108 - MGAWANYIKO WA WATU KATIKA WAHYI (UFUNUO)

عن أبي موسى الأشعريِّ، عن النبيِّ ﷺ قال:«مَثَلُ ما بعَثَني اللهُ به من الهُدى والعِلم، كمَثَل الغَيث الكثيرِ أصاب أرضًا: فكان منها نَقِيَّةٌ، قبِلَت الماءَ، فأنبتَت الكَلَأَ والعُشبَ الكثير، وكانت منها أجادبُ، أمسكت الماءَ، فنفعَ اللهُ بها الناسَ، فشَرِبوا وسَقَوْا وزرعوا، وأصابت منها طائفةٌ أخرى، إنما هي قِيعانٌ لا تُمسِك ماءً ولا تُنبتُ كلأً، فذلك مثَلُ مَن فَقُه في دِين الله، ونفَعه ما بعَثَني الله به فعَلِم وعَلَّم، ومَثلُ مَن لم يرفَعْ بذلك رأسًا، ولم يَقبَلْ هُدى الله الذي أُرسِلْتُ به» متفق عليه.

Kutoka kwa Abuu Mussa Al-Ash-Ariyy (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema,

1. Mfano wa aliyonituma kwayo Allah (s.w) miongoni mwa uongofu na elimu, ni kama mfano wa mvua nyingi iliyonyesha katika Ardhi Fulani, 

2. Ikawa Ardhi hiyo ni safi ikapokea maji na kuotesha mazao na mimea. 

3. Na ikawa sehemu nyingine ni kavu ikapokea maji, na Mwenyezi Mungu akawanufaisha watu kwa mvua hiyo wakanywa na wakanywesheleza mifugo na wakalima mazao. 

4. Na ikanyesha sehemu nyingine ya ardhi, hakika sehemuhiyo ni jangwa halihifadhi maji na wala halioteshi mimea  

5. Basi huo ni mfano  wa mtu aliopewa utambuzi katika dini na mwenyezimungu akamnufaisha na yale aliyonitumanayo kwayo, akayatambua na akawaelimisha watu wengine,na mfano wa Yule ambaye  hakuyapa kipaumbele wala hakukubali mwongozo wa mwenyezimungu ambao nimetumwa kwao.(Imepokelewa na Imam Bukhari na Muslimu).

Abuu Muusaa Abdullahi Ibn Qays

Ni Abuu Muusaa Abdullahi Ibn Qays Ibn Sulaym Ibn Hudhdhwaari Ibn Harbi Ibn A’mir Ibn Ash-Ar Al-Ash-Ariy, kiongozi mkubwa, mwana fiqhi,(msomi wa sheria ya dini),swahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake, mwenye kuhama mara mbili: ku-hamia habeshi na kuhamia madina(mji wa Mtume) alikua kiongozi katika mji wa basra katika ukhalifa wa Umaru Ibn Al-Khatwab (R. A) akawafundisha watu wa basra na akawapatia utambuzi juu ya dini yao, na akawasomesha qur’ani tukufu (kitabu cha Allah) na alikua ni bora sana katika maswahaba wa Mtume (s.a.w) kwa sauti ya kuiso-ma qur’ani tukufu.Alikufa mwaka (50:h)(1).

Marejeo

  1. 1 Rejea tafsiri yake katika: “Maarifaat al-Sahaba cha Abu Naim” (4/ 1749), “Kuna-sibishwa katika kuwajua Maswahaba kwa Ibn Abd al-Bar” (4/ 1762), “Asad al-Ghaba cha Ibn al. -Atheer” (5/306).


Miradi ya Hadithi