عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه : أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ قَالَ: «إِنَّ لِلَّهِ تِسْعَةً وَتِسْعِينَ اسْمًا؛ مِائَةً إِلَّا وَاحِدًا، مَنْ أَحْصَاهَا دَخَلَ الجَنَّةَ»، زَادَ في رواية: «إِنَّهُ وِتْرٌ يُحِبُّ الْوِتْرَ». متفق عليه

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) Amesema:

Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake:Hakika Mwenyezi Mungu ana majina tisini na tisa.mia moja ispokuwa moja,Mwenye kuyadhibiti ataingia Peponi.”Akaongeza katika riwaya nyingine: “hakika yeye (Mwenyezi Mungu) ni witiri anapenda witiri.”

imepokelewa na Bukhari Na Muslim

Muhtasari wa Maana

Mtume (rehema na amani ziwe juu yake) anaeleza kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ana Majina Mazuri tisini na tisa, yeyote atakayeyadhibiti kwa kufanya yanayoyahitajika; kama kujifunza maana yake, na akayafanyia kazi, ataingia Peponi.

Miradi ya Hadithi