema Mtume rehma na Amani zimshukie "Unawaona waaminio katika huruma yao, upendo na huruma, kama mwili mmoja , kiungo kimoja kikipata maumivu, Mwili wake wote unapatwa na kukosa usingizi na homa” [1].

Na Mtume rehma na Amani zimshukie ameeleza kuwa imani ya mja haikamiliki mpaka ampendelee nduguye utiifu na kheri anayoipendelea nafsi yake. Akipata mlango wa kheri huwaongoa ndugu zake, na ikiwa ndugu yake ana dhulma dhidi yake, huharakisha kumfanyia uadilifu nduguye kuliko nafsi yake na kumpa haki yake.

Maana ya Hadithi sio kwamba mtu aondoshe wema wa mapenzi yake kwa nafsi yake. Hakuna anayeweza kufanya hivyo, bali kinachokusudiwa ni kumtakia mema ndugu yake bila ya kumuumiza, na hilo ni rahisi kwa moyo wenye afya njema [2] 

Hii haimaanishi kuwa Muislamu asishindane katika kufikia viwango vya juu; Abu Bakr na Umar, Mungu awe radhi nao wote wawili, walikuwa wakishindana kwa ajili ya milango ya wema, na huu haukuwa upungufu katika imani yao. Kinachotakiwa ni kutakiana mema kwa ujumla, na kuepukana na maovu kwa ujumla. Ama mtu kutafuta fadhila za juu na ubora wa hali ya juu, hakuna ubaya kwa mtu kujitanguliza kuliko wengine [3]

Wanachuoni walipendezwa sana na Hadithi hii, hadi wakasema: Dini nzima imeegemezwa kwenye Hadithi nne, hii ni mojawapo. Hivyo hadithi hii ni robo ya Uislamu [4]


1. Kuwatakia kheri Waislamu ni sifa inayompeleka mhusika wa sifa hiyo katika viwango vya juu vya ukamilifu wa kimaadili. Ambapo anajinyanyua mwenyewe kutoka katika husuda, uovu, uchoyo, kinyongo na kiburi. Tunaomba Mwenyezi Mungu atubariki kwayo.

2. Kinachotakiwa kwa Muislamu ni kumpendelea kheri nduguye. Iwapo anajipendelea sifa ya dini au mali au mfano wa hayo basi aipendelee sifa iwe kwa rafiki yake. Ndio maana Ibn Abbas, Mwenyezi Mungu awe radhi nao wote wawili, walikuwa wakisema: “Hakika mimi nasoma aya katika Qur’ani na ninaielewa; halafu napenda watu wote waifahamu kama nilivyo ifahamu." [5]

3. Ni lazima kwa kila Muislamu kuitafuta tabia hii. Na ni kuwatakia wema ndugu zake Waislamu, mwenye kukosa sifa hii basi anaupungufu wa imani.

4. Muumini anajiweka katika nafasi ya nduguye Muislamu. Akifurahishwa na jambo basi analitamani kwa nduguye, na kama akichukia jambo basi hapendi limfike nduguye. Al-Ahnaf bin Qais, Mwenyezi Mungu amrehemu, amesema: “nilikuwa nikichukia jambo alilonifanyia mtu, basi nami simfanyii yeyote. [6]

5. Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwasifu Ansari katika Kitabu chake kitukufu walipowapendelea ndugu zao wahajiri kuliko nafsi zao, kwa hivyo wakagawana fedha zao kati yao, kiasi kwamba Saad bin Al-Rabiy Mwenyezi Mungu awe radhi naye akamgawia ndugu yake Abd al-Rahman bin Awf mali zake kwa usawa, na kumtaliki mmoja katika wake zake wawili ili aolewe baada ya eda yake [7]. Abd al-Rahman ibn Awf hakuwa na kiwango kidogo cha kumfadhilisha mtu kuliko ndugu yake Saad ibn al-Rabia. Na ndio maana Hakukubali kuchukua nusu ya mali zake au kumpa talaka mkewe kwa ajili yake, ati kutokana na umaskini uliompata; kwakuwa alimwachia Mwenyezi Mungu mali zake na nyumba yake na kila kitu, lakini alimshukuru ndugu yake Saad na kwenda sokoni kutafuta riziki yake kwa juhudi zake.

6. Mlinganiaji na Mlezi wawe makini katika kuboresha na kuimarisha mahusiano ya kijamii baina ya Waislamu.

7. Kuwapendelea kheri watu hakuzuwii kufanya ushindani nao katika nyumba ya dunia na akhera. Kuwatakia kheri na kufurahia mafanikio yao inatosha.

8. Mwanafunzi Muumini anawatakia ndugu zake wote mafanikio, na hakuna ubaya kuwa na hamu ya kuwa wa kwanza katika kundi lake, na vile vile mfanyabiashara anawatakia kheri wafanyabiashara wote, na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu atawapa riziki njema. Hili halimzuii kutamani mali nyingi, na hali kadhalika kwa daktari, mhandisi, mfanyakazi, na wengineo.

9.Mshairi akasema:

Ndugu yako ni ambaye anakulinda kwa bidii wakati haupo = na anayaficha maovu na mabaya yako. Na huyatangaza waziwazi yale yanayokupendeza, wala hadharau wema wala nasaha.


Marejeo


1. Imepokewa na Al-Bukhari (6011) na Muslim (2586).

2. “Al-Minhaj Sharh Sahih Muslim bin Al-Hajjaj” cha Al-Nawawi (2/ 17). Tazama: “Lisan al-Arab” cha Ibn Manzur (11/244).

3. "Kashf Almushkil Min Hadith Alshyhyni"  (3/232).

4. Tazama: “Al-Minhaj Sharh Sahih Muslim bin Al-Hajjaj” cha Al-Nawawi (11/27).

5. Imepokewa na al-Tabarani (10621).

6. sherh Sahih Al-Bukhari cha Ibn Battal (1/65).

7. Imepokewa na Al-Bukhari (2049) na Muslim (1427).


Miradi ya Hadithi