عن أبي هريرة رضي الله عنه، عن النبيِّﷺ قال:«مَن صلَّى صلاةً لم يَقرَأْ فيها بأُمِّ القُرآنِ فهي خِدَاجٌ – ثلاثًا - غيرُ تَمامٍ»،فقيلَ لأبي هُرَيْرةَ: إنَّا نكونُ وراءَ الإمامِ؟ فقال: اقرَأْ بها في نَفْسِكَ؛فإنِّي سَمِعْتُ رسولَ اللهِ ﷺ يقولُ: «قال اللهُ تعالى: قَسَمْتُ الصلاةَ بَيْني وبينَ عَبْدي نِصفَيْنِ، ولعَبْدي ما سألَ،فإذا قال العبدُ: {الْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ} [الفاتحة: 2]، قال الله تعالى: حَمِدني عبدي، وإذا قال: {الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ} [الفاتحة: 3]، قال الله تعالى: أثنى عليَّ عبدي، وإذا قال: {مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ} [الفاتحة: 4]، قال: مجَّدني عبدي،فإذا قال: {إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ} [الفاتحة: 5]، قال: هذا بيني وبين عبدي، ولعَبْدي ما سَألَ،فإذا قال: {اهْدِنَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ (6) صِرَاطَ الَّذِينَ أَنْعَمْتَ عَلَيْهِمْ غَيْرِ الْمَغْضُوبِ عَلَيْهِمْ وَلَا الضَّالِّينَ} [الفاتحة: 6، 7]، قال: هذا لِعَبْدي، ولِعَبْدي ما سَألَ»


Kutoka kwa Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amfikishie rehema na amani, kutoka kwa Mtume, Mwenyezi Mungu amfikishie rehema na amani, amesema:

1. “Mwenye kuswali swala ambayo hakusoma ndani yake Mama wa Qur’an, basi swala hiyo haijatimia, kayasema maneno haya mara tatu. 2. Akaambiwa Abu Hurayrah: Hakika sisi tunakuwa nyuma ya imamu? Akasema: Isomee moyoni mwako. 3. Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Amesema Mwenyezi Mungu: Nimeigawanya Swala baina yangu na mja Wangu vipande viwili, na mja wangu atapata alichoomba. 4. Iwapo mja atasema: “Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote” [Al-Fatihah: 2], basi Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: Mja wangu amenisifu, na ikiwa atasema: “Mwingi wa kurehemu, Mwenye kurehemu.” [Al-Fatihah: 3], Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “Amenisifu.” Akisema mja wangu "Mmiliki wa Siku ya Kiyama} [Al-Fatihah: 4] Anasema Mwenyezi Mungu:Mja wangu amenitukuza. 5. Akisema: “Wewe tunakuabudu na Wewe tunakuomba msaada” [Al-Fatihah: 5], Anasema: Haya ni baina Yangu na mja Wangu, na mja Wangu atapata analoliomba. 6. Akisema: “Tuongoze kwenye njia iliyonyooka (6), njia ya wale uliowaneemesha, si ya wale ambao wamewaghadhibikiwa, wala waliopotea. Mwenyezi mungu husema: Hili ni la mja wangu na atapata mja wangu kile alicho kiomba”

Muhtasari wa Maana

Abu Huraira, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, anasimulia kuwa Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, amesema kuwa mwenye kuswali swala ambayo hakusoma al-Fatiha, ina upungufu, upungufu unaoathiri usahihi wake. Akaulizwa Abu hurayra kuhusu kuisoma alfatiha nyuma ya imamu katika swala ya jamaa: akasema isomwe kwa utukufu wa hadithi ya Mtume kutoka kwa Mola wake kwamba ameigawa alfatiha baina yake na mja wake.

Miradi ya Hadithi