عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه، عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: (سَبْعَةٌ يُظِلُّهُمُ اللهُ فِي ظِلِّهِ يَوْمَ لَا ظِلَّ إلَّا ظِلُّهُ: الْإِمَامُ الْعَادِلُ، وَشَابٌّ نَشَأَ بِعِبَادَةِ اللهِ عز وجل، وَرَجُلٌ قَلْبُهُ مُعَلَّقٌ فِي الْمَسَاجِدِ، وَرَجُلَانِ تَحَابَّا فِي اللهِ؛ اجْتَمَعَا عَلَيْهِ، وَتَفَرَّقَا عَلَيْهِ، وَرَجُلٌ دَعَتْهُ امْرَأَةٌ ذَاتُ مَنْصِبٍ وَجَمَالٍ، فَقَالَ: إِنِّي أَخَافُ اللهَ، وَرَجُلٌ تَصَدَّقَ بِصَدَقَةٍ، فَأَخْفَاهَا حَتَّى لَا تَعْلَمَ يَمِينُهُ مَا تُنْفِقُ شِمَالُهُ، وَرَجُلٌ ذَكَرَ اللهَ خَالِيًا فَفَاضَتْ عَيْنَاهُ.

Kwa kutoka kwa Abu Hurairah Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kutoka kwa Mtume Swalla Allaahu alayhi wa sallam amesema: 1- “Watu aina saba Mwenyezi Mungu atawatia kwenye kivuli chake siku ambayo hakuna kivuli ila chake. 2- Imamu Muadilifu 3- Kijana aliyekulia katika ibada ya Mwenyezi Mungu. 4- Mtu ambaye moyo wake umefungamana na misikiti. 5- Watu wawili waliopendana kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. wakakusanyika kwa ajili yake na kutawanyika kwa ajili yake. 6- Mwanaume aliyekaribishwa na mwanamke mwenye cheo na mrembo, akasema: Mimi namuogopa Mwenyezi Mungu. 7- Mtu aliyetoa sadaka na akaificha mpaka mkono wake wa kushoto usijue mkono wake wa kulia unatoa nini. 8- Na mtu aliye mtaja Mwenyezi Mungu kwa siri, mpaka akalia”.


Abd al-Rahman ibn Sakhr al-Dawsi

MSIMULIZI: Ni: Abd al-Rahman ibn Sakhr al-Dawsi, al-Azdi, al-Yamani, anayejulikana sana kwa lakabu yake, “lakabu ni jina la kupewa tu kwa utani” na hili ndio jina mashuhuri zaidi ya majina yote yaliyosemwa juu yake na jina la baba yake. Ni sahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amanizimshukie. Alikuwa akienda naye popote aendapo, na alikuwa miongoni mwa masahaba walio hifadhi na kusimulia hadithi nyingi sana kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma na Amani ziwe juu yake, “kama alivyosema Al-Bukhari, Zaidi ya hadithi mia nane zilipokewa kutoka kwake –kati ya masahaba na matabiiy. Umar bin Al-Khattab aliMtumia kama gavana wa Bahrain, kisha akarudi na kuishi Madina na alikuwa ameshughulika na kusimulia hadithi na kuwafundisha watu kuhusu dini yao, na alikufa Madina mwaka wa (58 AH) [1]

Marejeo

  1. Rejea historia yake katika vitabu vifuatavyo: “Maarifaat al-Sahaba” na Abu Nu’aym (4/1846), “Alastieab Fi Maerifat Al'ashabi” na Ibn Abd al-Bar (4/1770), “Asad al-Ghaba” na Ibn al-Atheer (3/357), “Al-Isbah fi Tamazu al-Sahaba” cha Ibn Hajar al-Asqalani (4/267).


Miradi ya Hadithi