عَنْ أَنَسٍ رضى الله عنه، قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ «مَا بُعِثَ نَبِيٌّ إِلَّا أَنْذَرَ أُمَّتَهُ الأعْوَرَ الكَذَّابَ، أَلا إِنَّهُ أَعْوَرُ، وَإِنَّ رَبَّكُمْ لَيْسَ بِأَعْوَرَ، وَإِنَّ بَيْنَ عَيْنَيْهِ مَكْتُوبٌ "كَافِرٌ" 

Kutoka kwa Anas Mwenyezi Mungu awe eradhi naye amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani zimshukie:

“Hakutumwa Nabii ila aliwaonya watu wake kutokana na mwongo wenye jicho moja.Fahamu kuwa ni mwenye jicho mojaNa Mola wako Mlezi si mwenye jicho moja.Na baina ya macho yake imeandikwa neno “kafiri”

Anas bin Malik bin Al-Nadr bin Damdam Al-Ansari

Anas bin Malik bin Al-Nadr bin Damdam Al-Ansari, Abu Hamza, imamu, mufti, msomaji, Mbobezi katika fani ya hadithi, msimuliaji wa Uislamu, Mtumishi wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, amani iwe juu yake, na wa mwisho kufa katika masahaba huko Basra. Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuja Madina akiwa na umri wa miaka kumi, na wakati Mtume anakufa Anasi alikuwa na umri wa miaka ishirini, na alikuwa akimtumikia Mtume, rehema na amani ziwe juu yake. Alishiriki vita pamoja na Mtume zaidi ya mara moja, na alimpa ahadi ya utii chini ya mti. Alipokea kutoka kwa Mtume elimu kubwa, Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake alimwombea dua ya mali nyingi na watoto, na shamba lake la mitende lilikuwa likipamba mara mbili kwa mwaka, alifariki mwaka: (93 AH) [1]


Marejeo

1.  Rejea ufafanuzi wake katika: “Sir Al-Alam Al-Nubala” cha Al-Dhahabi (4/417-423), “Ma`rifat Al-Sahaba” cha Abu Naim (1/231), “Kamusi ya Maswahaba. ” cha Al-Baghawi (1/43), “Asad Al-Ghaba” cha Ibn Al-Atheer (1/ 151-153).

Miradi ya Hadithi