عن أبي يحيى صهيب بن سنان قال: قال رسول الله ﷺ: «عَجَبًا لأَمْرِ المُؤْمِنِ، إنَّ أمْرَهُ كُلَّهُ خَيْرٌ، وليسَ ذاكَ لأَحَدٍ إلَّا لِلْمُؤْمِنِ، إنْ أصابَتْهُ سَرَّاءُ شَكَرَ، فَكانَ خَيْرًا له، وإنْ أصابَتْهُ ضَرَّاءُ، صَبَرَ فَكانَ خَيْرًا له».

00:00
00:00
تحميل الملف الصوتي
00:00
00:00
تحميل الملف الصوتي

Kutoka kwa Abu Yahya Suhaib bin Sinan, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehma na amani zimshukie.

1- “Ni la kustaajabisha jambo la Muumini, kwani mambo yake yote ni kheri, na hayo si ya kila mtu isipokuwa kwa Muumini peke yake. 

 2- Ikimpata kheri hushukuru, na inakuwa ni kheri kwake. 

3- Na yakimpata matatizo husubiri, na inakuwa ni kheri kwake.” .

Vitendawili vya Qur'ani Vinavyohusiana

Amesema Mwenyezi Mungu mtukufu: “Hapana shaka tutakujaribuni kwa chembe ya khofu, na njaa, na upungufu wa mali na watu na matunda. Na wabashirie wanao subiri (55) Wale ambao ukiwasibu msiba husema: Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea (156) Hao juu yao zitakuwa baraka zitokazo kwa Mola wao Mlezi na rehema. Nao ndio wenye kuongoka” .

[Al-Baqara: 155-157]

Na akasema Allah mtukufu: “Na tulimtuma Musa pamoja na miujiza yetu, tukamwambia: Watoe watu wako kwenye giza uwapeleke kwenye mwangaza. Na uwakumbushe siku za Mwenyezi Mungu. Hakika katika hayo zipo ishara kwa kila mwenye kusubiri akashukuru” .

[Ibrahim: 5]

Pia Allah Mtukufu akasema: “Na alipo tangaza Mola wenu Mlezi: Mkishukuru nitakuzidishieni; na mkikufuru, basi adhabu yangu ni kali” .

[Ibrahim: 7]

Miradi ya Hadithi